Eli Cohen
JF-Expert Member
- Jun 19, 2023
- 4,460
- 13,715
Misiba yetu huwa ni event fupi yenye mambo mengi ya ajabu, yakuchekesha, kuhudhunisha na kustajaabisha.
Misibani huwa ndio fursa nzuri kwa ajili ya wambea na wanafiki. Wanatunga stori kuhusu kifo na maisha ya familia yenye msiba. Unakuta kuna vikundi vikundi vya wakina mama, vya wakina baba, wengine mchanganyiko kila kikundi kikiwa na stori yake ya chanzo cha kifo cha marehemu. Akifa baba utasikia mama ndio amemuua.
Misibani ndio pesa humwaga nyingi angali marehemu alipokuwa mgonjwa walikuwa wakilia ukata na huku watafuta sifa wakijionesha kufanya vikazi na kutoa michango ili jamii iwaone na wenyewe wamo.
Huku unakuta vijana vugu vugu limeanza kuhusiana na mgawanyo wa mali. Na wale wa uke wenza ndio shida balaa, kila mama anavutia kwake huku mke mkubwa akidai vikubwa kwa maana ndio ameanza ku-hustle na baba na huku mke mdogo akisema kuwa baba amefia kwake na yeye ndio amemuuguza na amemtakia yeye apate vitu fulani na fulani.
Misibani huwa ndio fursa nzuri kwa ajili ya wambea na wanafiki. Wanatunga stori kuhusu kifo na maisha ya familia yenye msiba. Unakuta kuna vikundi vikundi vya wakina mama, vya wakina baba, wengine mchanganyiko kila kikundi kikiwa na stori yake ya chanzo cha kifo cha marehemu. Akifa baba utasikia mama ndio amemuua.
Misibani ndio pesa humwaga nyingi angali marehemu alipokuwa mgonjwa walikuwa wakilia ukata na huku watafuta sifa wakijionesha kufanya vikazi na kutoa michango ili jamii iwaone na wenyewe wamo.
Huku unakuta vijana vugu vugu limeanza kuhusiana na mgawanyo wa mali. Na wale wa uke wenza ndio shida balaa, kila mama anavutia kwake huku mke mkubwa akidai vikubwa kwa maana ndio ameanza ku-hustle na baba na huku mke mdogo akisema kuwa baba amefia kwake na yeye ndio amemuuguza na amemtakia yeye apate vitu fulani na fulani.