Mitandao ya simu Tanzania na utapeli wanaoufanya kuongeza CPA "Click per Action".

Mitandao ya simu Tanzania na utapeli wanaoufanya kuongeza CPA "Click per Action".

snipa

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2013
Posts
4,437
Reaction score
2,043
Miaka ya hivi karibuni mitandao ya simu imekuwa ikitulazimisha kusoma sms, na wanafanya hivyo ili tu tusome matangazo yao mengine yasiyokuwa na Tija, bila kujua kuwa wanakwamisha watanzania Kwa kuwapotezea muda.

Mfano unapo angalia salio, asilimia kubwa hii mitandao imekuwa ikitulazimisha kusoma sms, yaani ukipiga USSD *102# Utaambiwa ndugu flani angalia sms Kwa maelezo kuhusu salio la vifurushi.

Screenshot_20250207-003543.jpg


Sasa fikiria mtandao upo chini, sms hazifiki, utasubiri we mpaka ujute, afadhali wanaotumia smartphone wanaweza tumia app, lakini asilimia kubwa hata watumiaji wa smartphone huangalia salio Kwa USSD,

Hii Hali imekuwa ikifelisha mambo mengi sana, unaweza nunua vidurushi mara mbili ukijua huna salio kumbe lipo ila sms hazifiki.

Kikubwa walichotarget ni matangazo yao na kutujazia sms zisizokuwa na msingi wakupe malink kwenye sms waongeze CPA, wakati Wana uwezo wakukuambia hapohapo kwamba salio la vifurushi ni hivi na hivi, japo baadhi wanafanya lakini ukiangalia, Yas, Halotel, Zantel ni yale yale
 
Back
Top Bottom