Mitume na manabii wa kisasa wasipodhibitiwa wanaweza kusababisha uchonganishi wa kitaifa.

Mitume na manabii wa kisasa wasipodhibitiwa wanaweza kusababisha uchonganishi wa kitaifa.

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Wasalaam.
Mahubiri mengi kwa hawa mitume na manabii wa kisasa yamejaa uchonganishi, manipulation, saikolojia na neno kidogo. Mengine yote sinashida nayo shida ni hii ambayo pia hata waganga huwa wanafanya. Uchonganishi.


Yaani mtu anaenda kuombewa, muombewaji anaaminishwa kalogwa, mlogwaji anatajishwa aliyemloga wenda ni mjomba, boss, dada, kaka, mama au jirani.
Sasa huyu jirani sio muumini. Hii inaleta chuki, ugomvi, kuviziana na visasi baina ya ndugu na ndugu, ofisini, familia.

Jana nilikuwa napiga story na dreva mmoja anasema yeye alitajwa kuwa anamloga shemeji yake. Akafunga safari kwenda hapo kwa mtume karibu na mbezi ili kama kweli ni muhusika wamtoe huo uchawi. Cha ajabu alipowaeleza wapambe wakamwambia yeye hayamuhusu apotezee. Akasema jambo hilo limeleta mpasuko mkubwa kwenye familia anaonekana no freemason, mchawi na hafai hata simu haipokelewi. Wale machawa walipoona jamaa haelewi, walimuitia mabaunsa wakambeba na kumfukuza kabisa hilo eneo.

Inavyoonekana yule mtoto aliyemtaja no kama alipangwa ili kuvuta wakereketwa kupitia media. Muhusika kufirisika alifirisika kwa kujitakia na anasa, na kanisani haaminiwi anapunwa sadaka tu.
Haya makanisa kwa sababu yanakua kila kona, wote wanatumia tekniki za kùfanana wanaweza kusababisha uchonganishi wa kitaifa na hali ya kuchukiana na kuviziana ikarudisha nyuma kasi ya maendeleo.

Ni hayo tu.
 
Sina ndugu anayeenda huko kwa hao wahuni,akitokea mmoja anayefanya hivyo atakosa raha kabisa kila akikutana na mimi,nitamsakama mpaka ajione ananuka shombo.
 
Sina ndugu anayeenda huko kwa hao wahuni,akitokea mmoja anayefanya hivyo atakosa raha kabisa kila akikutana na mimi,nitamsakama mpaka ajione ananuka shombo.
Wengi wanafanya siri. Kwa wazi anaendelea na dini yake, muislam, sabato au RC.
 
Mitune yenyewee ndio hii waongo waongo na wachumia tumbo km viongozi wa ccm
IMG-20240407-WA0020.jpg
 
Na sijui tu watu wanashindwaje kun'gamua vitu simpo tu.

Uchonganishi na sura zake zote, ni kazi ya kishetani VS Upatanishi na minyambuliko yake yoote ndio kazi ya kimungu.

Yapimeni mambo yote, yashikeni yaliyo mema. Eaaasy.

Halafu na we mtoa mada, mi nilidhani utaongelea kuchinganishwa kinataifa mfano kuwaambia waumini washadadie Palestina au kuwaambia waamini washadadie Israel. Kumbe ni mbanga za hapahapa local tu.

Tuanze na sheria inayowalinda ya kwamba ushahidi wa kanisani na kwenye vyombo vya imani kuwa na kinga. Tuweke vizuri hapo kama tunaweza. Maana pagumu hapooo
 
Mimi mtu akiniambia kaota kitu sijui yuko na Yesu wanakunywa juisi akamwambia a b c .
Simsikilizi,
😅😅😅 Mkuu n ww utaweza msikiliza lakin ana wafuwasi wake ambao uwambii ktu kuhusu Mchungaji wao
 
Wasalaam.
Mahubiri mengi kwa hawa mitume na manabii wa kisasa yamejaa uchonganishi, manipulation, saikolojia na neno kidogo. Mengine yote sinashida nayo shida ni hii ambayo pia hata waganga huwa wanafanya. Uchonganishi.


