Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Rais Uhuru Kenyatta amesema watahiniwa wote wa mitihani ya kitaifa kwa darasa la nane la kidato cha nne, KCPE na KCSE, watarudi shuleni hivi karibuni.
Rais alisema kwa sasa shughuli za mitihani hiyo ya kitaifa zitaendelea kama zilivyokuwa zimepangwa kabla ya janga la coronavirus kutokea.
Rais Uhuru Kneyatta amesema serikali inafanya mikakati kwa watahiniwa wa KCPE kurejea kazini.
"Tunaweka mikakati vile ambavyo watarudi shuleni kidogo kidogo na tutatoa mwelekeo kamili hivi karibuni,"
"Hio itaanzia na hawa ambao watafanya mitihani ili waweze kujiandaa kwa mitihani yao. Na tutahakikisha kuwa hizo siku hawajasoma zimeshughulikiwa," alisema Rais.
Rais aliwataka wazazi na watahiniwa hao kusubiri tangazo la serikali hivi karibu baada ya kutathmini hali ya janga la coronavirus.
Rais Uhuru Kenyatta na kikao cha wanahabari hapo awali. Kwenye mahojiano Jumatano, Aprili 22, Rais alisema hakuna mipango ya kuahirisha KCPE na KCSE.
Rais alisema mikakati itawekwa na wizara ya Elimu kuhakikisha kuwa watahiniwa wamefunzwa na kulipia muda waliopoteza.
Msimamo huo ni sawa na ule wa waziri wa Elimu Profesa George Magoha Jumapili, Aprili 19 alipowatangazia wazazi kuwa mitihani hiyo haitaahirishwa.
"Kufikia wakati huu, hakuna mtu amefikiria kuahirisha KCPE na KCSE, na kulingana na serikali inajua wanafunzi wanasoma kupitia mtandao," Magoha alisema.
Watahiniwa wa KCSE na KCPE wamekuwa na kiwewe kuhusu mtihani wao mwaka huu.
Rais alisema juhudi za wanafunzi hao kurudi shuleni zinafanywa huku serikali ikizingatia kuwa kuna baadhi ambao hawapati masomo kupitia mtandao au vyombo vya habari.
Aliwataka Wakenya kutii maagizo ya kukabiliana na covid-19 ili kukomesha ugonjwa huo na kuhakikisha Wakenya hawataseki kwa njia mbali mbali.
Kumekuwa na maswali kuhusu mitihani ya kitaifa kwani wanafunzi hawajakuwa shuleni tangu Machi 16.
Rais alisema kwa sasa shughuli za mitihani hiyo ya kitaifa zitaendelea kama zilivyokuwa zimepangwa kabla ya janga la coronavirus kutokea.
Rais Uhuru Kneyatta amesema serikali inafanya mikakati kwa watahiniwa wa KCPE kurejea kazini.
"Tunaweka mikakati vile ambavyo watarudi shuleni kidogo kidogo na tutatoa mwelekeo kamili hivi karibuni,"
"Hio itaanzia na hawa ambao watafanya mitihani ili waweze kujiandaa kwa mitihani yao. Na tutahakikisha kuwa hizo siku hawajasoma zimeshughulikiwa," alisema Rais.
Rais aliwataka wazazi na watahiniwa hao kusubiri tangazo la serikali hivi karibu baada ya kutathmini hali ya janga la coronavirus.
Rais Uhuru Kenyatta na kikao cha wanahabari hapo awali. Kwenye mahojiano Jumatano, Aprili 22, Rais alisema hakuna mipango ya kuahirisha KCPE na KCSE.
Rais alisema mikakati itawekwa na wizara ya Elimu kuhakikisha kuwa watahiniwa wamefunzwa na kulipia muda waliopoteza.
Msimamo huo ni sawa na ule wa waziri wa Elimu Profesa George Magoha Jumapili, Aprili 19 alipowatangazia wazazi kuwa mitihani hiyo haitaahirishwa.
"Kufikia wakati huu, hakuna mtu amefikiria kuahirisha KCPE na KCSE, na kulingana na serikali inajua wanafunzi wanasoma kupitia mtandao," Magoha alisema.
Watahiniwa wa KCSE na KCPE wamekuwa na kiwewe kuhusu mtihani wao mwaka huu.
Rais alisema juhudi za wanafunzi hao kurudi shuleni zinafanywa huku serikali ikizingatia kuwa kuna baadhi ambao hawapati masomo kupitia mtandao au vyombo vya habari.
Aliwataka Wakenya kutii maagizo ya kukabiliana na covid-19 ili kukomesha ugonjwa huo na kuhakikisha Wakenya hawataseki kwa njia mbali mbali.
Kumekuwa na maswali kuhusu mitihani ya kitaifa kwani wanafunzi hawajakuwa shuleni tangu Machi 16.