Aah,suruali za bioct,tokyo,savco,big sum,viatu vya mokasi,njumu za maradona(zilikuwa za vitambaa kigumu cheusi chini soli kama kiatu cha kusakata kabumbu na zilikuwa na majina ya wwahezaji tofauti.) kofia za Luck zilikuwa na bati juu na kwenye kenop ya mbele kuubwaa, redio ya mkulima band nne,betri unafunga kwenye box na mpira wa manati, redio ya casseti ya panasoni almaarufu redio ya memory ilikuwa na kitufe cha njano cha kurekodia, mashati ya juliana,bahama mama a.k.a ujiuji, mikanda ya suruali ya crocodile,kama hujatinga hui skull shauri yakooo! Mifuko ya kuwekea daftari ya sport,ilikuwa na kamba unabeba mgongoni kama kifurushi maana ilikuwa ni ya kunyonga, aaaaaaah long time agoo men! Wazee wa sukus star, sakayonsa,pomoni paka bushee,kwasakwasa,, ,