Mjawazito kugharamia tiba: Je kauli ya mkuu wa mkoa wa Dar ndio msimamo rasmi wa serikali? Serikali itoe kauli.

Mjawazito kugharamia tiba: Je kauli ya mkuu wa mkoa wa Dar ndio msimamo rasmi wa serikali? Serikali itoe kauli.

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Watanzania wamesikia kauli ya mkoa wa Dar, Albert Chalamila kuwa, mjawazito atawajibika kuchangia matibabu na akishindwa aende akajifungulie nyumbani. Japokuwa imetolewa kwa kebehi lakini ni kauli iliyobeba uzito mkubwa ikizingatiwa sera rasmi ya serikali katika sekta ya afya ni mjawazito kupatiwa huduma zote za msingi za uzazi bure ikiwemo kujifungua.

Sasa ili kuepusha migongano baina ya wanachi na watoa huduma, mamlaka zingine za kiserikali (za juu au kisekta) ni vyema zikaja hadharani kufafanua matamshi hayo kama ndio msimamo rasmi wa serikali kwa sasa kiujumla au kukanusha kauli ya Chalamila.
 
Lakini wakati ufike tuseme ukweli! Ngono na kungoneka ufanye wewe alafu kuzaa tugharimie wengine! Astaghafullulah! Wakati mimba imekaa miezi 9 hukujua utakuja kujifungua? Acha masikhara nyie waswahili!
 
Back
Top Bottom