Miwasho sehemu za siri

mchumi tumbo

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2018
Posts
832
Reaction score
992
Habari ya wakati huu.
Nina mwenza wangu (KE) anasumbuliwa na tatizo la kuwashwa ukeni(pembeni mwa uke kwa nje). Tumeenda hospitali mara kadhaa lakina tatizo limekuwa likijirudia rudia tu. Naleta kwenu kwa ambaye anafahamu chanzo cha tatizo, tiba na ushauri asisite kutoa maana hili tatizo lamletea discomfort sana likianza.
NB:hakuna discharge yeyote ni miwasho tu ambayo inapelekea michubuko kutokana na kujikuna. Umri wake ni 25years.
Nawasalisha
 
Hospital walisema ana ugonjwa gani?

Abadilishe chupi anazovaa avae chupi mpya cotton na ahakikishe anakua mkavu akioga ajifute maji huko

Inaweza kua anachotumia kushave, uti au maradhi mengine yoyote yale

Alipewa dawa zipi??
 
Hospital walisema ana ugonjwa gani?

Abadilishe chupi anazovaa avae chupi mpya cotton na ahakikishe anakua mkavu akioga ajifute maji huko

Inaweza kua anachotumia kushave, uti au maradhi mengine yoyote yale

Alipewa dawa zipi??
Kuna dawa za kuinsert kwenye vagina jina limenitoka na aliwahi pewa vidonge pia
 
Kuna dawa za kuinsert kwenye vagina jina limenitoka na aliwahi pewa vidonge pia
Hizo dawa anatakiwa akitumia usifanye naye mapenzi mpaka amalize doz akae kidogo kama wiki atumie tena mkuu maybe ni fangasi hao abadilishe chupi anazovaa akiwa anatumia doz pia
 
Hospital walisema ana ugonjwa gani?

Abadilishe chupi anazovaa avae chupi mpya cotton na ahakikishe anakua mkavu akioga ajifute maji huko

Inaweza kua anachotumia kushave, uti au maradhi mengine yoyote yale

Alipewa dawa zipi??
Tatizo halisi hawakusema walisema infection tu sasa hiyo infection ya nini yeast, bacteria or what ndo haijulikani
 
Hizo dawa anatakiwa akitumia usifanye naye mapenzi mpaka amalize doz akae kidogo kama wiki atumie tena mkuu maybe ni fangasi hao abadilishe chupi anazovaa akiwa anatumia doz pia
Ahsante kwa ushauri wako nitautendea kazi madam
 
Inaweza kuwa fangasi hiyo mkuu.

Kuna mwingine alikuwa na dalili kama hizo na alitumia dawa za kuweka na kumeza za kila aina ila hazikusaidia mwisho wa siku kuna dinspensary alienda wakamchoma sindano akapewa na dawa za kumeza leo imebaki stori.

Nendeni tena hospitali braza.
 
Mm nimekuwa nikisumbuliwa mbuliwa na tatizo hilo karibu miaka saba sasa ngoja narudi nije kakupatia maelezo vizuri kwani maramwisho nilienda Hindu Mandal hospital dokta akafanya uchunguz na kusema sio fungus walikuwa wakinisumbua Kuna tatizo alinitajia ntaenda kukuangalizia kwenye vyeti vyang vya hospital na kusema kwamba nahitaji dawa za muda mrefu kama miezi mitatu hivi ili tatizo langu liweze kuisha
 
Nakusubiri mkuu
 
Nakusubiri mkuu
Ni hivi mkuu nilipoenda hospital kwanza kabisa dokta aliniambia kwamba shida yangu kitalaam inajulikana kama Tinea Cruis na dozi nlizikuwa napatatiwa zisingeweza kuondoa tatizo bari kupunguza tu na baada ya muda itajirudia. Kwahiyo dokta aliamua kuniandikia dozi ya muda mrefu yaan miezi mitatu ili tatizo liweze kuisha. Dokta alisema kwamba ntatumia dawa ya kupaka na vidonge mwezi mzima mfurulizo na pia baada ya hapo ntaanza kutumia poda kupaka na hadi pale miez mitatu itapoisha inshallah mambo yanaweza kuwa sawa kwa sasa nko ntaendelea na doz na hari yang inaendelea vzuri huu ni ushauri wangu kwan kipindi chote hicho nlijua nasumbuliwa na fungus kumbe sio fungus
 
Nimechimba kuhusu huo ugonjwa ulioutaja hapo naona kutumia vitunguu maji au swaumu yasaidia pia ukivipaka kwa muda then ukaviondoa kwa maji hii imekaaje?.,,
 
pole sasa hapo unakuta manzi anakausha anakutana na jamaa yake mtu ana ingia chumvini πŸ˜΅πŸ˜΅πŸ™πŸ™
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…