1. Kisado -- Bidhaa ni rangi ya nyumba, ya kampuni ya Sadolin. Walikuwa wakiweka kwenye makopo ya ukubwa fulani yaliyopachikwa jina la "visadolini" au "visado".
2. Kimbweta - Kiti na meza cha zege, mara nyingi huwapo kwenye taasisi za elimu ya juu. Vilibuniwa na Prof. Mbwette. Wengine huviita Vimbwete.
3. Wekundu wa Msimbazi -- Timu ya Simba Sc. ilianza kutamkwa hivyo na Isaac Muyenjwa Gamba, alipokuwa mtangazaji katika kipindi cha michezo cha redio moja hapa nchini.
4. Ongezea misemo mingine tafadhali.