Mitungi ya Oxygen yawasili Bugando; tusichoke kupaza sauti kuishauri, kuipongeza na kuikosoa Serikali

Mitungi ya Oxygen yawasili Bugando; tusichoke kupaza sauti kuishauri, kuipongeza na kuikosoa Serikali

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
Hapo ni Bugando hospital,imeonekana mitungi inayosemekana ni ya Oksijen ikishushwa.

Ikumbukwe wiki hii nzima kumekuwa na kelele nyingi mitandaoni kuhusiana na ukosefu wa au upungufu wa mitungi hiyo katika hospitali hii na nyinginezo. Ni imani yetu Serikali imelisikia hilo na kulitatua haraka sana.

Kama mwanabodi naipongeza Serikali ya mama Samia kwa kulitatua hili kwa haraka sana, lakini tuendelee kumkumbusha pia aendelee kukubali kukosolewa na watu kuwa huru kutoa taarifa/maoni mbalimbali za msingi na maslahi mapana kwa jamii.

Yasiwe kama ya yule aliyetaka kumpa shuruba raia aliyetoa taarifa ya "ufa wa majengo ya udom" au "ubovu wa barabara kule mbugani"

Kutoka Sabasaba live kwenye uzinduzi wa Tela za Punda ni mimi Shujaa.

=====

Bugando yapokea mitungi 300 ya Gesi, kukabili corona

Hatimaye hospitali ya rufaa ya kanda ya Bugando ya jijini Mwanza imepata msaada wa mitungi 300 ya gesi kwa ajili ya kusaidia wagonjwa wenye matatizo ya upumuaji wakiwemo wa corona

Akizungumza na Nipashe ofisini kwake, Kaimu Mkurugenzi wa Bugando, Dk Fabian Massaga amesema mitungi hiyo imetolewa na Bohari Kuu ya Madawa (MSD).

Zaidi, soma: Hospitali ya Bugando yakumbwa na upungufu wa mitungi ya Oksijeni kwa Wagonjwa wa Kupumua
E512wYRXIAIGzyY.jpg
 
Hii ni ishara kuwa tuna uwezo wa kujenga sanamu ya kule 77.
 
Ikumbukwe wiki hii nzima kumekuwa na kelele nyingi mitandaoni kuhusiana na ukosefu wa au upungufu wa mitungi hiyo katika hospitali hii na nyinginezo. Ni imani yetu Serikali imelisikia hilo na kulitatua haraka sana.
Kuna fundi cherahani mmoja na msaidizi wake walisema hawajawahi kuvuta hewa hiyo na kamwe hawatarajii kuivuta, wakatushauri tunaovuta oxygen tutubu na kuokoka.
 
Hatari tupu!
Hatari na nusu.

Hio mitungi unaweza kukuta ndio iliokwisha oxygen, inasubiriwa gari ijekubeba na ikajazwe tena. Ila habari zimegeuzwa kwamba ndio imefika.

USHAURI:

Kwanini serikali isitengeneze chumba cha kujaza (Re-Fill) mitungi ya oxygen katika kila hospitali ya rufaa. Badala ya kuagiza na kusafirisha mitungi kila kukicha.

Mitungi ya oxygen ikiisha, inaingizwa kwenye chumba maalum wana re-fill oxygen halafu inarudishwa kwa wagonjwa.
 
Dalili mbaya zimeanza kuonekana, ikiwa ni pamoja na hofu ya kukosolewa, mwarobaini ni katiba mpya mengine mbwembwe na kudemka.
 
Hiyo Aya ya tatu mstari wa tatu muhimu sana, akubali kukosolewa pale anapoenda kinyume na matwaka ya katiba.
 
Back
Top Bottom