MJADALA: Je, Pikipiki gani ni bora kwa matumizi ya nyumbani au biashara kwa Tanzania?

Nilitaman mvuto pia ili kulinda status yng
UIMARA/HADHI/BANA MATUMIZI
kwa hadhi mkuu chukua Honda. zipo ndogo za cc 100, 125, 150 models mpya zilizoundiwa body kama pikipiki nyingi za mchina/india.

pia ni economical kwa mafuta kufikia 60-70 km/lt japo bei yake kiasi imechangamka. bei za kati ni 3-5m.

raha ya honda ni mkataba: hakuna uharibifu wa reja reja. unabaki na jukumu la oil exchange, filters, kusafisha air cleaner, chain adjustmen na petrol. sio rahisi kukutana na kukata shock up, cable, kuunguza clutch, kumaliza brake shoe, sprokets ndani ya mwaka.

wale yange yange pia sio wasumbufu upande wa hizi.

PUNDA/ROHO YA PAKA/RAFIKI WA OFF ROAD/MAFUNDI WENGI, VIPURI CHEE/HAPO KAZI TU
sanlg, sunlg, houjue(sina hakika speling), tan hero, kinglion, fekon

bei nafuu dukani kulinganisha na aina nyingine.

zina mtetemo (nyingi zina mfumo wa pushrods) hazifai kwa masafa, utachoka sana kiuno, mgongo, mikono hasa kwa wasio na uzoefu wa masafa.

kelele kubwa ya injini tofauti na tvs, boxer, honda

hizi kubebeshwa hadi kg 300 (kutegemeana na ujuzi/uzoefu wa dereva)

vipuri vipo kila kona na mafundi wengi wanazijulia. hata bila sevisi ya maana dude linatembea tu. wapo wanafunga hata kwa kamba likikata baadhi ya spea linakata milima tu.

haidumu muda mrefu sababu ya suluba zinazokutana nazo.

MASAFA/LIGI/CHOTARA
boxer (cc100, 125, 150 old na new)

*sina uhakika kama zipo za pushrods.

zinafaa sana kutembelea tu au kubeba mizigo isiyozidi 70kg (uzito wa abiria mmoja)

ni nyepesi sana, hazishiki barabara, ni rahisi kuhamishwa barabara maeneo yenye upepo. ##ilinitokea biharamulo 2016)

very and dangerous in terms of speed.
(ina mwendokasi usio wa kawaida japo dashboard ni kama inadanganya. inasoma 110 tu lkn wa magari mnatoana jasho)

inapenda kujaliwa sana (chotara) haitaki ubahiri kwenye spea na sio kila fundi anatengeneza kwa ubora. vipuri vyake ni aghali.

narudia tena; haipendi mizigo maana inapoteza spidi na huchakaa mapema

TVS hizi za kisasa sijawahi kutumia, sina uzoefu. waje wenyeji wake. ila nilimiliki na kutumia old model cc 100 na 110. sifa kama boxer. tofauti yake ni matumizi kidogo ya mafuta, starehe barabarani kwa shock ups zinazonesa kwa maringo lkn spea mmmh waweza kukimbia.

MWISHO.
uhai wa chombo huongezeka kulingana na matunzo na kujali kwa mtumiaji.
 
Mm
nmeshangaa hizo data sijui amezitoa wapi. Boxer inatembea mpaka 60km/lt. Ni Kati ya pkpk zenye cc150 na zinakula mafuta kidogo sn
mkuu hatukukatalii lkn boxer zipo na varieties. ukitaja boxer akili ya wengi inasoma cc150. hii ni km 40 kwenda chini.

hiyo unayosema wewe ni boxer cc 100 inaweza kufikia hadi 70km/lt kwa mwendo wa kutomaliza accelerator nzima. lkn kumbuka mtoa mada kasema analinda HADHI/STATUS/PROSPERITY yake. huwezi kumpandisha cc 100 yenye mwonekano km honda 110. kwanza kiko chini na siti iko flat kuanzia mkiani hadi kwenye tenki. unaweza kubeba watu hadi 5 body inaruhusu. (refer avatar ya watu 8), taa ipo kama kibatari na dash board sio classic km cc 150 old. japo cc 150 new model imeboreshwa zaidi kimwonekano. iko juu. kwa wale wa watefu inapendeza sana. pia kupita rough roads/off roads inaacha vumbi tu km ikipata mtekenyaji mzuri.
 
mengi tumeshakutajia mkuu. humu unganisha fikra ufanye maamuzi yako. ukiendekeza kila kitu uambiwe mwishowe utakosa la kufanya.

mimi nimekupa yangu kama mzoefu kimatumizi toka 2003 hadi sasa natumia pikipiki, sina gari, mara chache naendesha ya wadau lkn naukubali utamu wa pikipiki kuliko gari tofauti na kero za mvua.

pia mafundi na wauzaji wameshabwaga yao.

ukichambua kwa umakini utagundua washauri wengi wanapendekeza umiliki aina walizo nazo bila kuzingatia vigezo vyako ulivyoainisha ktk main post. hivyo kazi ni kwako.

