KERO Misafara imekua kero, Raia wanazuiwa muda mrefu kupisha misafara

KERO Misafara imekua kero, Raia wanazuiwa muda mrefu kupisha misafara

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

mirindimo

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2009
Posts
901
Reaction score
1,742
Anandika Khamis Kagasheki.

Ninaona usumbufu wa kufunga barabara na kusimamisha magari unazidi kuwa mkubwa. Ukiuliza unajibiwa "msafara." Tatizo hili limekuwa likiongezeka lakini kwa sasa limekuwa kero hapa Dar es Salaam.

Tarehe 7 July 1963 (Saba Saba Day) katika kilele cha cha sherehe za kuzaliwa TANU, Baba wa Taifa alihutubia Taifa kuhusu "Mbwembwe."

Tarehe 13 July 1963, Mwalimu aliwaandikia mawaziri wake wote na makatibu wakuu wote akiwaonya kuhusu jambo hilo la "mbwembwe." Kuhusu "police escorts" Mwalimu aliandika, "kabla hatujaingia serikalini kulikuwa na utulivu barabarani, lakini baada ya kuingia serikalini, hatuendi popote bila police escort." Aliendelea, " zipo nyakati escort inahitajika" na akailenga kwa Rais na Makamu wa Rais/Waziri Mkuu. Akaendelea kuandika, "the President of Tanganyika is fast becoming the worst public nuisance the City of Dar es Salaam has ever to put up with! Whenever he decides to out, whether to a dinner, a dance, or even to visit some friends, the normal flow of traffic has now to be interfered with...it is rapidly becoming impossible for anybody in Dar es Salaam to guess how long it will take him to drive from A to point B..." Hii ilikuwa 1963.

Leo asubuhi (Alkhamis) barabara nyingi maeneo ya Oysterbay zilikuwa zimefungwa na magari kusimamishwa kwa zaidi ya dakika 25. Pia naona wapo maaskari wanaokwenda mbali zaidi kwa kusimamisha baadhi wa raia.

Jana (Jumatano) barabara ya Ali Hassan Mwinyi (mida ya kuanzia saa kumi/kumi na moja) magari yamesimamishwa zaidi ya dakika 20. Sijui kama ilikuwa msafara au traffic officer.

Uslama wa viongozi wetu ni kipaumbele muhimu lakini tuzingatie humu barabarani sio wagonjwa wote husafiri kwa ambulance kwa maana ya ving'ora. Humu barabarani wamo watu wagonjwa, watu wazima wanaokabiliwa na changamoto nyingi za kiafya. Bahati mbaya wapo maofariki ndani ya magari wakipelekwa hospitali.

Escorts zimekuwa nyingi barabarani. Sitaki kutoa judgment lakini naomba sana mtazame ni watu gani wanastahili privilege hii.

Soma Pia: Wananchi wa Korogwe tunakereka kusimamishwa muda mrefu barabarani ili kupisha misafara ya viongozi wa Siasa, hii sio sawa

Barabara zetu ni kila kitu kwetu. Kufunga barabara dakika 20 au nusu au zaidi, uchumi wa taifa unaathirika kwa kiasi gani? Appointments za watu mbali mbali zina athirika kiasi gani.

Kuandika haya simfundishi mtu yeyote kazi yake lakini ninakumbusha tu.

Kazi njema.
 
Mzee wetu Hamis Kagasheki mtu wa Ukweli daima, Mhaya usiyepindisha maneno, Mhaya uliyenyoooka kama rula.

Wahenga tunakumbuka ulivyowanyoosha WAHUNI na OPARESHENI TOKOMEZA UJANGILI. uliwanyooosha wahuni wakala mitama, wakavuliwa nguo, wakaaibika wakaona isiwe shida wakafanya comeback wakakuundia zengwe kwamba OPARESHENI yako imekiuka haki za binadamu, oparesheni yako imevunja sheria na blaa blaa nyingi hatimaye wakakushusha.

