Uchaguzi 2020 Mjadala mkubwa juu ya kuenguliwa kwa wagombea wa vyama mbalimbali

Uchaguzi 2020 Mjadala mkubwa juu ya kuenguliwa kwa wagombea wa vyama mbalimbali

Singo Batan

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2020
Posts
295
Reaction score
198
TAHADHARI KWA NEC UCHAGUZI MKUU 2020

Siku za karibuni pameibuka mjadala Mkubwa Juu ya kuenguliwa kwa Wagombea wa vyama mbalimbali.

Pamoja na Ukweli kwamba Kuenguliwa huko kumezingatia ufuataji wa Katiba ya Nchi na Sheria za Uchaguzi, lakini kuna Mtego umewekwa Tume ionekane haitendi haki katika utekelezaji wa majukumu yake kisheria na upande wa pili, Vyama vibebe Agenda hiyo na kuitangaza sana kwamba vinaonewa na Tume.

Maelekezo haya ya siri yanatolewa na Viongozi wa ACT- Wazalendo & CHADEMA ambao waliwataka;
1. Wagombea wa baadhi ya kata na Majimbo kutojaza taarifa zao katika fomu namba 8B kwa Wagombea Ubunge na C kwa Wagombea Udiwani, ikiwa ni pamoja na kujaza majina ya Uongo na Tarehe za kuzaliwa zinazo kinzana na Taarifa za Nida nk

2. Kushindwa kuweka viambata muhimu katika fomu namba 8B na C Mfano Picha, Fomu namba 10 ya Tamko la Mgombea kukubali na kuheshimu Maadili ya Uchaguzi, "pay in slip" ya malipo ya dhamana nk. kujaza Wadhamini feki, Kutopitisha Fomu na. 8 kwa Hakimu ili asaini na mambo mengine.

Maelekezo haya yalitolewa Makusudi ili Wagombea wengi wakishaenguliwa pawepo na taharuki kwa wananchi, hivyo vyama hivi vitapata kura za Hasira kwa kigezo kwamba Tume inashirikiana na CCM kuvionea Vyama tajwa.

Lengo kubwa hapa sio kushinda Urais,Ubunge au Udiwani bali vyama hivi vipate kura nyingi zitakazovipatia Ruzuku.

Na kwakuwa Wananchi wanaaminishwa kwamba vyama vya ACT Wazalendo na CHADEMA vinaonewa, wanaweza wakasusia kupiga Kura hivyo Dunia itafahamishwa kwamba NEC imeharibu Uchaguzi kwa kuipendelea CCM.

Malalamiko mengi yaliyopo sasa ni kuishinikiza NEC ivunje Sheria na kutoa Favour kwa Wagombea waliokosa sifa baada ya kuomba kuteuliwa, Jambo ambalo litaharibu credibility ya TUME.

Mimi ni mwananchi ninayeona hila na mipango ovu ya wanasiasa uchwara. Madhara ya chokochoko hizi sio tu zitadhoofisha juhudi za Tume kufanikisha Uchaguzi Mkuu, bali kuleta chuki na kuzua vurugu nchini mwetu. Hatutaki tufikishwe huko,Tume ya Taifa ya Uchaguzi simameni Imara!
 
Tume kweli simamieni kanuni na Sheria za Uchaguzi pasi na kupepesa macho wala kusaga magego.

Mfamo mzuri kwa hivyo vyama vya upinzani tuliona tangu mwanzo. Mmoja wa wagombea aliuaminisha uma kua Tume imepanga kunyima Fomu lakini Tume ikampa, akaja kusema Tume imepanga kumuengua kugombea, lakini kwakua alitimiza vigezo japo tulisikia aliisumbua Sana Tume lakini ikampiyisha hivyo wanatafuta Huruma tu za wananchi. Wanaeneza chuki na uhasama.
 
Wafadhili nao Wanalalamika

20200910_200222.jpg
 
TAHADHARI KWA NEC UCHAGUZI MKUU 2020

Siku za karibuni pameibuka mjadala Mkubwa Juu ya kuenguliwa kwa Wagombea wa vyama mbalimbali....

Kama tume infahamu hizo mbinu kwanini isiwaelekeze kurekebisha kasoro hizo badala ya kuwaengua ili kufanikisha mpango wa hiyo taharuki inamaana wakirekebisha hizo kasoro si ndiyo wananchi watachagua hao wa ccm wanaopendwa kuna shida gani badala ya kuanza kuwa na wabunge wa kuteuliwa tena wababa wazima kuwakilisha tume bungeni ili iweje maana wananchi hawajawachagua hivo hawawezi kuwa Kuwawakilisha bila kuwachagua. Hili kundi la wabunge halipo hata kwenye makundi ya wabunge wanaoruhusiwa katika katiba yetu
 
Asante kwa kuielewa hii Mkuu. Lengo ni kuwafahamisha Tume wawe smart zaidi ya mipango iliyo nyuma ya pazia
20200910_200222.jpg
 
TAHADHARI KWA NEC UCHAGUZI MKUU 2020

Siku za karibuni pameibuka mjadala Mkubwa Juu ya kuenguliwa kwa Wagombea wa vyama mbalimbali...
Kuna mambo huwa yananichanga sana yaani sanaa

Kila uchaguzi kuna chama cha Kijani kinadai kinatuletea Tanzania Mpya.

Nafikiri huwa wanamaanisha upya wa matatizo, ujinga na umaskini.

Fikiria kwa miaka 55+ sasa - wanasema tusichague wengine kwa kuwa wataondoa amani lakini wakati chini ya utawala wao wa kiimla tuna WASIOJULIKANA,VIROBA FUKWENI, Disapperance of Azory , kutapeliwa korosho zetu, Kuvunjwa haki za binadamu na sheria mbaya za ovyo ovyo
 
TAHADHARI KWA NEC UCHAGUZI MKUU 2020

Siku za karibuni pameibuka mjadala Mkubwa Juu ya kuenguliwa kwa Wagombea wa vyama mbalimbali.

Pamoja na Ukweli kwamba Kuenguliwa huko kumezingatia ufuataji wa Katiba ya Nchi na Sheria za Uchaguzi, lakini kuna Mtego umewekwa Tume ionekane haitendi haki katika utekelezaji wa majukumu yake kisheria na upande wa pili, Vyama vibebe Agenda hiyo na kuitangaza sana kwamba vinaonewa na Tume.

Maelekezo haya ya siri yanatolewa na Viongozi wa ACT- Wazalendo & CHADEMA ambao waliwataka;...
 
CCM ni mabingwa wa misemo mingi kama "wanatumiwa na mabeberu", "wanasiasa uchwara" wakati ukija kwenye reality miaka 60 toka tupate uhuru hatuna huduma za afya za kueleweka, kwetu mpaka leo tunatumiwa hospitali walizojenga wamishenari enzi za Richard Turnbull; tunatumia madaraja ya enzi za "Missing in Action" ya Chuck Noris!

Aibu zaidi juzi juzi nimepishana na msafara wa wenye mamlaka na magari yao ya kifahari lakini gari la wagonjwa wanalolitegemea ikitokea dharura lina plate number ya DFP.

Kwa wale wasiojua kirefu cha DFP ni Donor Funded Project, ikiwa na maana Ambulance hii imenunuliwa kwa pesa za wale ambao "mapundaka" wanapenda kuwaita mabeberu!!!
 
Back
Top Bottom