EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,325
Tanzania imeshauriwa kuwaruhusu watoto wanaomaliza darasa la saba kuendelea na masomo ya sekondari kwenye shule za serikali bila kuzingatia matokeo yao kwenye mitihani ya mwisho ya darasa la saba. Ushauri huo umetolewa na shirika la haki za binadamu la Marekani (Human Rights Watch) na Tanzania Child Rights Forums kwenye barua yao kwenda kwa Waziri wa Elimu.
Kwa sasa ili mwanafunzi aweze kuchaguliwa kwenda shule ya sekondari ya serikali ni lazima afaulu mitihani yake ya mwisho kwa kiwango kilichowekwa na serikali. Hata hivyo, mashirika hayo yanadai kuwa zaidi ya watoto 400,000 (sawa na aslimia 49.4) walifeli mitihani yao ya darasa la saba mwaka 2013.
Juliane Kippnberg wa Human Rights Watch anadai kuwa watoto wote wa Kitanzania lazima wapewe haki ya kuendelea na masomo ya sekondari kwenye shule za serikali bila kuzingatia matokeo yao kwenye mitihani ya darasa la saba. Anadai kuwa kutumia matokeo ya darasa la saba kama kigezo cha kuamua nani aendelee na masomo ya sekondari ni kinyume na haki ya mtoto ya kupata elimu.
Serikali inafikiria kuwa na sera mpya ya elimu ambapo itakuwa ni lazima kwa kila mtoto kupata elimu ya sekondari hadi kidato cha nne. Hata hivyo, sera hiyo mpya haigusii chochote kuhusiana na kutumia matokeo ya darasa la saba kama kigezo cha kuamua nani aendelee na masomo ya sekondari. Katika barua yao, wanadai kuwa mitihani ya darasa la saba itumike tuu kupima uwezo wa mwanafunzi lakini siyo kama kigezo cha nani aendelee na elimu ya sekondari.
Mashirika hayo yanapendekeza serikali iwe na sera mpya ya elimu na kuhakikisha kuwa mitihani ya darasa la saba isitumike kuzuia watoto kuendelea na elimu ya sekondari. Pia yamependekeza serikali iboreshe vitendea kazi kwenye shule za sekondari ili shule hizo ziweze kufundisha wanafunzi wengi.
Aidha mashirika hayo yanadai kuwa mitihani ya darasa la saba inachangia kukiukwa kwa haki nyingine za watoto. Kwa mfano, Human Rights Watch wanadai kuwa katika uchunguzi wao walioufanya mwaka jana walikuta kuwa watoto waliofeli mitihani ya darasa la saba walikuwa katika hatari ya kujihusisha kwenye machimbo madogo madogo ya madini.
Tanzania imetia saini Mkataba wa Kimataifa wa Haki ya Mtoto. Kwa mujibu wa mkataba huo, kila mtu aliye chini ya umri wa miaka 18 ana haki ya kupata elimu. Je, tuache kutumia matokeo ya darasa la saba kama kigezo cha kuchagua nani aendelee na masomo ya sekondani na nani aishie kwenye elimu ya darasa la saba?
Barua hiyo kwenda kwa Waziri wa Elimu inapatikana: Letter by HRW and TCRF to Tanzania Minister of Education | Human Rights Watch
Invisible, gfsonwin, MTM, Kiranga, snowhite, Kongosho, Nyani Ngabu, Elly Andrew, xtra, TIQO, Enjoy Fumbo, MAKOLE, mwaJ, dedam, kyumana, mseveni, Masele Joe, kichwa kikubwa, buchuja, Chisco, Dr. Rama, Joseph Isaack, Meuzy, vanmedy, Issa Daudi, FALSETTO, Ramadhan vitalis, MDSON, chopeko, TAMBUA, Azizi Bin Adam, Chal, ndawo, Mdume, bshayo, Dark City, mgweno tajiri, Mkomawatu, ntamaholo, Baraka Roman, sundoka, Sam Love, swagazetu, ladyfurahia, Rugaijamu, Brother James, watu8, The Magnificent, Excel, Molembe, kbm, CHUAKACHARA, Sizinga, Munkari, BONGOLALA, Izack Mwanahapa, TUKUTUKU, Zogwale, kikokwe, Mhache, Njowepo, Mpita Njia, benzoo, Gama, Makupa, englibertm, Jabulani, Nivea, Window7, Mwl.RCT, mwekundu,
Kwa sasa ili mwanafunzi aweze kuchaguliwa kwenda shule ya sekondari ya serikali ni lazima afaulu mitihani yake ya mwisho kwa kiwango kilichowekwa na serikali. Hata hivyo, mashirika hayo yanadai kuwa zaidi ya watoto 400,000 (sawa na aslimia 49.4) walifeli mitihani yao ya darasa la saba mwaka 2013.