Wafia Nchi tunakujua mzee Kagasheki, tunajua kwa sasa unakereka na mengi, hupendi mbambambaaa, hili la Foleni za viongozi wakienda Dinner ni tonne tu umetoa lkn moyoni una mengi. Watanzania wanasiri. Wakati utaongea mzee wangu pumzika salama.
 
Fundisho kwa machawa!
Walikuwa kama sisi, baada ya kura zetu WANATUOGOPA, WANATUDHARAU, WANATUONA HATUNA MAANA, GHAFLA WAMEKUWA MIUNGU MITU!
 
Baridi unalisikia ukiwa nje ya maji lakini ukiwa ndani ya maji unamshangaa anayesema kuna baridi, Mhe. Mbona hili tatizo ni la miaka mingi tu hata kabla ya wewe hujaingia serikalini? au ulipanga kulisemea baada kutoka serikalini?
 
Anandika Khamis Kagasheki......
Ninaona usumbufu wa kufunga barabara na kusimamisha magari unazidi kuwa mkubwa. Ukiuliza unajibiwa "msafara." Tatizo hili limekuwa likiongezeka lakini kwa sasa limekuwa kero hapa Dar es Salaam...
Mbaya sana kuna jamaa yangu aliambia juzi jumanne maeneo ya mkata walisimamishwa dk 45 kusubiri msafara wa magari mawili tu!
 
Inakera siku hizi hadi Sana 11 alfajiri mnasimamishwa weee sijui wanakuwa wanaenda wapi usiku usiku hivyo!!!
 
Anandika Khamis Kagasheki......
Ninaona usumbufu wa kufunga barabara na kusimamisha magari unazidi kuwa mkubwa. Ukiuliza unajibiwa "msafara." Tatizo hili limekuwa likiongezeka lakini kwa sasa limekuwa kero hapa Dar es Salaam...

Na Ukipiga picha msafara kwa sababu unakereka UNATEKWA.
 
Anandika Khamis Kagasheki......
Ninaona usumbufu wa kufunga barabara na kusimamisha magari unazidi kuwa mkubwa. Ukiuliza unajibiwa "msafara." Tatizo hili limekuwa likiongezeka lakini kwa sasa limekuwa kero hapa Dar es Salaam...
Kabisa yote hayo ni kwa sababu ya CCM kuwa madarakani.
 
Anandika Khamis Kagasheki......
Ninaona usumbufu wa kufunga barabara na kusimamisha magari unazidi kuwa mkubwa. Ukiuliza unajibiwa "msafara." Tatizo hili limekuwa likiongezeka lakini kwa sasa limekuwa kero hapa Dar es Salaam...
Nasikia hata Makonda nae ana msafara
 
Hili ni la kutukia akili zaidi kama mhusika hana threat yeyote haina haja ya kusimamisha watu.

Kuna misafara na kuna haya mavx meusi yenye taa juu za vingora yamekiwa kero na yanasababisha ajali sana mitaani.

Ifike wakati sasa highway engineers wafikirie kujenga barabara pana zaidi ili hawa wala nchi wapite kwa haraka

Mji mkuu umeamia dodoma lakini kila siku hapa dsm. Kuna siku oysterbay inafungwa kuanzia coco beach mpaka st peter hakuna kupita mtu.

Kuna measure ya productivity kwa hawa watawala kweli.
 
Wanachezea raia tu na mbwembwe zao! Wanachezea hela, muda, kwa ulimbukeni wao!
 
Mzee wetu Hamis Kagasheki mtu wa Ukweli daima, Mhaya usiyepindisha maneno, Mhaya uliyenyoooka kama rula.

Hana lolote, angekuwa hapindishi maneno angelisema hili ndani ya Cabinet ya Kikwete. Au angeleta muswada bungeni wakati wake.

What the freak did you do about this freaking traffic disaster when you had the power, when you had the platform, you had access to highest leaders, to parliament, to cabinet ?

What the freak did you do ??????
 
Back
Top Bottom