Miss Tanzania 2014 kufungwa miaka 3

Miss Tanzania 2014 kufungwa miaka 3

palalisote

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2010
Posts
8,335
Reaction score
1,459
Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) wamesema endapo mrembo wa Taifa mwaka huu 'Redd's Miss Tanzania 2014', Sitti Mtemvu, atabainika kudanganya umri wake kwa kughushi vyeti vya kuzaliwa, atakabiliwa na kifungo cha kwenda jela kwa muda usiopungua miaka mitatu, imeelezwa jana jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili jana, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Rita, Josephat Kimaro, alisema adhabu hiyo imewekwa kwa wale watakaofanya makosa ya kutoa taarifa za uongo ili waweze kupatiwa vyeti vya kuzaliwa au kifo.

Kimaro alisema kwamba adhabu hiyo humpata mkosaji hapo hapo baada ya kukamilika kwa uchunguzi wa taarifa zake na kulinganisha na zile alizoziwasilisha Rita ili kupatiwa cheti kipya.

"Kifungu namba 28 (3) cha sheria ya kuandikisha vizazi na vifo kimeweka adhabu kwa makosa ya kutoa habari za uongo na adhabu hiyo hutolewa hapo kwa hapo," alisema Kimaro.

Kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Vizazi na Vifo (sura ya 108) toleo la mwaka 2002, ni kosa la jinai kutoa taarifa za uongo kwa Msajili, na pia kosa la jinai kughushi.

Alisema kwa sasa suala la Sitti limepelekwa kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo (Philip Saliboko) na mara baada ya kukamilika taarifa zake zitatolewa hadharani ili jamii ifahamu ukweli.

"Huo mkanganyiko tumeshaupokea na tunaufanyia kazi, tutafanya kazi hii kwa kuzingatia na kufuata sheria na miongozo," Kimaro alisema.
"Rita imebaini kuwapo na udanganyifu wa aina hiyo ambao unafanywa na waombaji kwa kutuma maombi mapya baada ya kutakiwa kupeleka vyeti ili wapate ajira, kujiunga na vyuo au kusafiri nje ya nchi.

Alisema pia wengine wamebainika kuomba vyeti vipya wakiwa na nia ya kubadili majina na kuyaacha yale ya awali waliyokuwa wanayatumia kwa sababu binafsi wanazozifahamu.
Alisema kwamba watachunguza kama mrembo huyo alifuata taratibu zinazostahili za kuomba cheti kipya ikiwapo kuwasilisha taarifa ya kupoteza cheti hicho inayotolewa katika kituo cha polisi.

Mapema Jumanne wiki hii, Sitti, alishindwa kusema ni kituo kipi alitoa taarifa baada ya kupoteza cheti chake cha kuzaliwa cha zamani huku pia akishindwa kukubali au kuikana hati yake ya kusafiria ambayo inayoonesha amezaliwa Mei 31, 1989 na ilitolewa Februari 15, 2007 na muda wake wa kutumika mwsiho ukiwa ni Februari 14, 2017.

Hati hiyo ina namba AB 202696 wakati cheti kipya cha kuzaliwa kilichotolewa Septemba 9, mwaka huu kinachoonesha amezaliwa Mei 31, 1991 ni namba 1000580309.

Katika cheti hicho kipya kinaonyesha kuwa baba wa Sitti ni Abbas Mtemvu Zuberi (Mbunge- Temeke) wakati mama yake ni Mariam Nassor Juma (Diwani- Temeke) jijini.

Hata hivyo, NIPASHE lilipotinga Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi kutaka kujiridhisha kuhusu utata wa umri wa Sitti, Msemaji wa Idara ya Uhamiaji, Abbas Ilovia alisema wameshapokea maswali mengi kutoka kwa waandishi, hivyo kwa sasa wanafanya uchunguzi na utakapokamilika wataitisha mkutano na wanahabari ili kuujulisha umma ukweli halisi.

Sitti aliibuka kidedea katika shindano la urembo la taifa lililofanyika usiku wa Jumamosi ya Oktoba 11 kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini na kuwashinda washiriki wenzake 29 waliokuwa wanawania taji hilo.

Chanzo: Gazeti la Nipashe


>>>>HAPA CHINI NI TAARIFA KUTOKA IDARA YA UHAMIAJI MAREKANI>>>>>

attachment.php


 
Ningekuwa ni mimi huyu miss Tanzania ningevua taji tu mwenyewe.....

Furaha imegeuka huzuni sasa.. ni aibu ya mwaka Yaani kivyovyote vile huyu dada sitti anawakati mgumu sana. Maana najua anasoma mitandao sana na anajua ni jinsi gani hakubariki na jumuiya ya watanzania .

Pia hawezi kupewa support yoyote ile. Dada nakushauri vua tu hilo taji..ubaki na amani kwani kuwa miss tz ndo utaenda peponi...??
 
