Mjeledi ulioogopa kumgusa Yesu Kristo

Mjeledi ulioogopa kumgusa Yesu Kristo

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MJELEDI WA ASKARI WA KIRUMI ULIOKATAA KUMCHAPA YESU KRISTO

Wasomaji wangu nimekuelezeni mara nyingi kuwa katika utoto wangu nikipenda sana kuangalia senema, senema za maana zinazoeleimisha.

Katika moja ya senema zinazoishi ndani ya ubongo wangu hadi sasa nimekuwa mzee ni ''Ben Hur the Story of Jesus Christ.''

Hiki ni kitabu aliandika Lew Wallace askari wa Union katika jeshi la Marekani wakati wa American Civil War (1861 - 1865).

Juu ya jina hilo Yesu Kristo utakutananae mara mbili tu katika kitabu na katika hii movie, mwanzo wake na mwisho.

Kisa kizima kinahusu dhulma aliyofanyiwa kijana wa Kiyahudi Ben Hur kutoka mji wa Judea aliyekamatwa na kufanywa mtumwa akapelekwa kutumika katika manowari za kivita za Warumi kama mpiga kasia.

Nikisema nihadithie kisa kizima tutakesha hapa.
Waigizaji walikuwa Charlton Heston na Stephen Boyd.

Chalton Heston akiwa Ben Hur na Stephen Boyd Messala.

Yesu utamuona akimpa maji Ben Hur wakati akisafirishwa kwenda katika msafara wa safari ndefu na watumwa wengine kwenda Bahari ya Mediterranean akatumike kwenye manowari.

Yesu akiwa bado kijana mdogo labda wa miaka 25 msafara unapita nje ya nyumba yao na kwa kumuonea huruma Ben Hur anampa maji akiwa kaanguka chini hajiwezi kwa uchovu na kiu.

Askari wa Kirumi anamwendea kutaka kumtia adabu Yesu Kristo.

Yesu ananyanyuka alipukuwa kainama kumpa maji Ben Hur na anamkabili askari wa Kirumi aliyevaa mavazi ya vita uso kwa macho bila hofu.

Askari hakuweza kunyanyua mjeledi wake kumpiga Yesu Kristo.

Mijeledi ina historia ndefu.

 
Shukrani babu ntaitafuta
Aelknes,
Mimi ni umri wa baba yako.

Ikiwa unapenda kuniita kwa heshima ya umri wangu niite baba na wewe unakuwa mwanangu.

Ukiwa mwanangu utanipa staha ya mtoto kwa baba.

Nikikuachia uniite babu ni kuwa nakufungulia mlango wa kunitania na kuniambia lolote.

Hizi ndizo mila zetu na muhimu kuzingatia ili tusitoke kwenye murua wetu.

Wajukuu wangu mkubwa ana miaka 5.
Sasa wanao ndiyo wanaweza kuniita mimi babu.
 
MJELEDI WA ASKARI WA KIRUMI ULIOKATAA KUMCHAPA YESU KRISTO

Wasomaji wangu nimekuelezeni mara nyingi kuwa katika utoto wangu nikipenda sana kuangalia senema, senema za maana zinazoeleimisha.

Katika moja ya senema zinazoishi ndani ya ubongo wangu hadi sasa nimekuwa mzee ni ''Ben Hur the Story of Jesus Christ.''

Hiki ni kitabu aliandika Lew Wallace askari wa Union katika jeshi la Marekani wakati wa American Civil War (1861 - 1865).

Juu ya jina hilo Yesu Kristo utakutananae mara mbili tu katika kitabu na katika hii movie, mwanzo wake na mwisho.

Kisa kizima kinahusu dhulma aliyofanyiwa kijana wa Kiyahudi Ben Hur kutoka mji wa Judea aliyekamatwa na kufanywa mtumwa akapelekwa kutumika katika manowari za kivita za Warumi kama mpiga kasia.

Nikisema nihadithie kisa kizima tutakesha hapa.
Waigizaji walikuwa Charlton Heston na Stephen Boyd.

