Mistari myekundu machoni

Mistari myekundu machoni

Crispin Nyoni

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
413
Reaction score
90
Kwanza shikamoo daktari/Mtaalam/Mwenye kujua utatuzi wa shida hii. Habari za huko nyumbani. Natumaini hujambo. Mimi ni kijana wa miaka 32.

Nina tatizo kwamba macho yangu yana mistari mingi myekundu na jicho hili la kulia kwa juu hapa pana kama kangozi fulani kekundu. Kwa hiyo nakuomba unijulishe hili ni tatizo gani? Na unanisaidiaje katika kulitibu.

Ndimi Crispin Nyoni.
 
Nafikiri atakae jibu swali lako uwenda wakawa wachangiaji tofauti wenye fani na wasikuwa na fani ya Udaktari...
Kiufupi Daktari unaemuakia na kumtakia hali pamoja na kujua hali ya nyumbani atakuwa katoka:bange:

Jibu...au ushauri wangu nenda Hospitali ya macho iliyo karibu nawe alaka iwezekanavyo kama uko Dar nenda CCBRT
 
Marahaba. Umejieleza kiufasaha nimekuelewa. Kuna siku mwana JF mmoja akatuwekea picha yenye mistari akasema tafuta kidoti cheusi. Nilishindwa kukiona.

Nikashauriwa kula sana karoti. Na wewe sasa nenda ukale karoti kwa wingi. Dr. MziziMkavu amedokeza pia kwamba bamia zitakusaidia pia.

Siku njema.
 
ndio madhara ya kamjiti ketu kale kaasiri....
 
bora upate matibabu haraka manake kanda ya ziwa hawachelewi kukutaabisha
 
Tayari nimetibiwa kwa ushauri wa miwani ya kusomea (TSHS 60,000),mboga za majani kama spinachi nile na karoti. Kupunguza matumizi ya kompyuta na simu. Asanteni.
 
Back
Top Bottom