Mjadala juu ya Mustakabali wa Akili Mnemba (AI)

Mjadala juu ya Mustakabali wa Akili Mnemba (AI)

Joined
Apr 6, 2020
Posts
16
Reaction score
48
Wakati wengi wanakubali kuwa Akili Mnemba (AI) ina uwezo wa kuleta mapinduzi ya viwanda na kuboresha maisha, kuna wasiwasi unaoongezeka juu ya athari za kimaadili na usalama wa maendeleo yake ya haraka.

Tarehe 25/09/2024 itakumbukwa sana katika historia ya dunia kama siku ambayo mabadiliko makubwa yalitokea katika ulimwengu wa teknolojia. Hii imekuja hivi karibuni baada ya kampuni maarufu duniani, OpenAI, inayojihusisha na masuala ya Akili Mnemba kutangaza kuwa inahama kutoka mfumo wa biashara usio wa faida hadi mfumo wa biashara wa faida.

Kumetokea na mabadiliko makubwa pia katika mfumo wake wa uongozi. Kampuni hii ndiyo iliyogundua mfumo maarufu wa ChatGPT ulioleta mapinduzi chanya kwenye teknolojia. Afisa Mkuu wa Utafiti wa OpenAI, Bob McGrew, na Makamu wa Rais wa Utafiti, Barret Zoph, waliacha kazi katika kampuni hiyo siku ya Jumatano (Septemba 25, 2024), saa chache baada ya Afisa Mkuu wa Teknolojia wa OpenAI, Mira Murati kutangaza kuwa ataondoka.

Elon Musk, Mkurugenzi Mtendaji wa Space X na mmoja wa waanzilishi wa Open AI alipinga mabadiliko ya hivi karibuni ya Open AI. Kupitia chapisho la X (zamani, twitter) Musk alisema kuwa: "Huwezi tu kubadilisha biashara isiyo ya faida kuwa faida. Hicho ni kinyume cha sheria."

Mtumiaji mwingine wa X aliyethibitishwa pia anaandika kujibu chapisho la Elon Musk X:

"Kwa hivyo wacha nielezee hii moja kwa moja, OpenAI inaamua kuwa kampuni ya faida sasa. Afisa Mkuu wa Teknolojia, Mkuu wa utafiti, na Makama wa Raisi wa mafunzo na utafiti wote huamua kuondoka siku hiyo hiyo hii inatangazwa. Sam Altman (Mtendaji Mkuu wa OpenAI) anapata malipo ya $ 10.5B (7% ya kampuni) siku hiyo hiyo. Nadhani Sam alifanya kitu."

AI Elon Musk Post.png

Nini maoni yako kuhusu haya mabadiliko? Karibu tujadili.


Je unadhani mabadiliko haya yana athari gani katika jamii yetu ya sasa?
 
Nashukuru kwa kupata nafasi hii ili kutoa mchango wangu juu ya yale yote yaliyowasilishwa na mtoa mada hapo juu.
ninachoweza kusema ni kwamba matumizi ya akili nemba yamekuwa na mchango mkubwa sana kwenye maisha ya watu wengi. nitatoa mfano kwangu mimi binafsi kama mtu nisiyeona, kujua matumizi ya akili nemba kumeniwezesha kupata urahisi kwenye kuchanganua taarifa mbalimbali zinazopatikana mtandaoni ambazo hapo mwanzo sikuwa na uwezo wa kufanya.
mfano halisi hivi sasa ninaweza nikatambua nini kipo katika picha mbalimbali kwa usahihi zaidi tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.
kingine, matumizi ya nakala laini zenye maudhui ya graph au vitu vingine vyenye michoro ninaweza kupata maelezo yake kwa usahihi zaidi tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.
Jambo jingine ni matumizi ya visoma screen yaani screen readers ambavyo hutumia sauti yani text to speech engines vimeboreka zaidi. Ambapo, ubora wa sauti hizi unaniwezesha mimi kufanya shughuli zangu kwa utulivu. kwa sababu sauti zinapokuwa na mfumo wa kiroboti yani robotic voices ninakuwa sifurahii matumizi ya sauti hizo.
lakini kwa nchi zetu za ulimwengu wa tatu kama tanzania na kwingineko bado maendeleo ya sayansi na teknolojia hasa matumizi ya internet yako chini. nchi imefanya jitihada sana katika kuongeza upatikanaji wa umeme. kwa maoni yangu hili lingekwenda sambamba na upatikanaji wa huduma ya internet kokote kule umeme unakufika. kwa njia ya hizi cable angalau ingepunguza gharama za matumizi ya intaneti. ulimwengu wa sayansi na teknolojia hasa matumizi ya akili nemba hayawezi kuwa endelevu kama huduma ya internet itabaki kutegemea vifurushi vya simu za mkononi ambavyo sio marobaini sahihi wa maendeleo haya hasa kwa vizazi vijavyo. asanteni
 
