Mivutano ya katiba na ukweli wa mambo ndani ya mioyo ya wanasiasa

Mivutano ya katiba na ukweli wa mambo ndani ya mioyo ya wanasiasa

Nyakarungu

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2011
Posts
472
Reaction score
377
[h=5]KUTOKA MOYONI MWANGU, KUHUSU MIVUTANO YA KATIBA MPYA!
Soma kwa makini sana UELEWE!

Serikali ya tanganyika ilikuwepo na ikamezwa na muungano, ili kuleta balance hakukuwa na namna zaidi ya kulifunika jina la Tanganyika.

Kwa sasa wapo watu wanaodai serikali ya tanganyika, ukiwauliza wamekosa nini kwa kutokuwepo jina la tanganyika, hakuna jibu zaidi ya kutaka kutajwa kwa jina hilo tu, ambalo kwa sasa halipo kiumbo lakini kiuhalisia Tanganyika ipo na ndio inayoendesha Tanzania.

Wapo Wanaodai serikali yenye dola kamili, yaani tafasiri halisi ni kuwa kusiwepo na muungano tena, mamlaka ya muungano iwe mtumwa wa serikali hizi mbili ndicho wakitakacho wazanzibar, wakidai kuwa tanganyika imewakandamiza na hata hivyo hawataki serikali tatu tu, bali wao shida yao ni dola kamili ya zenji.

WANASIASA
CUF, wanahitaji serikali tatu wakiamini watapata ushindi wa kuongoza serikali ya zanzibar, wakiamini kuwa ccm haitakuwa na nguvu ya ushawishi kwa zanzibar ikiwa katka hali ya serikali tatu (pengine ni kweli na wanaweza kufanikiwa kwa sababu hii)

CHADEMA, wanahitaji serikali tatu, miongoni mwao wapo wanaoidai tanganyika kwa maana ile niliyoitaja hapo juu kuwa wao furaha yao ni kuwepo kwa jina la tanganyika tu na sio kwamba wanajua kuwa tanganyika ndio hii inayoendelea sasa na wala hawana sababu za kuidai wala hawana hitaji la kuwa wanavitu wanavikosa kwa kukosa jina hilo.

Lakini wapo humohumo wanaopiga hesabu za kisiasa na kupata jibu kuwa ccm inafaidika sana na kura za wazanzibar na kwa kuwa chadema yenyewe haina ushawishi na imeshindwa kufanikisha hilo visiwani kwa hiyo ni bora ipatikane serikali tatu ili balance iwepo na ikiwezekana kura za zanzibar ccm zipungue, yamkini watafanikiwa kupata ushindi katika uchaguzi ( kwa hilo bado ni mtihani kwani mpaka sasa takwimu za ccm ni kubwa kulinganisha na chadema huku bara, labda ifikapo 2015 mambo yawe yamebadilika)

CCM , wao nao wamegawanyika makundi mawili, kwa kuwa wote wanapaza sauti za kuitaka katiba iweke muundo wa serikali mbili,
Lakini walioasisi mjadala na kuamua kupigia debe serikali mbili ni wenye ufahamu juu ya siri ya muungano, na wenye kuona ukweli kabisa na hatari ya kuvunjika kwake kama kukiwekwa serikali tatu ambazo zitarahisisha zanzibar itengeneze dola kamili kama inavyodai kwa sasa

kundi la pili ni wanachama na washabiki wanaounga mkono hoja za wakubwa wao, yaani hakuna mwanachama anaefurahi endapo hoja ya chama chake itashindwa na ya chama kingine.

Mwisho kabisa, naupongeza muungano wa vyama vya upinzani, lakini nikiwashauri kuelewa maana halisi ya demokrasia, kwani unapokubali kuingia kwenye uringo wa demokrasia ukubali kushinda au kushindwa.

Maana ya demokraisa sio kuwa mdogo tu ashinde, bali ni kuwa mmoja ashinde.
Hata kwa zengwe mradi ameshinda kwa kura, zengwe ni kiungo mojawapo cha demokraisa ya afrika na ndio sababu hata kwenye chaguzi za vyama vya tanzania kiungo hiki cha zengwe huchukua nafasi kubwa sana.

Na Grayson M. Nyakarungu
KITABU CHA PRACTICE WHAT YOU PREACH KIKO MADUKANI SASA
[/h]
 
Jaribio lako la kuwasiliana nami limeshindwa kwa sababu ya kukosa umakini wa kujieleza upande wako.

I feel like I am reading a bad English translation of a novel originally written in French.

It is possible you have a point to make, but something is lost in translation.

