Wakuu habari,
Gari tajwa hapo juu ilikua na nguvu sana ila ilianza kuua nosel moja ikawa na mis, sasa nikabadili nosel na ikawa poa kabisa.
Jana imeanza tena mis plug no moja haichomi vizuri na kuna time haichomi kabisa.
Fundi amejaribu kuweka plug mpya bado, amekagua fuel pump iko ok, amechek distributor iko njema na mfumo wote wa umeme umekaa sawa ila bado tatizo la misfire lipo kwa mbali hivyo gari kukosa nguvu japo sio sana.
Sasa kuna fundi wa mtaani ananiambia kuwa tatizo litakua kwenye engene tuifungue tusafishe/ tusage valve kumaliza hilo tatizo.
Je wataalam mna mawazo gani anaweza kuwa sahihi.
Gari ni ya petrol