Mitagato: Nilishikiliwa na Polisi siku 11 bila kufunguliwa mashitaka, nikasafirishwa hadi Dar

Mitagato: Nilishikiliwa na Polisi siku 11 bila kufunguliwa mashitaka, nikasafirishwa hadi Dar

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
MITAGATO AMTUMIA WARAKA ASKOFU, AELEZA JINSI ALIVYOSHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA SIKU 11 PASIPO KUFUNGULIWA MASHTAKA MAHAKAMANI

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Nashukuru kushiriki kunipazia sauti uliposikia kuwa nilikuwa nimechukuliwa na Jeshi la Polisi. Mimi ni Mjumbe wa Kamati Tendaji ya CHADEMA Kanda ya Magharibi yenye Mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi!

Nilikamatwa siku ya Jumatatu tarehe 9 mchana, nikaambiwa RCO wa Kigoma ana shida na mimi. Nikaondoka nao mpaka Central Police, na kuwekwa lockup bila maelezo yoyote. Kesho yake Jumanne Saa Tisa mchana nikatolewa na kupelekwa nyumbani kwangu kwa ajili ya kupekuliwa. Tulipofika nyumbani, baada ya upekuzi waliondoka na vifaa vya uenezi vya CHADEMA ambavyo ni bendera, t-shirts, skafu, vitabu, openers na keyholders! Tukarudi Central Police.

Baada ya muda nikaingizwa kwenye gari nikiwa nimefungwa pingu na kuondoka nikiwa sijui ninapelekwa wapi, safari iliendelea mpaka Tabora Central Police nikalala hapo. Asubuhi ya Jumatano nikatolewa lockup (ndani) na kufungwa tena pingu nikaingizwa kwenye gari likiwa na watu watano wenye siraha, ambao sio wale niliotoka nao Kigoma. Mpaka hapo, familia yangu haijui niko wapi!

Safari ikaanza kuelekea nisikokujua, mpaka Saa Tano usiku tukafika Kituo cha Polisi Chang'ombe, Dar es Salaam. Nikashushwa na kuingizwa lockup (ndani) mpaka nilipoachiliwa usiku wa Alhamisi tarehe 19. Niliachiliwa usiku ok baada ya Wanaseheria wa CHADEMA kuwafungulia mashtaka Mahakamani viongozi wa Jeshi la Polisi kwa kutushikiria kinyume cha Sheria. Nilituhumiwa eti kwa kuhamasisha maandamano! Masharti ya kuachiwa kwangu na Jeshi la Polisi ni kwamba nikifika Kigoma niende kuripoti kwa RCO. Simu zangu wamebaki nazo Polisi wa Dar es Salaam!

Kupitia kwako Baba Askofu, ninaomba niweze kuwashukuru wote walioshiriki kunipazia sauti pamoja na Wanasheria wetu.

Mitagato Benjamin
Mjumbe wa Kamati Tendaji,
CHADEMA Kanda ya Magharibi (Tabora, Kigoma & Katavi)

700AC94F-0979-4647-B6E9-958DCB23F3CB.jpeg
 
Nchi ya ajabu sana hiyo.Nadhani kuna jambo la kufanya ili heshima iwepo na haya yasiendelee.Si tu kumwachia Mungu atende mtu afe Watanzania wenyewe sasa wachukue hatua
Mungu hapana, lazima kufanya kitu, actions, siyo maneno maana Mungu ni maneno. Dictators can not heed to words , only actions
 
Kama CHADEMA hawaweki kumbukumbu sahihi na kamilifu kabisa kwa matukio yote haya, watakuwa wanawaangusha sana wanachama wao, na waTanzania kwa ujumla.

Hapa ndipo CHADEMA haijafanya vizuri hata kidogo na ndiyo maana nadhani wanachama wao wengi wanasita kujitoa mhanga wa kukaa mahabusu bila ya kuvunja sheria yoyote, kwa sababu chama chao hakiwapi 'support' ya kutosha, hata ile ya kutoa taarifa/kutangaza waTanzania wote wajue ni wanachama wapi wapo mahabusu kwa uonevu

Habari hizi zinatakiwa kutangazwa kwa kila njia inayowezekana ili wananchi wote wajue. Hizi siyo habari za kukaa nazo kwenye mafaili peke yake.

Huu ni uonevu usiostahiri kufanyiwa mtu yeyote.
 
Kama CHADEMA hawaweki kumbukumbu sahihi na kamilifu kabisa kwa matukio yote haya, watakuwa wanawaangusha sana wanachama wao, na waTanzania kwa ujumla...
Kweli kabisa. Nakubaliana na wewe 100%.

