Naona una kasumba ya wabongo kuchukia ukweli ama umehamua tu kuwa mbishi wa kuelewa vitu. Toka lini kusema ukweli kukawa ni tatizo ama kuponda kitu? Kuwa mzalendo si lazima upende hata upuuzi ila unatakiwa pia kukosoa kwa niaba ya wahusika na ndicho nilichokifanya, je kuna kosa? Unajuwa wewe na mimi tunaweza kuangalia kitu kwenye TV na tukawa na mawazo tofauti kabisa ya tulichokiona. Mimi naweza kufagilia tulichokiona wewe ukaponda na pengine sote tukawa hatuna point katika kusifia na ukosoaji wetu. Sasa nikuulize wewe Mpoki, kwa sisi kuwa na mawazo tofauti ya tulichokiona ni kukosa uzalendo ama? Ishu hapa ni kwamba ninashangazwa na acting ya Ze Comedy, kwangu haichekeshi hata kidogo kwani acting yao is pathetic to me. Umeelewa mpaka hapo ama nirudie? Na nikasema ninashangazwa na uchekeshaji wao kwani ni wa ngumbalu, maana ngumbalu ndipo unakuta jokes kama zile za Mpoki. Sasa hapa kosa ni lipi? Na nikaongeza kusema kwamba nafurahia series zingine za kibongo kama Mze Small na King Majuto pamoja na zingine kwani zinachekesha. Sikusifia sinema hata moja ya nje ya Tanzania, sijuwi mwenzangu umeona wapi hayo maneno niliyoandika wakati hayapo, ebu naomba uniambie. Usitoe vitu tu kwenye mawazo yako finyu na kusema fulani kasema wakati si kweli. Usiwe mvivu wa kusoma na kuelewa vitu, soma na uelewe ndipo utoe mada usikurupukie tu kujibu watu ili upate kuonekana kwenye quotes.