Mirathi

Ang'ino

Member
Joined
Jun 9, 2013
Posts
42
Reaction score
8
Wanajamvi naombeni Ushauri kuhusu taratibu za kufungua Mirathi,nimepewa jukumu la kuwa msimamizi wa Mirathi ya Shemeji yangu ambaye alikuwa mwajiriwa na kuna mali alizopata baada ya mauti ya mumewe ambaye ni kaka yangu. Je, inawezekana kufungua Mirathi ya mwanamke ukizingatia walioana na ndoa inatambulika kisheria? Mali za Marehemu Kaka yangu zishafunguliwa Mirathi.Huyu Shemeji yangu ana mtoto mmoja wa kike ambaye kwa mujibu wa vikao vya familia ndiye MRITHI wa mali za mama yake.
Zingatia: Marehemu kaka alikuwa na wake wawili,mmoja marehemu mwingine yuko hai na alimjengea kila mmoja wa wake zake nyumba ya kuishi inayojitegemea.
 
Mirathi lazima ifunguliwe.
Kikao cha ukoo kinatakiwa kiteue msimamizi wa mirathi hiyo,muandike muhtasari.
Nendeni mahakamani kufungua shauri la mirathi ambatanisha hati ya kifo na muhtasari wa kikao cha ukoo.
Huo ndo ushauri wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…