Ningekuwa ni mimi huyu miss tanzania ningevua taji tu mwenyewe.....furaha imegeuka huzuni sasa..ni aibu ya mwaka. Yaani kivyovyote vile huyu dada sitti anawakati mgumu sana. Maana najua anasoma mitandao sana na anajua ni jinsi gani hakubariki na jumuiya ya watanzania . Pia hawezi kupewa support yoyote ile. Dada nakushauri vua tu hilo taji..ubaki na amani kwani kuwa miss tz ndo utaenda peponi...??

kweli kabisa usemayo
bora avue tu awe na amani maana sasa kila kona anaonekana kitukk
 
Hivi authority za USA zikipelekewa taarifa kwamba huyu mrs Tanzania alikuwa anatembea na false documents zitachukua hatua gani?
 
Kuna ile clip yake ya mahojiano na waandishi wa habari kashindwa hata kujitetea anasema hajajiandaa kujibu maswali apewe mda na kakana kuwa na mtoto
 
kuna ile clip yake ya mahojiano na waandishi wa habari kashindwa hata kujitetea anasema hajajiandaa kujibu maswali apewe mda na kakana kuwa na mtoto

labda nataka akatengeneze cheti cha kuzaliwa cha mtoto kuonyesha , mtoto ana miaka 12 hivyo yeye asingeweza kumza akiwa na miaka 6.
 
Siti bana ana nyota ya kuongelewaa huyuu kama Diamond
 
Siti bana ana nyota ya kuongelewaa huyuu kama Diamond
kashindwa hata kuwapongeza sauti sol kwa kushinda best african act ya EMA wakati wao walimpa hadi happy b day? ahhhh dangoote nooma bana
 
kashindwa hata kuwapongeza sauti sol kwa kushinda best african act ya EMA wakati wao walimpa hadi happy b day? ahhhh dangoote nooma bana

sio lazima kuwapa hongera kama kawaambia halaf hujui
 
Oke oke ngoja niweke senti zangu 2. Kama mimi ni kiti cha utomvu na nina hela ya kutosha this is how I am getting out of this shit.
  1. Naingia katika moja ya vituo vya polisi vilivyojaa bongo. Nakata mkwanja utakaoniwezesha kutengeneza faili la kupotelewa na cheti soon baada ya hiyo wanayoita kambi ya miss Tz kuanza. Hii ni kuonesha kuwa nilitumia cheti cha zamani kuomba nafasi ya kushiriki hayo mashindano.
  2. Natengeneza cheti kingine (fake) cha kuzaliwa kinachoonesha tarehe hizi hizi za 1991 ila hiki kinakuwa na tarehe ya zamani kidogo sema labda mwaka 1992 hivi. Natoa nakala na kumkabidhi uncle Lundenga atupie kwenye mafaili yake.
  3. Nachukua nakala ya namba 1 hapo juu na kuipenyeza RITA (monie talks au sio?) na kutengeneza rekodi nyingine mpya ila ya tarehe za zamani kidogo (obviously tarehe iliyo mbele ya ile ya ripoti ya polisi). Hapo suala la RITA litakuwa limeisha maana rekodi zote zitakuwa sawa.
  4. Naita waandishi wa habari naomba radhi na kusema kuwa kwa kweli maneno yaliyosemwa ni mengi na pengine ndiyo yalinifanya ni-act emotionally mwanzoni. Hata hivyo nitaonesha rekodi zote hizo hapo juu.

Passport naisolve kama ifuatavyo.
Nafanya plastic surgery ya kubadilisha "iris" na alama za vidole halafu nasema hizo document sio zangu wala sizifahamu. Kazi kwisha.
 
Ningekuwa ni mimi huyu miss Tanzania ningevua taji tu mwenyewe.....

Furaha imegeuka huzuni sasa.. ni aibu ya mwaka Yaani kivyovyote vile huyu dada sitti anawakati mgumu sana. Maana najua anasoma mitandao sana na anajua ni jinsi gani hakubariki na jumuiya ya watanzania .

Pia hawezi kupewa support yoyote ile. Dada nakushauri vua tu hilo taji..ubaki na amani kwani kuwa miss tz ndo utaenda peponi...??
On the contrary kwa imani yake (nadhani ni muislamu) kuwa miss Tz ni kama vile anaelekea ruti ya motoni hivi.
 
Mpk saiv sijaelewa wanachunguza nn ambacho hakionekani. Mbona kila kitu kipo wazi. Hapo wanachotaka sasa ni kubadilisha ukwely kuwa uongo. Na tutashanga baada ya uchunguzi utasikia ameshinda na anaenda kugombea miss world. Na mwakani tutamuona anamvisha mwingine taji. This is our tanzania kipi hatujasikia jmn. Hamna uchunguzi hapo. Labda mtwambie tunachofanya sasa ni kubadilisha ukwely ili uwe uongo basi. Koz kiukwely hapo ni hela tu ndo inayoongea hamna kingine
 
sitti rudisha taji na urudi zako marekani.....
 
Back
Top Bottom