Nashukuru kwa kupata nafasi hii ili kutoa mchango wangu juu ya yale yote yaliyowasilishwa na mtoa mada hapo juu.
ninachoweza kusema ni kwamba matumizi ya akili nemba yamekuwa na mchango mkubwa sana kwenye maisha ya watu wengi. nitatoa mfano kwangu mimi binafsi kama mtu nisiyeona, kujua matumizi ya akili nemba kumeniwezesha kupata urahisi kwenye kuchanganua taarifa mbalimbali zinazopatikana mtandaoni ambazo hapo mwanzo sikuwa na uwezo wa kufanya.
mfano halisi hivi sasa ninaweza nikatambua nini kipo katika picha mbalimbali kwa usahihi zaidi tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.
kingine, matumizi ya nakala laini zenye maudhui ya graph au vitu vingine vyenye michoro ninaweza kupata maelezo yake kwa usahihi zaidi tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.
Jambo jingine ni matumizi ya visoma screen yaani screen readers ambavyo hutumia sauti yani text to speech engines vimeboreka zaidi. Ambapo, ubora wa sauti hizi unaniwezesha mimi kufanya shughuli zangu kwa utulivu. kwa sababu sauti zinapokuwa na mfumo wa kiroboti yani robotic voices ninakuwa sifurahii matumizi ya sauti hizo.
lakini kwa nchi zetu za ulimwengu wa tatu kama tanzania na kwingineko bado maendeleo ya sayansi na teknolojia hasa matumizi ya internet yako chini. nchi imefanya jitihada sana katika kuongeza upatikanaji wa umeme. kwa maoni yangu hili lingekwenda sambamba na upatikanaji wa huduma ya internet kokote kule umeme unakufika. kwa njia ya hizi cable angalau ingepunguza gharama za matumizi ya intaneti. ulimwengu wa sayansi na teknolojia hasa matumizi ya akili nemba hayawezi kuwa endelevu kama huduma ya internet itabaki kutegemea vifurushi vya simu za mkononi ambavyo sio marobaini sahihi wa maendeleo haya hasa kwa vizazi vijavyo. asanteni
Umenena vyema
 
Ulipokuwa ukiingia Vhathpt wdliandoka try chat gpt. Ina maana sasa tutaanza kuilipia huduma . Au kina huduma hatutalipia.
Tutalipiaje huduma ambayo nao wamekopi data za wengine ! Wamekopi vitabu mbsli mbali kuiwezesha gpt. Inawezekana hata maoni yetu ya JF yakawa yanrlishwa Chatgpt. Aftika nasi tuwe macho. Yuanzishe AU zetu ili tusiwe watumwa wa wazungu.Wenzetu Asia hawasubiri mzungu awaundie AI nao wapo busy sisi Afrika tumelala
 
Wakati wengi wanakubali kuwa Akili Mnemba (AI) ina uwezo wa kuleta mapinduzi ya viwanda na kuboresha maisha, kuna wasiwasi unaoongezeka juu ya athari za kimaadili na usalama wa maendeleo yake ya haraka.

Tarehe 25/09/2024 itakumbukwa sana katika historia ya dunia kama siku ambayo mabadiliko makubwa yalitokea katika ulimwengu wa teknolojia. Hii imekuja hivi karibuni baada ya kampuni maarufu duniani, OpenAI, inayojihusisha na masuala ya Akili Mnemba kutangaza kuwa inahama kutoka mfumo wa biashara usio wa faida hadi mfumo wa biashara wa faida.

Kumetokea na mabadiliko makubwa pia katika mfumo wake wa uongozi. Kampuni hii ndiyo iliyogundua mfumo maarufu wa ChatGPT ulioleta mapinduzi chanya kwenye teknolojia. Afisa Mkuu wa Utafiti wa OpenAI, Bob McGrew, na Makamu wa Rais wa Utafiti, Barret Zoph, waliacha kazi katika kampuni hiyo siku ya Jumatano (Septemba 25, 2024), saa chache baada ya Afisa Mkuu wa Teknolojia wa OpenAI, Mira Murati kutangaza kuwa ataondoka.

Elon Musk, Mkurugenzi Mtendaji wa Space X na mmoja wa waanzilishi wa Open AI alipinga mabadiliko ya hivi karibuni ya Open AI. Kupitia chapisho la X (zamani, twitter) Musk alisema kuwa: "Huwezi tu kubadilisha biashara isiyo ya faida kuwa faida. Hicho ni kinyume cha sheria."

Mtumiaji mwingine wa X aliyethibitishwa pia anaandika kujibu chapisho la Elon Musk X:

"Kwa hivyo wacha nielezee hii moja kwa moja, OpenAI inaamua kuwa kampuni ya faida sasa. Afisa Mkuu wa Teknolojia, Mkuu wa utafiti, na Makama wa Raisi wa mafunzo na utafiti wote huamua kuondoka siku hiyo hiyo hii inatangazwa. Sam Altman (Mtendaji Mkuu wa OpenAI) anapata malipo ya $ 10.5B (7% ya kampuni) siku hiyo hiyo. Nadhani Sam alifanya kitu."

View attachment 3110965
Nini maoni yako kuhusu haya mabadiliko? Karibu tujadili.


Je unadhani mabadiliko haya yana athari gani katika jamii yetu ya sasa?
Kwa sasa najifunza zaidi.

Nasoma kitabu kipya cha Dr. Yuval Noah Harari "Nexus: A Brief History of Information Networks from the Stone Age to AI".

Dr. Harari anaonya na kuasa kuwa tunahitaji kupunguza speed ya kutengeneza AI networks na kujikita zaidi katika kuelewa madhara yake na jinsi ya kuyakabili kwanza kabla hatujazidiwa kabisa uwezo na hii teknolojia.

Gazeti la The Guardian la UK limeweka review ya jitabu hiki hapa.


Kitabu kingine muhimu ni "The Singularity is Nearer" cha Ray Kurzweil. Hiki kinafuatia "The Singularity is Near" alichoandika na kutabiri haya mambo mengi miaka kama 20 iliyopita.

 
Back
Top Bottom