Kila mwanachadema anayekamatwa ni lazima taarifa zake zisambazwe ktk vyombo mbalimbali vya habari.

Na yote yaliyowafika wakiwa mikononi mwa Polisi ni lazima yabainishwe ili wananchi waweze kuelewa kinachoendelea.

cc Erythrocyte
 
Nchi ya ajabu sana hiyo.Nadhani kuna jambo la kufanya ili heshima iwepo na haya yasiendelee.Si tu kumwachia Mungu atende mtu afe Watanzania wenyewe sasa wachukue hatua
Mkuu, unataka hatua gani waTanzania wazichukue wakati huu ambapo mtesi ndio anazidi kutapatapa?

Unataka kumtupia kamba ya kujiokoa wakati unaona vitendo vyake vinaashiria kwamba sasa hana wigo tena wa kuendelea kuwanyima haki waTanzania?

Unataka CHADEMA wafanye nini zaidi ya wanayofanya sasa yanayomhangaisha mtesaji huyu?

Acha 'pressure' izidi kuongezeka, itakapofika mahali ambapo haiwezi tena kuongezeka, utaona matokeo yake. Sasa hivi CHADEMA waendelee hivyo hivyo kumtia mtesaji kichaa ili ajimalize haraka.
 
Kama CHADEMA hawaweki kumbukumbu sahihi na kamilifu kabisa kwa matukio yote haya, watakuwa wanawaangusha sana wanachama wao, na waTanzania kwa ujumla.

Hapa ndipo CHADEMA haijafanya vizuri hata kidogo na ndiyo maana nadhani wanachama wao wengi wanasita kujitoa mhanga wa kukaa mahabusu bila ya kuvunja sheria yoyote, kwa sababu chama chao hakiwapi 'support' ya kutosha, hata ile ya kutoa taarifa/kutangaza waTanzania wote wajue ni wanachama wapi wapo mahabusu kwa uonevu

Habari hizi zinatakiwa kutangazwa kwa kila njia inayowezekana ili wananchi wote wajue. Hizi siyo habari za kukaa nazo kwenye mafaili peke yake.

Huu ni uonevu usiostahiri kufanyiwa mtu yeyote.
CC John Mnyika, John Mrema, Kigaila, Lisu
 
Ndiyo nchi yetu ilipofikia Mkuu. Maovu ya kutisha sana ili tu kung’ang’ania madarakani. Wengi tulidhani baada ya kufa yule dhalimu mwendazake tutayasahau maovu haya lakini bado yanaendelea kwa kasi ile ile!
Bila katiba mpya udhalimu huu kamwe hautoweza kukoma
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Watu wenye silaha/dola hawaogopi maneno maneno.,walishaona watu Ni maboya na Cha kuwafanya wanajua hakipo.
 
Kama CHADEMA hawaweki kumbukumbu sahihi na kamilifu kabisa kwa matukio yote haya, watakuwa wanawaangusha sana wanachama wao, na waTanzania kwa ujumla.

Hapa ndipo CHADEMA haijafanya vizuri hata kidogo na ndiyo maana nadhani wanachama wao wengi wanasita kujitoa mhanga wa kukaa mahabusu bila ya kuvunja sheria yoyote, kwa sababu chama chao hakiwapi 'support' ya kutosha, hata ile ya kutoa taarifa/kutangaza waTanzania wote wajue ni wanachama wapi wapo mahabusu kwa uonevu

Habari hizi zinatakiwa kutangazwa kwa kila njia inayowezekana ili wananchi wote wajue. Hizi siyo habari za kukaa nazo kwenye mafaili peke yake.

Huu ni uonevu usiostahiri kufanyiwa mtu yeyote.
Huyu mhanga ametoka baada ya wana sheria wa Chadema kuwafungulia mashtaka viongozi wa polisi. Kwa hiyo sio kweli kuwa Chadema imewatelekeza. Habari zake zilikuwepo kwenye social media siku nyingi.

Pamoja na kukubaliana na wewe kwa kiasi fulani, ninavyojua mimi Chadema hawana gazeti au kituo cha radio au televisheni. Labda wanachoweza kufanya ni kuwajumuisha watu wao wote kwenye kilio chao juu ya Mwenyekiti. Na labda waweke orodha kwenye social medium platform zao zenye majina ya wale wote walio ndani kwa sababu za kisiasa. Na kama vile wanavyofanya kwa Mbowe wawe wanakumbusha kila siku, siku ambazo wamekaa ndani. Orodha ijumuishe pia wale ambao wamepotea na hawana taarifa zao.

Amandla...
 