Unless you trully are disorganized and couldn't escape the jumbled diction which truly represent a jumbled mind.
 
jaribio la kuwasiliana nawe kivipi mkuu sijakusoma kabisa
 
Una hakika gani kama CCM bado inakubalika sana huku Bara?Lini ulifanya huo UTAFITI na mikoa mingapi uliitembelea kwaajili ya huo UTAFITI?Msepende kuishi,kufanya mambo na kufikiri kwa kukariri,Mambo hubadilika kulingana na nyakati,Mambo(mazingira na hali maisha) haya na nyakati hizi pia hubadili namna watu wanavyofikiri na kufanya mambo yao.Usifikiri wewe unavyoangalia mambo basi kila mtu anafanya kama wewe.
Labda nikuulize swali jepesi tu!Ikiwa CCM bado inakubalika kama unavyodai basi iweje CCM inatumia nguvu nyingi sana wakati wa kampeni?Kama kwamba hiyo haitoshi iweje Chama hiki ambacho bado ni kipenzi cha Watanzania kitumie mbinu ya kuiba kura ili kishinde chaguzi mbalimbali?Kwanini Chama hiki pendwa kitumie Dola kupambana na Vyama vya Upinzani katika shughuli mbalimbali za kisiasa?Kwa mtazamo wangu Chama chochote kinapokubalika namna hiyo na Wananchi lazima kitajiamini sana,Sasa iweje CCM hii inayopendwa na Wananchi kishindwe kujiamini hivi?.
Mwisho,CCM bado aiheshimu misingi na kanuni za kidemokrasia.
 
Hoja nyingine hujaziona wewe umeona hilo la ccm kukubalika tu? halafu elewa maneno ya kiswahili, naposema takwimu ni tofauti sana na umati kaka mkubwa@ tech wiz
 
Nyakarungu kama sikusahau ukikuwa role model wangu enzi hizo ukiwa ktk kilinge cha bavicha, hata hivyo hasira za mkizi. Niseme tu walau baada ya yale mambo yako tunakujua wewe sasa uko wapi, maana kwa maandishi haya naonyesha matendo yako na matendo hufahamisha zaidi, action speaks louder. Karibu sana maana nakumbuka enzi zile umetoa very professional postmortem analysis ya tarime wale waliokufa kwa risasi za polisi na kulazimisha kuwazika kwa nguvu na ulisimama kidete hakika nilijua tuna mtaalam aliyeamua kwa dhati. Hta hivyo unaweza ukarudi ja kuwa kama enzi hizo karibu sana maana umepotea sana
 
Hoja nyingine hujaziona wewe umeona hilo la ccm kukubalika tu? halafu elewa maneno ya kiswahili, naposema takwimu ni tofauti sana na umati kaka mkubwa@ tech wiz

Kwahiyo hukuielewa point yangu sio?Kwani unapozungumzia mambo ya TAKWIMU kui-favor CCM sio ndio kukubalika kwenyewe huko au?Au Kiswahili kinakupiga chenga ndugu yangu?
 
jaribio la kuwasiliana nawe kivipi mkuu sijakusoma kabisa

Kwanza kabisa, ulipoandika

Kwa sasa wapo watu wanaodai serikali ya tanganyika, ukiwauliza wamekosa nini kwa kutokuwepo jina la tanganyika, hakuna jibu zaidi ya kutaka kutajwa kwa jina hilo tu, ambalo kwa sasa halipo kiumbo lakini kiuhalisia Tanganyika ipo na ndio inayoendesha Tanzania.

Unamaanisha nini? Kwamba wanaodai serikali ya Tanganyika hawana mantiki zaidi ya kutaka jina?

Umesema watu wanataka serikali, halafu unauliza "wamekosa nini kwa kutokuwepo jina la Tanganyika?". Ushasema watu wanataka serikali, unaulizaje swali linaloishia kwenye jina katika jambo linalohusu serikali?

Una maana gani kwa kusema "...kwa sasa halipo kiumbo lakini kiuhalisia Tanganyika ipo na ndiyo inayoendesha Tanzania".

Tanganyika hii kiuhalisia ipo wapi? Imeainishwa kwa katiba gani? Na kama ndiyoinayoendesha Tanzania mbona SMZ ina msemo mkubwa sana katika mambo ya Muungano?

Hapo ni kwa kuanzia tu.

Kauli zako ziko vague, hazieleweki, zinaeleaelea tu, na zinazua maswali mengi kuliko majibu zinazotoa.

Kama unaandika kitabu itabidi kifanyiwe uhakiki maridadi.
 
Kwahiyo hukuielewa point yangu sio?Kwani unapozungumzia mambo ya TAKWIMU kui-favor CCM sio ndio kukubalika kwenyewe huko au?Au Kiswahili kinakupiga chenga ndugu yangu?

Achana nae huyo anaweza kuwa katafuna bangi mbichi manake huko kwao ziko nyingi nani alimwambia sisiem inakubalika? kati ya raia milioni 45 rais wao kachaguliwa na milioni tano sijui au chini yapo hapo sasa huo ukubali uko katika sura ya vitenge na kofia au wingi wa bodaboda. Huku bara sisiem itashinda tu kwa nguvu ya dola na fedha hata miaka mingine hamsini ijayo lakini sio kwa kukubalika. Leo hii wanaleta wachina majukwaani kutuletea mauzauza kwa kuwa haohao ndio mabingwa wa uchakachuaji wa bidhaa mpaka masanduku ya kura
 
Back
Top Bottom