NYONGEZA:
service ya maana ni ku-fix lolote kabla hakijaleta madhara, ukisubiri sana ukaendeleza kutembelea tatizo huzaa mengine.
mf. upepo mdogo hichana tairi na kuvinba/kutunishwa nyaya au kupasuka au kukata nali.

oil rojorojo (zaidi ya km 1000) huchakaza/ziba filters na kuzalisha moshi au kuunguza piston rings, plugs kuungua na kukosa nguvu.

jenga mazoea ya kuhudumiwa na fundi mmoja kwa service ya uhakika labda ukiwa mbali naye kwa dharula.

jenga hulka ya kutomwamini fundi. asikununulie spea nunua mwenyewe yeye awe mfungaji. aghalabu wanakula na wenye maduka. unatozwa bei ya spea halisi anakufungia bomu ya bei chee anajilia chenji na huku unamlipa kabhour charges, ukitembea km chache unarudi kwake.

jenga tabia ya kujifunza kutambua hitilafu kabla ya kupeleka kwa fundi. wapo wanaobadili spea. mf unaenda kubadili rings za piston unamuachia chombo, anafungua plates au plugs zako org. anamufungia mteja mwingine. hii ni tabia ya mafundi wengi hasa watz ndio waizi waizi toka tumeacha kunyonya.

usimpe ovyo mtu baki usafiri wako. wewe ndiye unayejua thamani na umuhimu wa hicho chombo. wapiga norinda kwenye lami, wacheuaji na upanguaji wa fujo mara nyingi. vyombo si vyao-wamekodi. fikiria kwanini iwe ngumu kumkabidhi mtu hata memsahibhu pochi yenye 1,500,000 akushikie ukienda msalani lkn iwe nyepesi kumpa ignition key mtu. aburuze boxer yako uliyotolea 2.3m eti aisikilize!!

thamini vyako hata kama utasemwa au wakiona ni cha bei chini. wangapi hawana? A MAN BRAGS HIS PENIS HOWEVER TINY (usitafsiri kwa kiswahili hii sio mada ya Piston)
 
 
Mkuu namaanisha boxer bm 150 na nna uhakika nayo kwasababu ndio nayotumia kwa miaka minne sasa, hiyo ya cc100 hata siijui kabisa hata mwonekano wake
 
Je nikichukua Haujue for personal use..maana jmosi tu hii nlifanya survey ya bei pia..my budget 2M mpaka 2.5 ila sitaki boxer na TVS sasa hizi zingine sijajua ipi imara sana aila mtumizi private tu sio business..tena hapa Dar kwennda kurudi kazini..route za ghafla na misele mingine
 
Pikipiki imara na bora ni Honda ikifuatiwa na Yamaha na jamii ya Suzuki.Tatizo bei zake na hata vipuli vyake ni ghali.
Nilianza na HOnda click 125 na 150 ndio first choice...sa hivi nina Yamaha pia....then nimejikuta nipo na hizi fekon, sankg na haoujue katika choices...naona Honda zimepungua madukani...advice sasa ipi niichukue next month for non-commercial use
 
Mi nilijua zinazungumziwa pikipiki za maana kama vile Harley Davidson, Kawasaki, yamaha,Honda, ducat,BMW kumbe huu uchafu wa mchina na muhindi
tumekomaa na Honda ila sasa uchumi umetubana arifu..acha tupambane tu na hizo za wanafunzi wa prrimary wa China 😆
 
hapa umejibu vizuri sana..jumlishaprice hapo mtu anafanya maamuzi sahihi..mfano nishaona itanpa shida mimi kwa kuanzia kwa sababu ulizotaja hapo
 
Honda Cbr
Suzuki Hayabusa
KTM
MV Augusta
Kawasaki Ninja
BMW Adventure
Aprilia
Harley Davidson
Hizo ndio pikipiki achana na takataka za mchina
hivi hapa si ni sawa na unasemea V8, Prado, Harrier na zingine kubwa kubwa au? yani zile za gaharama af hizo zingine ndio kama IST, Starlet, etc
 
Haojue is the option kama unataka na baadae ufanyie biashara, ila kwa boxer kama unataka kutumia mwenyewe na uje kufanyia biashara sikushauri kwani zinawahi kuchoka na spare zake ni ghali
Je Haojue kwa binafsi tu na baadae ibaki kuwa binafsi tu no biashara..haitafaa maan naona wanasema ni ngumu inafaa kwa binafsi na baishara...kwa kuitumia tu mishe zako kazini misele vipi.
 
kwa nini Haojue ni nzuri kwa biashara maana ninawaza niichukue kwa matumizi binafsi
 
Mkuu umejibu na kuelezea vizuri sana> ya kwanza hiyo niliipenda sana ila gharama sasa, pia hadhi sawa ila siwezi lazimisha kuonekana niko kwenye chombo cha hadhi af maisja yangu ya ovyo ovyo...bora nimaintain quality life kuliko show ya hadhi...jili moja

na hizi paka roho hizi sasa Hazidumu muda mrefu sababu ya shoruba au shuguli...sasa je nikiitumia hi kwa matumizi binafsi..hasa ukizingatia suala la hadhio mi lipo kwenye kuongea statuz ya kazi na ofisi niliyopo ila kwa chombo navunga i dnt care..sawa sawa na nina IST au startlet tu ofisini sawa haina hadhi ila mimi nin hadhi kwa inputs na position.

za mwisho chotara hizi nakausha kwanza

Anyway tukiondoa suala la hadhi je fekon au Haoujue ni imara kuwa nayo na spare zake zipo etc. kwa matumizi binafsi lakini

Honda spare zikoje///maana naipenda ila bei zake ndio nakausha tu...pia naona zimekuwa adimu madukani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…