Misemo ya makonda wa Daladala

Abiria: We konda kuna siti humo?

Konda: Zipo bi mkubwa, choma ndani, unaenda wapi?

Abiria: Magomeni

Konda: Fungua nauli kabisa...........................poapoa, haya rudi nyuma

Abiria: We konda mbona sizioni siti?

Konda: Acha masihara bi mkubwa, hao wenzako wamekalia mawe kwani?
 
Abiria: nishushe hapo hapo mbele

Konda: nani akushushe!,shuka mwenyewe..kwani mi ndo niliyekupandisha?

Hapo tayari kashachukua nauli yake kitambo sana,huwezi kusikia kauli kama hii ikiwa bado hajachukua nauli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…