MJADALA: Je, Pikipiki gani ni bora kwa matumizi ya nyumbani au biashara kwa Tanzania?

Shukrani kwa maelezo mujarab kaka.... Safiiii
 
SUNLG 150 hutojuta. Moo wake tu ni burudani tosha.
 
Hahahahhaha! Eti miluzi ikawa mingi......nimecheka sana
 
nipe bei ya Honda ace.
 
Swa
Swali langu Lina maana nzuri tu labda Kama hukutaka kulitafakari, Nina miaka nane naendesha pikipiki na hizo boxer na TVS Nina experience nazo kwa miaka minne Sasa.
Mkuu bora nimekupata.

Mimi bhana sina uzoefu na chochote zaidi ya daladala na time za kuwa usafiri shida au afadhali.

Naomba utujibu maswali yetu kwa sisi ambao tuna ndoto za kumiliki vipikipiki mkuu mana kujua ABC ni muhimu sanaaa.


Unasemaje kwa chombo kama hiki hapaa chini udhaifu na uafadhali wake..?

 
Hizi nimeplan ninunue miaka ya mbele.
Zimeenea sana huku visiwani na ziko poa.

Ila sasa nataka nijue udhaifu wake na ubora wake kwa wazoefu kabla ya kununua.

Vp mkuu na wewe unataka uvute hii kitu?

Mana naskia wanasema hazinywi mafuta kabisa,sasa tungepata wataalamu ingekuwa powa sanaa
Hazina mnyororo na ni autoView attachment 1123367
 
TVS gharama kubwa ipo kweny spear aisee.... ninayo 150 mpya sithubutu kumpa mtu aiguse, nilikuwa na 125 nikakaa nayo miaka 5 bila kuiharibu siku nilimpa mtu ikarudi skrepa ndani ya masaa mawili tu,.... PIKIPIKI NI SERVICE NA USTAARBU KWENYE KUENDESHA SIYO KUKIMBIZA KAMA MAJAMBAZI. tvs ni nzuri sana ukiitunza isikugarimu spear. Ninayo mwaka sasa haijaharibika chochote.
 
Naomba kufaham kuhusu maintenance ya pikipik kwa ujumla, hususan boxer au tvsn mfano services inakuaje? Masuala ya kubadilisha oil, Ujazaji wa oil, usafishwaji wa injin au chombo chenyewe n. K....pia itakuwa vyema kueleza tatzo kubwa kwa aina flan ya pikpk....

Wazoefu na wajuvi wa hiv vyombo (pkpk) bb nawakaribisha kwa elimu... Karbun.....
 
Boxer inatumia kilometers 45 kwa lita
labda hizi ndogo cc 100/125 lakini 150 mkuu haiko zaidi ya 40 na hapo rpm usiwe unaisogelea kati. yaani kph iwe <70. angalau masafa marefu na speed ya 110 (dashboard ni 10 lakini ile ya kinglion 180 unampita kama amesimama) itakufikisha 35-38 bila mzigo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…