Mipango ya kuwazuia Dr Slaa na Lowassa kugombea Urais yaiva.

Mipango ya kuwazuia Dr Slaa na Lowassa kugombea Urais yaiva.

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Njama zimesukwa kuhakikisha kwamba mgombea wa Urais mwenye nguvu zaidi Dr Wilbroad Slaa kutokea Chadema hapati nafasi ya kugombea Urais.

Wapanga mkakati huo wamepenyeza kifungu kwenye Rasimu ya Katiba mpya kinachosema mgombea Urais hapaswi kuwa ameshawahi kuwa mbunge kwa vipindi vitatu mfululizo.

Kifungu hicho ambacho wachunguzi wa mambo wanasema ni kifungu Kandamizi na cha kipuuzi kinawalenga pia wagombea Urais wenye nguvu kutoka CCM kama Edward Lowassa,Bernard Membe,Samwel Sitta na John Magufuli.

Endapo kipengele hicho kitapita kama kilivyo inaonekana wanasiasa watakaokuwa na sifa ya kugombea Urais ni pamoja na January Makamba,Emmanuel Nchimbi,Dr Asha Rose Migiro na wengineo wasiokuwa na majina makubwa.

Wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema walengwa wakuu wa kipengele hicho ni Dr Wilbroad Slaa na Edward Lowassa wanasiasa wenye nguvu kubwa ndani ya vyama vyao.

Hata hivyo swali la kujiuliza ni Je Tume ya Katiba ya Joseph Warioba ilikubali kusigina haki za watu kwa kununuliwa na wanasiasa uchwara?

Kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania baadhi ya wanasiasa ndani ya CCM wamekuwa wakipiga kelele kubwa kuhusu muundo wa serikali tatu ili kufunika kipengele hiki cha kijinga kisijadiliwe na hatimaye kipitishwe ndipo watu washtuke ambapo watakuwa wameshachelewa.

Source:Mtanzania Jumapili.
 
He! Hapo ndo ujue kuwa Jaji Warioba bado ni CCM damudamu na anafanya kazi kwa malengo ya CCM
 
Kamanda hivo ni porojo ambazo ni sawa na dua la kuku halimpati mwewe. Wanapoteza muda wao wasubirie Kimbunga tu.

 
mkuu molemo ondoa hofu kwani lazima wananchi wapige kura kukubari katiba wakiweka kipengere hicho ni elimu itolewe kwa wananchi waikatae katiba basi... tuendele na ya 77.

"Tatito la akili dogo kuongoza akili kubwa by mch msingwa"

TULIANZA NA MUNGU 2010
NA TUTAMALIZA NA MUNGU 2015
 
Unaonaje ukagombee wewe urais badala yake?


Mambo yanakwendaje Mkuu Lukosi, Huwa nashangaa sana kusoma posts na comments zako. Nadhani wakati umefika kuwa na Mtazamo wenye manufaa kwa taifa na sio kupanda meli ambayo inazama. Sio wewe Lukosi uliyetuhakikishia ushindi wa Kimbunga kule Arusha sasa unaonaje na yule jamaa uliyetaka kumlipia malazi London nipe kauli yako Kamanda nakukubali ingawa mengi natofautiana nawe
 
Ni mpuuzi tu atakaye toa pendekezo kama hilo na sidhani kama Tume watalikubali wazo hilo la kipuuzi liingie kwenye katiba.
 
Mbona unafikiri karibu sana mkuu hao uliowataja kwani ndiyo watanzania pekee acha utoto tanzania kunawatu zaidi ya milioni nne kwahiyo hawa wote uliowataja hata wasipogombea watanzania wenye sifa wapo wengi sana labda kama kunammoja wao kati ya hawa uliowataja anakulisha na amekutuma uje kuandika utoto wako humu.
 
Mawazo ya ovyo sana na hakuna justification inayo-make sense.Rascality of the highest order!
 
2015 for Lowassa, wengine wote ni wasindikizaji na wanatekeleza wajibu wao wa kikatiba
 
kama ni hivyo basi chama tawala kinaendelea kukosa direction!! hivi ni kweli au wewe uliyeleta thread hii ni wazo lako tu!!
 
slaa ni janga la taifa ataleta udini.iko kipengele poa kwel 2
 
ibara ya 123. mgombe ubunge lazima awe raia wa tanzania kwa miaka yote.
Unaoinaje ukimwambia haya NASSARI mbunge wa chadema?

Usitupe mawe kama unaishi nyumba ya kioo.

Ukumbuke kuwa katiba inabadilishwa na kuna kitu kinaitwa dual nationality. najua unanisema mimi na nakuhakikishia kuwa nitatimiza nia yangu
 
dr slaa ndio rais wetu iwe ni kwa kura itatosha ama aitatosha tumechoka kuburuzwa.
 
Njama zimesukwa kuhakikisha kwamba mgombea wa Urais mwenye nguvu zaidi Dr Wilbroad Slaa kutokea Chadema hapati nafasi ya kugombea Urais.

Wapanga mkakati huo wamepenyeza kifungu kwenye Rasimu ya Katiba mpya kinachosema mgombea Urais hapaswi kuwa ameshawahi kuwa mbunge kwa vipindi vitatu mfululizo.

Kifungu hicho ambacho wachunguzi wa mambo wanasema ni kifungu Kandamizi na cha kipuuzi kinawalenga pia wagombea Urais wenye nguvu kutoka CCM kama Edward Lowassa,Bernard Membe,Samwel Sitta na John Magufuli.

Endapo kipengele hicho kitapita kama kilivyo inaonekana wanasiasa watakaokuwa na sifa ya kugombea Urais ni pamoja na January Makamba,Emmanuel Nchimbi,Dr Asha Rose Migiro na wengineo wasiokuwa na majina makubwa.

Wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema walengwa wakuu wa kipengele hicho ni Dr Wilbroad Slaa na Edward Lowassa wanasiasa wenye nguvu kubwa ndani ya vyama vyao.

Hata hivyo swali la kujiuliza ni Je Tume ya Katiba ya Joseph Warioba ilikubali kusigina haki za watu kwa kununuliwa na wanasiasa uchwara?

Source:Mtanzania Jumapili.
Mkuu molemo sasa unazeeka vibaya kweli hoja kama hii inakupashida wakati tanzania kunawatu wote hawa mimi naamini tutapata mgombea mzuri tu hata wasipogombea hao wengine wote uliowataja.
 
kama ni hivyo basi chama tawala kinaendelea kukosa direction!! hivi ni kweli au wewe uliyeleta thread hii ni wazo lako tu!!

Mkuu gazeti la Mtanzania la leo limeeleta vizuri sana.
 
Hawataweza kupambana na dhoruba na mafuriko ya Mabadiliko ya kweli na haki. Waache watapetape tu hatma yao imewadia
 
Back
Top Bottom