01': Mechi imeanza na Masry wamekuwa wa kwanza kufika katika lango la Simba. Manula yuko makini
03': Simba wanamuachia Mohammed kupiga kichwa akiwa peke yake, hakulenga
06': Kuna faulo karibu kabisa na lango la Simba, ni hatariDk 6 sasa, Simba wamerudi nyuma na wanalinda zaidi ya kushambulia
07': pira mkali wa faulo, Kapombe anaokoa kwa kichwa na sasa yuko chini pale, anaanza kutibiwa
08': Kapombe anatolewa nje kwa ajili ya kutibiwa zaidi
09': Kuna mchezaji wa Al Masry yuko chini, tatizo la nyama, MPIRA UMESIMAMA
11': Bado mchezaji yule hajatolewa na Manula amekuwa akimulikwa na mwanga wa kijani ili kumchanganya, hawa ni mashabiki
12': Mpira umeanza na yule mchezaji ametolewa
SUB: Anaingia Bance kuchukua nafasi ya Ahmed Gomaa aliyeumia
15': Okwi alimchambua beki na kutoa pasi kwa Kapombe lakini alikuwa amevutwa na kuangushwa
17': Krosi safi ndani ya lango la Simba lakini Simba wako makini, mpira ni goal kick
20': Manula analala chini pale inaonekana aliumia wakati aliporuka kuokoa
21': Bocco anaingiza krosi safi kabisa lakini Okwi anachelewa na mpira unakuwa goal kick
23': Mpira umesimama, Gyan amegongana na Hamty wa Al Masry na wote wanatibiwa
25': Hatari kwenye lango la Simba lakini Manula anaruka na kudaka mbele ya Bance
26': Manula anafanya kazi ya ziada kudaka mpira mbele ya Mustapha, ilikuwa krosi hatari ndani ya lango la Simba
27': Okwi anawekwa chini hapa na mpira unapigwa kwenda Masry
28': Kipa wa Masry anaruka juu na kuudaka mpira kama nyani baada ya krosi ya Gyan
29':Bance anakwenda vizuri lakini Mkude anamuwahi na kuchukua mpira
30': Masry wanapata kona ya kwanza, inachongwa hatariiii, goal kick
34': Bado Masry wanapata kona baada ya krosi hatari kabisa
35': Kona inachongwa Kwasi anaruka na kuokoa, kona tena inachongwa Simba wanaokoa
36': Bance anawachomoka Simba, anaachia mkwaju mkali hapa, Manula anadaka kwa ustadi
39': Mlipili analazimika kumlza chini Salam katika eneo hatari baada ya Gyan kupoteza mpira
41': Kuna vurugu zinaendelea na wachezaji wanafukuzana na kurushiana mikono mpira umezimama
43': Kuna faulo karibu kabisa na Simba baada Kotei kugongana na Gomaa wakati wakiwania mpira
44': Nyoni analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Glindo
45': Dakika 3 za Nyongeza nimeonyeshwa
MPIRA MAPUMZIKO (AL MASRY 0 - 0 SIMBA)
Timu zimerudi uwanjani
45': Kipindi cha pili kinaanza hapa
48': Masry wanapata faulo karibu kabisa na lango la Simba, si eneo salama
49': Manula anaruka na kuokoa, ilikuwa hatari kabisa
51': sasa, Masry wanaonekana kuwa na kasi lakini bado Simba wanalinda zaidi
Manula anafanya kazi ya ziada kuruka na kuokoa mpira juu ya kichwa cha Mustapha
53': Mkude anaonyeshwa kadi ya njano kwa kumuangusha Mohammed
54': Inachongwa faulo, Gyan anaokoa na kuwa kona ya kwanza kipindi cha pili
55': Hatari kwenye lango la Simba, Manula anagongwa lakini mwamuzi hakuona huenda, mpira unapigwa lango la Simba likiwa tupu, goal kick
56': Gyan anaachia mkwaju mkali kabisa, unatoka pembeni kidogo ya lango la Masry, ilikuwa hatari
59: Mohammed wa Masry anajiangusha na mwamuzi anasema faulo
Hatari kwenye lango la Simba, mpira unatoka pembeni kidogo
61': Kwasi anajaribu mkwaju, goal kick
63': Manula anagonjwa wakati akijaribu kuokoa na sasa yuko chini na mchezaji mmoja wa Masry yuko chini pia
SUB. 66': Simba wanafanya mabadiliko, anaingia Mavugo kuchukua nafasi ya Mlipili
67': Okwi anawekwa chini, mwamuzi anasema twende, sijaona
Kotei naye anafanyiwa madhambi, mwamuzi anasema sijaona twende. Wachezaji wa Simba wanaonekana kukasirishwa wanamfuata mwamuzi na yeye anamuita Okwi na kumuonya asiendele kumlaumu. Kotei bado anatibiwa
68': Sasa, Gyan naye yuko chini pale akitibiwa huku mashabiki wa Masri wakiendelea kuzomea
69': Okwi anaingia vizuri na kuachia mkwaju mzuri hapa, mabeki wa masry wanaondosha hatari
71': Simba wanaonekana kuanza kufunguka na kushambulia
72': Kotei anafanya kazi ya ziada kumzia bance na mpira unakuwa wa kurushwa
SUB! 73': Simba wanamtoa Kotei na nafasi yake inachukuliwa na Shiza Kichuya
75': Simba wanaonekana kuanza kufunguka, wanashambulia na Gyan anaachia mkwaju mkali hapa lakini goal kick
78': Mkude anaachia mkwaju mkali hapa lakini hakulenga
79': Mavugo ndani ya 18, anaachia mkwaju mkali lakini kipa anaonyesha ujuzi mkubwa anadaka ilikuwa nafasi nzuri zaidi kwa Simba katika mchezo huu
80': Bocco anaruka vizuri hapa lakini kipa anaokoa hapa
KADI: Juuko analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Gomaa ambaye bado yuko cchini pale
85': Yusuf Otara anaingia kuchukua nafasi ya Islam Issa
87': Wachezaji wa Al Masry wanajilaza chini ila mara kwa sasa. Inaonekana ni jaja yao ya kupoteza muda
90': Dakika 5 zimeongezwa kwenye mchezo hii