Juliane Kippnberg wa Human Rights Watch anadai kuwa watoto wote wa Kitanzania lazima wapewe haki ya kuendelea na masomo ya sekondari kwenye shule za serikali bila kuzingatia matokeo yao kwenye mitihani ya darasa la saba. Anadai kuwa kutumia matokeo ya darasa la saba kama kigezo cha kuamua nani aendelee na masomo ya sekondari ni kinyume na haki ya mtoto ya kupata elimu.
Serikali inafikiria kuwa na sera mpya ya elimu ambapo itakuwa ni lazima kwa kila mtoto kupata elimu ya sekondari hadi kidato cha nne. Hata hivyo, sera hiyo mpya haigusii chochote kuhusiana na kutumia matokeo ya darasa la saba kama kigezo cha kuamua nani aendelee na masomo ya sekondari. Katika barua yao, wanadai kuwa mitihani ya darasa la saba itumike tuu kupima uwezo wa mwanafunzi lakini siyo kama kigezo cha nani aendelee na elimu ya sekondari.
Mashirika hayo yanapendekeza serikali iwe na sera mpya ya elimu na kuhakikisha kuwa mitihani ya darasa la saba isitumike kuzuia watoto kuendelea na elimu ya sekondari. Pia yamependekeza serikali iboreshe vitendea kazi kwenye shule za sekondari ili shule hizo ziweze kufundisha wanafunzi wengi.
Aidha mashirika hayo yanadai kuwa mitihani ya darasa la saba inachangia kukiukwa kwa haki nyingine za watoto. Kwa mfano, Human Rights Watch wanadai kuwa katika uchunguzi wao walioufanya mwaka jana walikuta kuwa watoto waliofeli mitihani ya darasa la saba walikuwa katika hatari ya kujihusisha kwenye machimbo madogo madogo ya madini.
Tanzania imetia saini Mkataba wa Kimataifa wa Haki ya Mtoto. Kwa mujibu wa mkataba huo, kila mtu aliye chini ya umri wa miaka 18 ana haki ya kupata elimu. Je, tuache kutumia matokeo ya darasa la saba kama kigezo cha kuchagua nani aendelee na masomo ya sekondani na nani aishie kwenye elimu ya darasa la saba?
Barua hiyo kwenda kwa Waziri wa Elimu inapatikana: Letter by HRW and TCRF to Tanzania Minister of Education | Human Rights Watch
Invisible, gfsonwin, MTM, Kiranga, snowhite, Kongosho, Nyani Ngabu, Elly Andrew, xtra, TIQO, Enjoy Fumbo, MAKOLE, mwaJ, dedam, kyumana, mseveni, Masele Joe, kichwa kikubwa, buchuja, Chisco, Dr. Rama, Joseph Isaack, Meuzy, vanmedy, Issa Daudi, FALSETTO, Ramadhan vitalis, MDSON, chopeko, TAMBUA, Azizi Bin Adam, Chal, ndawo, Mdume, bshayo, Dark City, mgweno tajiri, Mkomawatu, ntamaholo, Baraka Roman, sundoka, Sam Love, swagazetu, ladyfurahia, Rugaijamu, Brother James, watu8, The Magnificent, Excel, Molembe, kbm, CHUAKACHARA, Sizinga, Munkari, BONGOLALA, Izack Mwanahapa, TUKUTUKU, Zogwale, kikokwe, Mhache, Njowepo, Mpita Njia, benzoo, Gama, Makupa, englibertm, Jabulani, Nivea, Window7, Mwl.RCT, mwekundu,