Mjadala wa kitaifa: Tuziainishe faida na hasara za uraia-pacha (dual citizenship) kwa Tanzania yetu

Mjadala wa kitaifa: Tuziainishe faida na hasara za uraia-pacha (dual citizenship) kwa Tanzania yetu

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na mijadala kuhusu Tanzania kuruhusu uraia pacha. Wapo wanaopendekeza Tanzania kama nchi ikubali uwepo wa uraia pacha ili kuzipata faida zitokanazo na uraia wa aina hiyo. Wapo wenye mtazamo kuwa muda wa Tanzania kuwa na uraia pacha bado haujafika. Hivyo basi, wanauunga mkono msimamo wa Serikali wa kutokubali na kuanzisha uraia pacha hapa nchini.

Uraia ni jambo la kisheria. Endapo Serikali itaridhia kuanzishwa kwa uraia pacha, lazima sheria inayosimamia masuala ya uraia ifanyiwe marekebisho kukidhi matakwa ya mabadiliko hayo. Ilivyo sasa, uraia unaokubalika hapa nchini ni uraia wa nchi moja: kama ni raia wa Tanzania au la. Raia wa Tanzania, ilivyo sasa, haruhusiwi kuwa raia wa nchi nyingine yeyote duniani. Ikitokea hivyo, raia husika itampasa kupoteza uraia mmojawapo: ima wa Tanzania au wa hiyo nchi nyingine.

Kwa kuwa mimi si mbobezi wa masuala ya kimataifa na kiuraia na naamini JF ni nyumba ya wabobezi wa mambo hayo na mengine, naomba kuwasilisha hoja na wito kwa waungwana kuziainisha faida na hasara za kuwa na uraia pacha hapa nchini kwetu Tanzania. Kujua faida na hasara kutachochea au kupooza wito wa wananchi wa kutaka uwepo wa uraia pacha kwa watanzania.

Karibuni waungwana wa JF...
 
Kwanza, kwa taarifa yako Wakili msomi, Tanzania kisheria ina ruhusu kwa na uraia pacha, hata mtoto wangu ni raia wa Tanzania na nchi ya ng’ambo aliko zaliwa!

Kuanzaia kuzaliwa mpaka miaka 18, unaweza kuwa na uraia wa Tanzania na nchi nyingine ila, sifa hiyo itakoma, ukifikisha miaka 18!
Pili, nafikiri kuna faida kubwa zaidi kwa nchi yetu kuwa na uraia pacha kuliko hasara. Kwa mfano, mtoto wangu amezaliwa USA, kuna masilahi binafsi mengi kwake, kuwa Mmarekani, kuliko kuchagua Utanzania!

Lakini kiuhalisia, amezaliwa Marekani ni raia, ana wazazi Watanzania, ni Mtanzania! Sheria inatakiwa ivuke mipaka imfuate mtoto wangu, na siyo kumlimiti!
 
Kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na mijadala kuhusu Tanzania kuruhusu uraia pacha. Wapo wanaopendekeza Tanzania kama nchi ikubali uwepo wa uraia pacha ili kuzipata faida zitokanazo na uraia wa aina hiyo. Wapo wenye mtazamo kuwa muda wa Tanzania kuwa na uraia pacha bado haujafika. Hivyo basi, wanauunga mkono msimamo wa Serikali wa kutokubali na kuanzisha uraia pacha hapa nchini...
Mie nionavyo,mijadala mingine kwa Tz kwa mambo kama haya, kwa wengine labda kutaka kuhusisha kila mtu, ni kizungumkuti' maana mambo kama haya, nafikiri ili kupata tija ni uwezekano tu wa kujaribu kuhusisha watu walio na uelewa na experience ya faida na hasara walizopata nchi nyingine zilizofanya hivyo, na kama faida ina'outweight hasara' basi hakuna haja ya kupoteza muda na pesa na kuhusisha kila mtu kwenye mambo haya yanahitaji uelewa mpana,ama sivyo mnaweza ishia kukwama kama mambo yale ya bunge la Katiba.... kazi iendelee.
 
Ipo imani kwamba ni rahisi kwa mtu mwenye uraia wa nchi mbili kuweza kuifanyia hujuma Tanzania. Cha ajabu ni kwamba wenye kuifanyia mambo ya ajabu wengi ni wale wenye kuvaa koti la uzalendo.