Huyu mhanga ametoka baada ya wana sheria wa Chadema kuwafungulia mashtaka viongozi wa polisi. Kwa hiyo sio kweli kuwa Chadema imewatelekeza. Habari zake zilikuwepo kwenye social media siku nyingi.

Pamoja na kukubaliana na wewe kwa kiasi fulani, ninavyojua mimi Chadema hawana gazeti au kituo cha radio au televisheni. Labda wanachoweza kufanya ni kuwajumuisha watu wao wote kwenye kilio chao juu ya Mwenyekiti. Na labda waweke orodha kwenye social medium platform zao zenye majina ya wale wote walio ndani kwa sababu za kisiasa. Na kama vile wanavyofanya kwa Mbowe wawe wanakumbusha kila siku, siku ambazo wamekaa ndani. Orodha ijumuishe pia wale ambao wamepotea na hawana taarifa zao.

Amandla...
Mbona umekubaliana na mimi kwa kiasi chote!
Pamoja na kukubaliana na wewe kwa kiasi fulani, ninavyojua mimi Chadema hawana gazeti au kituo cha radio au televishen
Au ni wapi ambapo hatukukubaliana?

Ukweli ni kwamba eneo hili la kuwapigania wafuasi na wanachama wao na wengine wote wanaoonewa na serikali ili habari za uonevu zienee kwa wananchi ndilo lingekuwa eneo muhimu zaidi kwa mapambano yao.
Lengo la waonevu ni kuwatia woga wananchi na kuwakatisha tamaa wanaotafuta haki. Kuwatangazia wananchi (kwa njia zozote zinazowezekana) ni kuwatia moyo wapambanaji kuendeleza mapambano CHADEMA wanaposhindwa kufanya hivyo maana yake watesi wanatimiza malengo yao, na kuifanya kazi ya CHADEMA kuwa ngumu zaidi.
 
MITAGATO AMTUMIA WARAKA ASKOFU, AELEZA JINSI ALIVYOSHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA SIKU 11 PASIPO KUFUNGULIWA MASHTAKA MAHAKAMANI

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Nashukuru kushiriki kunipazia sauti uliposikia kuwa nilikuwa nimechukuliwa na Jeshi la Polisi. Mimi ni Mjumbe wa Kamati Tendaji ya CHADEMA Kanda ya Magharibi yenye Mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi!

Nilikamatwa siku ya Jumatatu tarehe 9 mchana, nikaambiwa RCO wa Kigoma ana shida na mimi. Nikaondoka nao mpaka Central Police, na kuwekwa lockup bila maelezo yoyote. Kesho yake Jumanne Saa Tisa mchana nikatolewa na kupelekwa nyumbani kwangu kwa ajili ya kupekuliwa. Tulipofika nyumbani, baada ya upekuzi waliondoka na vifaa vya uenezi vya CHADEMA ambavyo ni bendera, t-shirts, skafu, vitabu, openers na keyholders! Tukarudi Central Police.

Baada ya muda nikaingizwa kwenye gari nikiwa nimefungwa pingu na kuondoka nikiwa sijui ninapelekwa wapi, safari iliendelea mpaka Tabora Central Police nikalala hapo. Asubuhi ya Jumatano nikatolewa lockup (ndani) na kufungwa tena pingu nikaingizwa kwenye gari likiwa na watu watano wenye siraha, ambao sio wale niliotoka nao Kigoma. Mpaka hapo, familia yangu haijui niko wapi!

Safari ikaanza kuelekea nisikokujua, mpaka Saa Tano usiku tukafika Kituo cha Polisi Chang'ombe, Dar es Salaam. Nikashushwa na kuingizwa lockup (ndani) mpaka nilipoachiliwa usiku wa Alhamisi tarehe 19. Niliachiliwa usiku ok baada ya Wanaseheria wa CHADEMA kuwafungulia mashtaka Mahakamani viongozi wa Jeshi la Polisi kwa kutushikiria kinyume cha Sheria. Nilituhumiwa eti kwa kuhamasisha maandamano! Masharti ya kuachiwa kwangu na Jeshi la Polisi ni kwamba nikifika Kigoma niende kuripoti kwa RCO. Simu zangu wamebaki nazo Polisi wa Dar es Salaam!

Kupitia kwako Baba Askofu, ninaomba niweze kuwashukuru wote walioshiriki kunipazia sauti pamoja na Wanasheria wetu.

Mitagato Benjamin
Mjumbe wa Kamati Tendaji,
CHADEMA Kanda ya Magharibi (Tabora, Kigoma & Katavi)

poleni sana waathirika wa uonevu Mungu awape ustahimilivu
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom