Misingi ya ndoa Migumu sana

kidaganda

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2013
Posts
2,995
Reaction score
2,572
Misingi mingine ya ndoa zetu ni migumu sana.
Pata simulizi hii toka Marekani.

PhupySmith na mkewe hawajawahi kuwa na mzozo ndani ya miaka 25 ya ndoa yao. Jambo hili likamfanya jirani yao mmoja kumuuliza PhupySmith amewezaje kuishi na mkewe muda huo wote bila kuzozana!

PhupySmith anaeleza:
[emoji117] Tulienda fungate Australia miaka 25 iliyopita,
Wakati mke wangu akiwa amempanda farasi,
Farasi aliruka na mke wangu akaanguka,
Aliamka, akampigapiga farasi kwa upole, akasema,
"hii ni mara yako ya kwanza",
Baada ya muda ikatokea tena,
Alimpigapiga tena na kusema,
"hii ni mara yako ya pili",
Farasi alifanya tena mara ya tatu,
Mke wangu alitoa silaha na kumuua yule farasi,
Nilishitushwa sana na kitendo kile nikamgombeza sana mke wangu,
- umechanganyikiwa?,
- una matatizo gani?,
- kwa nini umemuua farasi?,
Mke wangu aliniangalia, akatabasamu, kisha akasema,
"hii ni mara yako ya kwanza",
Tangu siku hiyo nikaushona mdomo wangu,
Hii ndiyo siri ya kuishi miaka yote hii bila kuzozana...! [emoji118]
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Hahahahahaha. Jamaa akaogopa. Ila kuushona mdomo sio dawa, akizingua unamchana tu, akimind poa. Atalia, atanuna lakn moyo wko tayar utakuw na amani kwmb amejua usichokipenda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…