Uchaguzi 2020 Misingi imara ambayo Mwl. Julius Nyerere aliwaachia watanzania imesababisha CHADEMA ipoteane wakati wa kampeni

Uchaguzi 2020 Misingi imara ambayo Mwl. Julius Nyerere aliwaachia watanzania imesababisha CHADEMA ipoteane wakati wa kampeni

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Kwa sasa kama ni kwenye mpira unaweza kusema CHADEMA wamepoteana. Maana hawajui mpira waanzie wapi! Waanzie pembeni nyuma au waanzie mbele. Maana kila hoja wanayoibua imeonekana ni hoja mfu na haiuziki.

Lakini yote ya haya yanayowakuta CHADEMA ni kwa sababu muasisi wa taifa letu Mwl Julius kambarage Nyererea aliacha misingi imara ndani ya mioyo ya Watanzania. Na misingi hiyo ni kuwa wazalendo. Maana taifa huwa linajengwa ndani ya mioyo ya wanananchi wake.

Kwa uzalendo walionao watanzania kila hoja ambayo imekuwa ikiibuliwa na CHADEMA wamekuwa wakiipuuza na kuwaona kuwa hawafai. Mfano walikuja na hoja ya kuwa hivi sasa kinachofanyika ni maendeleo ya vitu na sio watu. Kwa uzalendo wa watanzania, CHADEMA imepuuzwa sana. Maana huwezi kusema ujenzi wa kituo cha afya au barabara sio maendeleo ya watu, maana vinajengwa ili vitumiwe na watu.

Walikuja na hoja ya kipuuzi eti kujenga miundo mbinu,shule na hospital si kitu si chochote. Maana hata mkoloni alijenga. Pia walienda mbali na kudai eti, maendeleo katika sekta hizi hayana maana sababu hivi sasa hakuna uhuru. Maneno haya yamewaudhi sana watanzania wazalendo. Yaani CHADEMA hawajui kuwa mkoloni alikuwa anatunyonya kwa kila kitu? Kuwa alijenga miundo mbinu sehemu ambazo alikuwa na maslahi, kama sehemu ambazo kuna malighafi. Na kuhusu uhuru unaweza kusema hakuna uhuru hapa Tanzania? Watu wanafanya shughuli na kujadili mambo usiku na mchana!

Wamekuja kuona wamebugi wakaja na hoja ya bima ya afya kwa kila mtanzania. Watu wakahoji mtaitekeleza vipi? Wakakosa majibu. Kumbe ilani ya CCM imelitanabaisha hili suala vizuri kabisa na limewekwa wazi namna ambavyo litatekelezwa. Hapo ndio wameishiwa nguvu.

Kuharibu kabisa pale walipowadhalilisha watanzania kuwa nchi hii inalishwa kila kitu na mabeberu. Hili limewakera sana watanzania. Sababu misingi aliyoiacha mwl Nyerere ni kuwa taifa linalojitegemea. Ndio maana ukienda kila kona watanzania wanajishulisha na kilimo,biashara na ufugaji. Na hii imewavunja nguvu CHADEMA maana wananchi wamewapuuza sana. Hata moto walionza nao kwenye kampeni umeanza kufifia.
 
Ni vigumu saana kwa watanzania kuchagua upinzani hii inasababishwa na mfumo wa kijamaa

watanzania wengi wanaamini wapinzani wapo kwa maslahi ya wazungu
 
Ni vigumu saana kwa watanzania kuchagua upinzani hii inasababishwa na mfumo wa kijamaa

watanzania wengi wanaamini wapinzani wapo kwa maslahi ya wazungu
Nafikiri ishu sio ujamaa,bali umakini wa Ccm unawamaliza hawa wapinzani.
 
Nyerere mnamjua nyinyi ccm? Mngembambika sanamu yenye sura isiyo yake
IMG_20200906_113622.jpg
 
Mkiwa hamna hoja acheni wengine waandike!Ika ukitaka kuandika wewe tu mwisho wa siku unajikuta unaandika vitu vya kawaida kabisa ambavyo unadhani ni propaganda yenye uhai,kumbe watu wanakuona ni "walewale"!
Hakuna hoja ya msingi hapo?
 
Wananchi hawataki wagombea ambao hawajui shida zao; wagombea ambao wanaonekana kipindi cha kampeni tu. JPM analazimisha wananchi kuchagua ccm kwa nguvu, haiwezekani.
Mwananchi jua wewe ndio mwenye nguvu kipindi hiki, zitumie nguvu zako vizuri kuleta mabadiliko.
 
Mbona huyu anajenga miundombinu sehemu zenye wabunge wa ccm, hujasikia alichosema kule Mara?
 
Bila kujadili itikadi ya chama unapozungumzia maendeleo ya vitu na watu jikite katika hicho unachozungumzia iwapo kina matokeo ya moja kwa moja ya kila maisha ya mtanzania. Usipotoshe unapozungumzia shule, huduma za afya mfano hospitali au au barabara vijijini. Hivyo ni vitu ila impact yake ni kubwa katika kuondoa maradhi ujinga na umaskini katika maisha ya mtanzania .Kama muelewa bila kujali kuwa yanaongelewa na nani tusiwapotoshe watanzania. Hakuna chama kinachopiga vita uwepo au kuelekeza kodi za watanzania katika miundo mbinu hiyo. Aidha unapotosha kupitia bandiko lako ambalo kwa mtu mwenye uelewa ndio mbinu inayotumiwa na hao wanaopotosha watu au maana nimesema aidha hujaelewa ni nini alichomaanisha Muasisi wa Taifa hili.
 
Hawapendi maendeleo.. wanafikiria hizo pesa zilizotumika.. zinawaumaaa.. kwa wao zingeingia mikononi mwao.. miundo mbinu n.k. ni kitu mojawapo.. vizuri.. ambavyo vinarahisisha.. mwananchi aweze kufanya mengi kiurahisi.. na kujiongezea kipato..
 
Bila kujadili itikadi ya chama unapozungumzia maendeleo ya vitu na watu jikite katika hicho unachozungumzia iwapo kina matokeo ya moja kwa moja ya kila maisha ya mtanzania. Usipotoshe unapozungumzia shule, huduma za afya mfano hospitali au au barabara vijijini. Hivyo ni vitu ila impact yake ni kubwa katika kuondoa maradhi ujinga na umaskini katika maisha ya mtanzania .Kama muelewa bila kujali kuwa yanaongelewa na nani tusiwapotoshe watanzania. Hakuna chama kinachopiga vita uwepo au kuelekeza kodi za watanzania katika miundo mbinu hiyo. Aidha unapotosha kupitia bandiko lako ambalo kwa mtu mwenye uelewa ndio mbinu inayotumiwa na hao wanaopotosha watu au maana nimesema aidha hujaelewa ni nini alichomaanisha Muasisi wa Taifa hili.
Nini umeandika?
 
Tungekuwa tumepanic tungemkokota Mama Maria Nyerere aje kutuombea kura hadi akaishia kusema amelazimishwa.
Ahaaaa. Msipotoshe umma mama wa taifa alikuja kwa nia njema tu. Hakulazimishwa na heshima kubwa kuwa nae pale uwanjani.
 
Back
Top Bottom