Mjadala wa kitaifa: Tuziainishe faida na hasara za uraia-pacha (dual citizenship) kwa Tanzania yetu

Au visevesa! Kwanini usiamini kwamba watutumia hizo fursa kutunufaisha Sisi?
 
Ujamaa ni msingi wa haya maamuzi ya kukataa uraia pacha. Bado kuna zile mentalities za Nyerere kwamba adui mbaya hayupo kati yetu bali ni yule anayetokea nje.

Wizi mkubwa mkubwa kama ule wa EPA, ESCROW wahusika ni watanzania wenye kuishi humu humu nchini waliolelewa wakiambiwa mzalendo ni wa ndani na wa nje ni adui.

Tutakuja kubadilika kwani kuna ongezeko kubwa la watanzania wa diaspora na ndipo tutakapogundua ukubwa wa fursa tulizozipoteza kwa miaka mingi.
 
Hasara: Mtu mwenye Raia pacha hawezi kuwa Rais wa Nchi yoyote, hivyo unaweza kosa kiongozi mzuri kutokana na jambo hilo.
Wrong.Somalia mtu mwenye uraia pacha anaweza kuwa Rais ikiwa tu asili yake ya mwanzo ni mzaliwa wa Somalia yaani hajazaliwa nje ya Somalia.
 
Sisi tunapata "the worst of both worlds".

Yani kwenye kufuata Ujamaa hatupo kamili, tunapata mabaya ya kufuata Ujamaa, bila kupata mazuri ya kufuata Ujamaa.

Ndipo hapo unakuta mambo ya low investment, kuogopa "maadui wa nje", bila subsidized healthcare, education etc

Kwenye Ubepari nako hatupo kamili, tunapata mabaya ya Ubepari bila kupata mazuri ya ubepari.

Ndipo hapo unakuta watu wameuziana nyumba za umma, wameuziana viwanda, wamepiga hela EPA bila kuzuiwa na mazuri ya ubepari kama free press, labor unions, strong opposition, open market etc.

Tunapigwa kutoka pande zote.

Kama nchi, tutapata hasara za kutokuwa na uraia pacha kwa kukosa connections za maana na investment, bila kupata faida za kuwa na uraia mmoja tu ambazo ni za mazingaombwe zaidi.

Wewe nchi mpaka utawala wa Kikwete Ikulu ilikuwa inatumia email ya Yahoo, hapo unahitaji raia wa kigeni aingie nchini kuku compromise?

Kila siku tunasikia watu wanafanya mambo mitandaoni, bado watu wanashikilia uraia kuwa ndiyo kitu kitakachowahakikishia usalama?
 
Faida:
1. Itawawezesha watu kupata fursa za ajira, kazi na biashara ambazo zinakuwa reserved kwa raia wa nchi husika tu.

2. Itahamasisha watanzania waishio nje kuwekeza nchini wakijua wana haki sawa na raia wengine .

3. Itahamasisha wataalamu watanzania waishio nje waje kufanya kazi nchini na kuleta ujuzi na mitaji yao bila ya kuwa na hofu ya kupoteza walichojijengea huko nje.

4. Itaondoa vikwazo na kuhamasisha vijana wenye elimu na taaluma nchini kwenda kutafuta fursa nchi nyingine bila kuwa na wasiwasi wa kupoteza haki zao kama watanzania, hii itatusaidia kupunguza tatizo la ajira na kuongeza remittances.

5. itawawezesha watu kupata passport ya taifa lenye nguvu zaidi ya Tanzania hivyo kukurahisishia safari za kimataifa.

6. Itasaidia kuchangaya rangi na kupata vitoto chotara vingi (joking)

Hasara:
1. Hamna.
 
ukiruhusu uraia pacha wakenya watakuja kutuchukulia ardhi yetu yote, Watanzania Tutakuwa wapangaji.
Hivi huo uraia mutaugawa kama njugu? Jifunzeni kwa wakoloni wetu- wao wanaruhusu hata uwe na passports 195 ili mradi tu ufuate sheria yao ya kuishi kwao... hakuna bugudha... kama Tanzania tumeshindwa kutengeneza sheria yetu inayo ruhusu uraia Pacha basi tujifunze kwa majirani au wakoloni wetu wa zamani... duniani humu hakuna cha uzalendo wala nini, ni maslahi tu ndio yanazungunza- kuanzia ngazi ya familia hadi taifa ni maslahi tu... ya nini kuoneana wivu na kuyafanya maisha magumu? Tusaidianeni bila vikwazo ndio tutasonga mbele kama nchi
 
Na utanzania wa kawaida una faida gani kwa maskini wa hali ya chini? Na ni Kwa nini maskini wa hali ya chini awe ndio reference point yako ? Suala la umaskini halihusiani na uraia Pacha ndugu yangu...unmaskini sera za serikali , kuuondoa inategenea vipaumbele vya nchi - kwanza na waseme umaskini ni kitu gani? Wengine mlo mmoja ndio raha zao...wengine maharwagee ndio style yenyewe- ya nini ku reference umaskini kama kipimo cha uraia Pacha ?
 
ukiruhusu uraia pacha wakenya watakuja kutuchukulia ardhi yetu yote, Watanzania Tutakuwa wapangaji.
Huo ushahidi uko wapi? Na kwa nini iwe rahisi kihivyo? Au watunga sheria watakuwa fofofo?
 
Leo kwa mada hii, tupo pamoja! Nakupa like!
 
Pole kwa kuikosa hiyo kazi ya maana huko US.
 
What a load of trollop. Raia ni raia, iweje tena kuwe na mipaka? Inapofika vita vya Nduli Iddi Amin, mathalani, tukitakuwa kuchangia damu, si anaweza kusema kuwa mue sina ardhi? Kama huko atokako ana ardhi, atawapenda zaidi? Sikubta Olympic atachezea njinipu? Kwa nini inapojiri asiibe ndege zetu na makanikia yetu kama kina tundulissu na fatmakarume kuwatetea mabeberu KKY (kama kwaida yao)? Tumefunga Serengeti kupitia Bologonja au Mlina Kilimsnharo kutojea Tsavo, kama yeye ni raia kwa nini asipite na watalii wake? Imagine if a man and his wife have dual marriages, I mean, married in each dual country, itakuwaje?
 
Pole kwa kuikosa hiyo kazi ya maana huko US.
Mimi nilikuwa na kazi yangu nzuri tu nafanya, hao recruiters wakawa wananitaka, kwa hiyo niliendelea tu na kazi yangu.

Ila ningefanya pale hata miaka miwili tu baada ya hapo ningekuwa hot cake sana, ukiwa katika industry huku na uzoefu wa kufanya kazi Benki Kuu unakuwa hot cake.

Hilo jambo ni moja ya mambo yaliyonifanya niachane na kusubiri habari za uraia pacha niendelee na maisha yangu kivyangu na kuchukua uraia huku niliko.

Maana unaweza kujifanya mzalendo halafu opportunities zinakupita, na huo uzalendo wako haukusaidii wewe wala nchi yako.

Kuna kazi nyingine nyeti unahitaji kuwa na "security clearance" kuzifanya. Na kuna level fulani ya "security clearance" huwezi kuzipata ukiwa si raia.

Nikasema kitovu changu kipo tu Bandari ya Salama, Misheni Kota kwetu, Mwanza kwetu, hata kama nachukua makaratasi ya ughaibuni.
 
Pumba juu ya pumba
 
Aliyeelewa huu upuuzi anisaidie 🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…