Chalton Heston akiwa Ben Hur na Stephen Boyd Messala.

Yesu utamuona akimpa maji Ben Hur wakati akisafirishwa kwenda katika msafara wa safari ndefu na watumwa wengine kwenda Bahari ya Mediterranean akatumike kwenye manowari.

Yesu akiwa bado kijana mdogo labda wa miaka 25 msafara unapita nje ya nyumba yao na kwa kumuonea huruma Ben Hur anampa maji akiwa kaanguka chini hajiwezi kwa uchovu na kiu.

Askari wa Kirumi anamwendea kutaka kumtia adabu Yesu Kristo.

Yesu ananyanyuka alipukuwa kainama kumpa maji Ben Hur na anamkabili askari wa Kirumi aliyevaa mavazi ya vita uso kwa macho bila hofu.

Askari hakuweza kunyanyua mjeledi wake kumpiga Yesu Kristo.

Mijeledi ina historia ndefu.

Mzee wetu, movie ya ben hur, ipo ile ya version ya 2016, hiyo ndio nzuri, the best kabisa inayo represents tamaduni za mashariki vizuri..... Pamoja na roma, ni nzuri ile movie jamani acha tu..... Moja sentence ninazokumbuka.... Baada ya juda kupona kwenye collapse ya meli kule baharini.... Alielea hadi ufukweni akaokotwa na merchants ya kiafrica ufukweni akiwa hajitambui.... Mzee akamchukua akampa mission ya kuikomboa nchi yake kutoka kwa roman.. Kupitia games za kifo... Juda anakuwa mbishi kutokana mateso aliyopata 5 years kule kwenye ship. Kwahiyo aliona yeye kapitia magumu sana kuliko watu wote pale judae.

Juda Akamjibu mzee... Umekuwa motivational speaker siku hizi, unadhani kila mtu waweza mdanganya ili akafie uwanjani.... Mzee akacheka... Akajibu your 5 years in Port of tyrus, now you think that you know everything from suffering, your situation is not unique juda, my son also died in the that mission. Judae akatulia tuli, akamsikiliza mzee akachuma hekima zake, mzee akampa mbinu... Baadae juda alikuja kufanikiwa kuikomboa nchi yake toka kwenye mikono mizito ya chuma ya roma, watu walimpenda balaaa...... Nilijifunza sana.

Sent from my 5023F using JamiiForums mobile app
 
Mzee wetu, movie ya ben hur, ipo ile ya version ya 2016, hiyo ndio nzuri, the best kabisa inayo represents tamaduni za mashariki vizuri..... Pamoja na roma, ni nzuri ile movie jamani acha tu..... Moja sentence ninazokumbuka.... Baada ya juda kupona kwenye collapse ya meli kule baharini.... Alielea hadi ufukweni akaokotwa na merchants ya kiafrica ufukweni akiwa hajitambui.... Mzee akamchukua akampa mission ya kuikomboa nchi yake kutoka kwa roman.. Kupitia games za kifo... Juda anakuwa mbishi kutokana mateso aliyopata 5 years kule kwenye ship. Kwahiyo aliona yeye kapitia magumu sana kuliko watu wote pale judae.

Juda Akamjibu mzee... Umekuwa motivational speaker siku hizi, unadhani kila mtu waweza mdanganya ili akafie uwanjani.... Mzee akacheka... Akajibu your 5 years in Port of tyrus, now you think that you know everything from suffering, your situation is not unique juda, my son also died in the that mission. Judae akatulia tuli, akamsikiliza mzee akachuma hekima zake, mzee akampa mbinu... Baadae juda alikuja kufanikiwa kuikomboa nchi yake toka kwenye mikono mizito ya chuma ya roma, watu walimpenda balaaa...... Nilijifunza sana.

Sent from my 5023F using JamiiForums mobile app
Maziwa...
Nitaiangalia na hii In Shaa Allah.
 
Back
Top Bottom