Mitumbwi yatumika kuvusha wanachi Mkuranga

Mitumbwi yatumika kuvusha wanachi Mkuranga

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
19 Oktoba 2020
Mkuranga, Pwani
Tanzania

MITUMBWI YATUMIKA KUVUSHA WANACHI MKURANGA


Wakazi wa kata ya Tambani wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani, Tanzania wanalazimika kutumia mitumbwi kutoka eneo moja kwenda jingine baada ya daraja la Kifolongo kukatika.

Daraja hilo lilikatika Aprili, 2020 lakini mvua zilizonyesha kati ya Oktoba 13 hadi 18, 2020 zimesababisha maji kujaa eneo hilo na wananchi kulazimika kutumia mitumbwi kuvuka.

Katika mitumbwi hiyo wanafunzi wanatozwa Sh200 na watu wazima Sh300. Watu hulazimika kupanga foleni kusubiri mtumbwi mmoja ambao unatajwa kuwa salama zaidi kuliko mingine ambayo mara kadhaa ubinuka na kusababisha watu kutumbukia kwenye maji.

Source : Mwananchi Digital
 
Daraja hilo lilikatika Aprili, 2020

Hawana Mbunge wala Diwani, Mkurugenzi wa halimashauri wala DC, au walipigia kura chama cha wenye madevu ndipo magufuli akaamua kuwaonesha
 
Hawa changii pato la taifa
Ali sikika bashiru kwa mbaliii
 
Wakati huo huo Uwanja wa Ndege wa Chato hakuna hata Senene anayetua
 
Hahaha Magufuli na ccm watawaahidi kuwapelekea watu wa mkuranga maji kama kawaida yao.

Utasikia tumetenga bilioni 74 za kupekeka maji mkuranga mkinichagua nitamwambia mkumbo alete maji.
 
Wewe unashangaa hayo, mimi Kuna mdogo wangu huko huko mkuranga anasoma Nasibugani high school, mvua ikinyesha wanafunzi wanavushwa kwa mtumbwi kwa km 3 kabla ya kufika ng'ambo ya maji kuelekea kituo cha afya.
 
Back
Top Bottom