Yaani mtu anaenda kuombewa, muombewaji anaaminishwa kalogwa, mlogwaji anatajishwa aliyemloga wenda ni mjomba, boss, dada, kaka, mama au jirani.
Sasa huyu jirani sio muumini. Hii inaleta chuki, ugomvi, kuviziana na visasi baina ya ndugu na ndugu, ofisini, familia.

Jana nilikuwa napiga story na dreva mmoja anasema yeye alitajwa kuwa anamloga shemeji yake. Akafunga safari kwenda hapo kwa mtume karibu na mbezi ili kama kweli ni muhusika wamtoe huo uchawi. Cha ajabu alipowaeleza wapambe wakamwambia yeye hayamuhusu apotezee. Akasema jambo hilo limeleta mpasuko mkubwa kwenye familia anaonekana no freemason, mchawi na hafai hata simu haipokelewi. Wale machawa walipoona jamaa haelewi, walimuitia mabaunsa wakambeba na kumfukuza kabisa hilo eneo.

Inavyoonekana yule mtoto aliyemtaja no kama alipangwa ili kuvuta wakereketwa kupitia media. Muhusika kufirisika alifirisika kwa kujitakia na anasa, na kanisani haaminiwi anapunwa sadaka tu.
Haya makanisa kwa sababu yanakua kila kona, wote wanatumia tekniki za kùfanana wanaweza kusababisha uchonganishi wa kitaifa na hali ya kuchukiana na kuviziana ikarudisha nyuma kasi ya maendeleo.

Ni hayo tu.

Nyuzi kama hizi, aina ya kina MK254 ni chungu kuliko cyrstapen
 
Na sijui tu watu wanashindwaje kun'gamua vitu simpo tu.

Uchonganishi na sura zake zote, ni kazi ya kishetani VS Upatanishi na minyambuliko yake yoote ndio kazi ya kimungu.

Yapimeni mambo yote, yashikeni yaliyo mema. Eaaasy.

Halafu na we mtoa mada, mi nilidhani utaongelea kuchinganishwa kinataifa mfano kuwaambia waumini washadadie Palestina au kuwaambia waamini washadadie Israel. Kumbe ni mbanga za hapahapa local tu.

Tuanze na sheria inayowalinda ya kwamba ushahidi wa kanisani na kwenye vyombo vya imani kuwa na kinga. Tuweke vizuri hapo kama tunaweza. Maana pagumu hapooo
Kimataifa waumini hawapaswi kuwa upande wa Israel wala Palestina. Wanatakiwa kuwa upande wa Amani, na ubinadamu.

Kama mtu amekuroga, Yesu atashughulikia kurogwa kwako, na kumuonyesha aliyekuroga kuwa upande wa Yesu uchawi haufanyi kazi, hadi jamaa aone ujinga wa uchawi.

Sasa wajomba wao wanataka kupambana na wachawi na kuwaombea visukari, vifo na paralysis
 
Kabisa,na ndio sababu kila ninapokaa na watu huwa sisiti kuwasiliba hao jamaa,ili nijue nani ni kondoo wao kati yetu.
Mfano jamaa aliambiwa mkewe kalogwa na bosi wake. Jamaa akahapa mkewe akifa tu atamlamba mapanga huyo bosi lowalo na liwe. Sasa hapo hakuna dini tena ni vita.

Mimi nimewahi kumsaidia dada mmoja, sasa hivi ni mama mchungaji, akiandisha vijini vinamtaja bibi jirani. Wale familia tukawambia waachane na bifu na bibi, hata kama ni kweli anatumika tu. Tukashughulikia tule tujini akawa mzima na jirani na yeye ni mzima. Na sasa anafamilia mama mchungaji wanakula maisha.