Mtu anatembea na tai yenye rangi za bendera ya taifa kumbe akiwa mbali na kamera ni mpigaji mkubwa. Waliokuwa wanakausha maji kule kwenye bwawa la mtera ili majenereta yauzwe Kariakoo na mjini katikati ni wazalendo wanaoweka mikono juu ya kifua wakati wimbo wa taifa unapoimbwa.

Uraia pacha utaisaidia zaidi Tanzania kuliko hizi dhana potofu zilizopo. Upeo wa mtu aliyezaliwa Denmark ambaye mama yake ni mwenyeji wa kule na baba mtanzania ni tofauti na yule aliyezaliwa Nzega na kukulia Mwanza mjini.

Utangamano wa Afrika ya Kusini ndio chanzo cha uchumi kuwa mkubwa na wenye kuheshimika, wasingekuwepo wazungu na wahindi kule nina uhakika wale weusi wangekuwa wachovu tu kama mataifa yanayoizunguka nchi ile.
 
Tuanzie hapa,

Uraia pacha una faida gani kwa masikini wa hali ya chini (Kwa Tanzania Masikini Ni 95%)???
 
Kwanza, kwa taarifa yako Wakili msomi, Tanzania kisheria ina ruhusu kwa na uraia pacha, hata mtoto wangu ni raia wa Tanzania na nchi ya ng’ambo aliko zaliwa!
Kuanzaia kuzaliwa mpaka miaka 18, unaweza kuwa na uraia wa Tanzania na nchi nyingine ila, sifa hiyo itakoma, ukifikisha miaka 18!
Pili, nafikiri kuna faida kubwa zaidi kwa nchi yetu kuwa na uraia pacha kuliko hasara. Kwa mfano, mtoto wangu amezaliwa USA, kuna masilahi binafsi mengi kwake, kuwa Mmarekani, kuliko kuchagua Utanzania! Lakini kiuhalisia, amezaliwa Marekani ni raia, ana wazazi Watanzania, ni Mtanzania! Sheria inatakiwa ivuke mipaka imfuate mtoto wangu, na siyo kumlimiti!
Unaona sasa, yaani pro dual citizenship hamnaga hoja.
Sasa hapa umeongea nini?
 
Kwanza, kwa taarifa yako Wakili msomi, Tanzania kisheria ina ruhusu kwa na uraia pacha, hata mtoto wangu ni raia wa Tanzania na nchi ya ng’ambo aliko zaliwa!
Kuanzaia kuzaliwa mpaka miaka 18, unaweza kuwa na uraia wa Tanzania na nchi nyingine ila, sifa hiyo itakoma, ukifikisha miaka 18!
Pili, nafikiri kuna faida kubwa zaidi kwa nchi yetu kuwa na uraia pacha kuliko hasara. Kwa mfano, mtoto wangu amezaliwa USA, kuna masilahi binafsi mengi kwake, kuwa Mmarekani, kuliko kuchagua Utanzania! Lakini kiuhalisia, amezaliwa Marekani ni raia, ana wazazi Watanzania, ni Mtanzania! Sheria inatakiwa ivuke mipaka imfuate mtoto wangu, na siyo kumlimiti!
Hatutaki uraia chotara. Kama ilivyo kwa mtu chotara anajipendekeza kwa mbari nyeupe na kujiweka mbali na watu weusi. Tabia yao wengine ni wabaguzi kuliko mtu mzungu au mwarabu. Vivyo hivyo uchotara wa uraia mtu utamkuta kujifanya mzalendo uzunguni au uarabuni. Wanaweza kutumia haki za uraia afrika kwa faida ya huo uraia wake wa kizungu au asia kwa kuzifaidisha nchi zingine na kuwafukarisha wenyeji wa nchi yake asili.
 
A matter of international law.

Mimi kama raia wa Marekani, nikiwa Tanzania kama raia wa Marekani tu bila uraia pacha, serikali ya Marekani ina uwezo mkubwa sana wa kunitetea kama raia wake ambaye nina uraia wa Marekani tu.

Nikiwa na uraia pacha, wa Tanzania na Marekani, serikali yangu ya Marekani inapata vizingiti fulani vya kisheria kunitetea nikipata matatizo Tanzania.Kwa sababu ya uraia wangu pacha wa Tanzania na Marekani.
 
Back
Top Bottom