Ndugu Katavi,
Salaam. Nimekupigia rununu yako bila majibu. Nilitaka nikufahamishe hitimisho la sakata ya kanguvuke ya Dowans kama ilivyojadiliwa bungeni.
Suala limejadili bila weledi na hii inanipa kihoro kuhusu hatima ya mgao wa umeme. Kwa mintaarafu ya yaliyojiri imebidi iundwe kamati ndogo ya kamati ya madini ili kuanzisha taftishi, na haiyumkiniki kuwa muktadha wa jambo hili utakuwa katika siku za usoni.
Nimeona katika runinga aina mpya ya ngamizi zenye baobonye ambazo puku zake hazitumii waya. Nimepewa dokezo kuwa kinakishi na nukushi vinapatikana kisutu madukani mkabala na jengo la mfuko wa jamii. Jaribu kutembelea wavuti ya JF ili kubaini uwezo wa kichaka matini yake kabla hujaagiza.
Usisahau kumwambia bujibuji ujumbe wake murua nimeupata. Ukiweza kumtia machoni Dena Amsi muulize kulikoni? ni muda sijasikia kutoka kwake. Vipi unategmea kuhudhuri kongamano aliloaanda Lizzy, mimi nitakuwa na warsha na nadhani AD, Hapanuchi nao watajumuika nami.
Tadhali usomapo ujumbe huu naomba usuli. Wajulie hali akina invisible, malaria sugu na Masanilo. Nasikia hamkani si shwari kwao walipata ban je ni kweli. Nasikia pia MMU wanaomba uanisho mtu anapofungiwa, je mchakato wa suala hilo umeshamfikia Melo.
Maslaam
Kaka Nguruvi.