Hizi dini za kuchochea bifu sio za Yesu.
 
.....kuna jamaa yangu aliambiwa mke wake na mtoto wake mdogo ni wachawi.
Huyu Musa wa Temboni ni hopeless sana....kavunja familia ya watu...howcome mtoto wa miaka 8 akawa mchawi.
 
Mfano jamaa aliambiwa mkewe kalogwa na bosi wake. Jamaa akahapa mkewe akifa tu atamlamba mapanga huyo bosi lowalo na liwe. Sasa hapo hakuna dini tena ni vita.

Mimi nimewahi kumsaidia dada mmoja, sasa hivi ni mama mchungaji, akiandisha vijini vinamtaja bibi jirani. Wale familia tukawambia waachane na bifu na bibi, hata kama ni kweli anatumika tu. Tukashughulikia tule tujini akawa mzima na jirani na yeye ni mzima. Na sasa anafamilia mama mchungaji wanakula maisha.

Hizi dini za kuchochea bifu sio za Yesu.
nina wasiwasi hata huto tujini kama kweli tupo mkuu....ni mawenge tu
 
nina wasiwasi hata huto tujini kama kweli tupo mkuu....ni mawenge tu
Ni kweli aisee maana mimi nilikuwa muhusika pale. Wako wanaoigiza na wako wanateswa kweli.
 
.....kuna jamaa yangu aliambiwa mke wake na mtoto wake mdogo ni wachawi.
Huyu Musa wa Temboni ni hopeless sana....kavunja familia ya watu...howcome mtoto wa miaka 8 akawa mchawi.
Hapo ili kumpiga pin, anaweza kuambiwa asimwambie mtu yeyote.

Hata familia isipokaa vizuri inaweza kusambaratika. Shetani anapenda kusambaza familia maana anajua atapata jeshi la watoto wasio na malezi.
Kuendesha zile biashara lazima IQ iwe kubwa kidogo
 
Wasalaam.
Mahubiri mengi kwa hawa mitume na manabii wa kisasa yamejaa uchonganishi, manipulation, saikolojia na neno kidogo. Mengine yote sinashida nayo shida ni hii ambayo pia hata waganga huwa wanafanya. Uchonganishi.


Yaani mtu anaenda kuombewa, muombewaji anaaminishwa kalogwa, mlogwaji anatajishwa aliyemloga wenda ni mjomba, boss, dada, kaka, mama au jirani.
Sasa huyu jirani sio muumini. Hii inaleta chuki, ugomvi, kuviziana na visasi baina ya ndugu na ndugu, ofisini, familia.

Jana nilikuwa napiga story na dreva mmoja anasema yeye alitajwa kuwa anamloga shemeji yake. Akafunga safari kwenda hapo kwa mtume karibu na mbezi ili kama kweli ni muhusika wamtoe huo uchawi. Cha ajabu alipowaeleza wapambe wakamwambia yeye hayamuhusu apotezee. Akasema jambo hilo limeleta mpasuko mkubwa kwenye familia anaonekana no freemason, mchawi na hafai hata simu haipokelewi. Wale machawa walipoona jamaa haelewi, walimuitia mabaunsa wakambeba na kumfukuza kabisa hilo eneo.

Inavyoonekana yule mtoto aliyemtaja no kama alipangwa ili kuvuta wakereketwa kupitia media. Muhusika kufirisika alifirisika kwa kujitakia na anasa, na kanisani haaminiwi anapunwa sadaka tu.
Haya makanisa kwa sababu yanakua kila kona, wote wanatumia tekniki za kùfanana wanaweza kusababisha uchonganishi wa kitaifa na hali ya kuchukiana na kuviziana ikarudisha nyuma kasi ya maendeleo.

Ni hayo tu.
Hivi hakuna sheria inaweza wabana ukiwa sue kwa uchonganishi kama huo?
 
Back
Top Bottom