Mipango ya serikali bora inatakiwa kutatua kiini cha matatizo yake. Miradi ya kimkakati ni changa la macho

Mipango ya serikali bora inatakiwa kutatua kiini cha matatizo yake. Miradi ya kimkakati ni changa la macho

DaudiAiko

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
372
Reaction score
310
Wanabodi,

Katika kipindi hiki, mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu, uchaguzi utakaotupa fursa kama wananchi kutafakari masuala mbalimbali yanayotuhusu kisiasa na kimaendeleo, hatuna budi kupasua kichwa tukiwaza jinsi ambavyo kama nchi tunaweza kujikwamua kutoka kwenye hali tuliyonayo sasa hivi.

Utagundua kwamba mbali na kura yako moja kama silaha, tumaini la kuwa na ushawishi wa kutosha kwenye maamuzi nyeti kwenye uendeshaji wa nchi yako ni finyu. Ukitilia hayo maanani, utakuwa na muonekano badala utakao kufanya uelewe kwamba “Miradi ya kimkakati” inachangia kidogo sana katika suala zima la kuikwamua serikali kiuchumi. Miradi hii inaweza ikaleta ahueni kwa wananchi kwa kupata huduma mbalimbali ambazo hazikuwepo katika kipindi cha awali lakini bado Tanzania ni nchi masikini na yenye wananchi wengi wenye kipato cha chini sana.

Niliyoeleza yana dhihirisha kwamba walio katika nafasi za juu serikali wanaweza wakawa wanatupooza kwa kutukumbusha kuhusu miradi ya kimkakati wakati kiini cha matatizo ya taifa kina uhusiano mdogo na miradi hiyo.

Tujiulize je, nchi yenye walipa kodi milioni mbili tu inawezaje kujikwamua kiuchumi?. Je uchaguzi ujao utatuletea viongozi na mipango ambayo itakuwa “Business as usual” au kuna “Risks” ambazo serikali itachukua kututoa tulipo sasa?. Je bajeti ya serikali ita fadhiliwa kwa misaada mpaka lini?.

Ninavyosema “Risks” nina maanisha kwamba serikali inaweza kuwekeza kwenye shughuli zinazo iingizia kipato wakati ikifanya miradi ya kimkakati. Katika hili, serikali haita tegemea kodi za wananchi tu kwasababu ya kipato hiki mbadala.

Inaweza ika “Monopolise” baadhi ya masoko nchini na kutengeneza bidhaa zinazo uzika kwa wananchi, au kutoa huduma ambazo haziwezi kutolewa na wafanyabiashara ilhali tuwe na serikali ambayo ni “active” na haitegemei mapato kutoka kwa walipa kodi tu. Hili pamoja na mambo mengine yanayoweza kufanywa yatahitaji ubunifu wa hali ya juu na ni risk kubwa kutekeleza. Cha muhimu kuelewa ni kwamba risk hizi zisipofanywa, tutabaki pale pale tulipo na hakuna kitakacho badilika

Mwisho, tuwe makini na ahadi tunazo pokea kutoka kwa wanasiasa kwasababu mara nyingi wanachotaka kutekeleza hakitatui kiini cha matatizo tuliyonayo.

Tuwe makini kwasababu maamuzi yetu hutiliwa maanani mara moja tu ndani ya miaka mitano. Nina amini kwamba tukitatua fumbo hili tutakuwa na mawaidha ya kutupeleka mbali sana.

Je Serikali ya Tanzania inaweza kuchukua hatua zipi kujiongezea kipato na kujikwamua kiuchumi?
 
"60% ya watumishi waliopo serikalini hawana uwezo"Prof Asad.

Ni ngumu sana kupata viongozi wenye maoni ikiwa tuna mfumo wa hovyo wa kuandaa viongozi katika nafasi nyeti.leo sifa ya kupata nafasi ni connection na sio uwezo,kwa namna hii kufikia nafasi nzuri ya makusanyo ni ndoto za alinacha.
 
Wanabodi,

Katika kipindi hiki, mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu, uchaguzi utakaotupa fursa kama wananchi kutafakari masuala mbalimbali yanayotuhusu kisiasa na kimaendeleo, hatuna budi kupasua kichwa tukiwaza jinsi ambavyo kama nchi tunaweza kujikwamua kutoka kwenye hali tuliyonayo sasa hivi.

Utagundua kwamba mbali na kura yako moja kama silaha, tumaini la kuwa na ushawishi wa kutosha kwenye maamuzi nyeti kwenye uendeshaji wa nchi yako ni finyu. Ukitilia hayo maanani, utakuwa na muonekano badala utakao kufanya uelewe kwamba “Miradi ya kimkakati” inachangia kidogo sana katika suala zima la kuikwamua serikali kiuchumi. Miradi hii inaweza ikaleta ahueni kwa wananchi kwa kupata huduma mbalimbali ambazo hazikuwepo katika kipindi cha awali lakini bado Tanzania ni nchi masikini na yenye wananchi wengi wenye kipato cha chini sana.

