Kuna thread niliileta nikikemea kuwa kuwa walimu wa msingi hawakufeli kidato cha 4,wengi wamesema walimu walifeli.Hoja yangu leo je, ni hao walimu tu ndiyo wanazorotesha elimu ya TZ?
Mjenga nchi ni mwananchi: serikali ya awamu ya tatu ilitoka na sera ya ujenzi wa vyule vya kata. Mjenzi mkuu wa shule hizo walikuwa wananchi baada ya hapo upande wa pili yaani serikali ikatega mgongo bila kufuatilia nini kinachoendelea kwenye shule hizo kazi kubwa ikawa ni kuproud majukwaani kuwa tumeongeza udahili kwa level ya secondari. lakn baada ya wananchi kujenga shule hzo bado sirikali haikutaka kupeleka walimu kwenye shule hzo mfano shule nliyosoma mimi ilifikia sehemu tukabakia na Headmaster kama akisafiri basi shule anamwachia headprefect. Lakn hata baada ya walimu kuajiriwa wakaterekezwa huko kijijini kwahiyo ikawa both walimu na wanafunzi wote wakawa wafungwa wa elimu. SO ELIMU YA TANZANIA INAUAWA NA SIASA ZA KINA KIKWETE. Ukumbuke alishawahi kusema hahitaji kura za waalimu baada ya kukataa kuwaongezea mishahara.