Niliyoeleza yana dhihirisha kwamba walio katika nafasi za juu serikali wanaweza wakawa wanatupooza kwa kutukumbusha kuhusu miradi ya kimkakati wakati kiini cha matatizo ya taifa kina uhusiano mdogo na miradi hiyo.

Tujiulize je, nchi yenye walipa kodi milioni mbili tu inawezaje kujikwamua kiuchumi?. Je uchaguzi ujao utatuletea viongozi na mipango ambayo itakuwa “Business as usual” au kuna “Risks” ambazo serikali itachukua kututoa tulipo sasa?. Je bajeti ya serikali ita fadhiliwa kwa misaada mpaka lini?.

Ninavyosema “Risks” nina maanisha kwamba serikali inaweza kuwekeza kwenye shughuli zinazo iingizia kipato wakati ikifanya miradi ya kimkakati. Katika hili, serikali haita tegemea kodi za wananchi tu kwasababu ya kipato hiki mbadala.

Inaweza ika “Monopolise” baadhi ya masoko nchini na kutengeneza bidhaa zinazo uzika kwa wananchi, au kutoa huduma ambazo haziwezi kutolewa na wafanyabiashara ilhali tuwe na serikali ambayo ni “active” na haitegemei mapato kutoka kwa walipa kodi tu. Hili pamoja na mambo mengine yanayoweza kufanywa yatahitaji ubunifu wa hali ya juu na ni risk kubwa kutekeleza. Cha muhimu kuelewa ni kwamba risk hizi zisipofanywa, tutabaki pale pale tulipo na hakuna kitakacho badilika

Mwisho, tuwe makini na ahadi tunazo pokea kutoka kwa wanasiasa kwasababu mara nyingi wanachotaka kutekeleza hakitatui kiini cha matatizo tuliyonayo.

Tuwe makini kwasababu maamuzi yetu hutiliwa maanani mara moja tu ndani ya miaka mitano. Nina amini kwamba tukitatua fumbo hili tutakuwa na mawaidha ya kutupeleka mbali sana.

Je Serikali ya Tanzania inaweza kuchukua hatua zipi kujiongezea kipato na kujikwamua kiuchumi?
Tatizo ni jamii kuto buni mbinu za kukabiliana na changamito tulizo nazo na zitakazo kuja hapo baadae tunategemea watu wachache wanaopewa dhamana ambao wengi wao ni wajinga, (nyumbu)

Unyumbu wa kisiasa ni tabia ya baadhi ya watu wanao pewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza, kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi na uoga kwa viongozi wao bila utii, (unafiki), a.k.a kujizima data ama kuahirisha kufikiri kizalendo, (uchawa)
 
Sahihi kabisa, miradi ya kimkakati kimsingi ni commissions tu zinatengenezwa zikafichwe Uswiss na Jersey kule. Kwa mfano kwa mtu makini kuweka matrilioni kwnye SGR inayohudumia watu 4000 kwa siku sio tu ni wendawazimu bali ni kichaa kamili, mwenye busara angejengea barabara nchi nzima kila kona na kuweka viwanda vya kilimo ingekuwa na impact kwa watu 20-40 miliion na ingesisimua uchumi vya kutosha na ndani miaka 5-6 angepata faida ya kujenga SGR nchi nzima bila hata kukopa. Ila nashukuru wanawapa wazungu uwezo wa kutukopesha tena, maana haohao wanarudi kukopa pesa zao walizoweka tena kwa riba kubwa sana.
 
Sahihi kabisa, miradi ya kimkakati kimsingi ni commissions tu zinatengenezwa zikafichwe Uswiss na Jersey kule. Kwa mfano kwa mtu makini kuweka matrilioni kwnye SGR inayohudumia watu 4000 kwa siku sio tu ni wendawazimu bali ni kichaa kamili, mwenye busara angejengea barabara nchi nzima kila kona na kuweka viwanda vya kilimo ingekuwa na impact kwa watu 20-40 miliion na ingesisimua uchumi vya kutosha na ndani miaka 5-6 angepata faida ya kujenga SGR nchi nzima bila hata kukopa. Ila nashukuru wanawapa wazungu uwezo wa kutukopesha tena, maana haohao wanarudi kukopa pesa zao walizoweka tena kwa riba kubwa sana.
Wanaopewa dhamana ni wajinga sana, baadhi huahirisha kufikiri kizalendo, a.k.a kujizima data
 
Back
Top Bottom