Mjengwa:Nimepumzika Kuandikia Rai Mwema

Mjengwa:Nimepumzika Kuandikia Rai Mwema

magoma

New Member
Joined
Mar 2, 2009
Posts
4
Reaction score
0
Hii nimeisoma mjengwablog;

Nimepumzika Kuandikia Raia Mwema
Kwa wasomaji wa makala zangu,

Baadhi yenu mmeshangaa kutonisoma kwenye ' Raia Mwema' toleo la jana. Nawajulisha kuwa nimepumzika kuliandikia gazeti la Raia Mwema ili niweze kuwaongoza wenzangu tulioshiriki kuandaa gazeti la Gozi Spoti ( Halipo tena mitaani) kujipanga upya kwa kutumia uzoefu tulioupata.

Tayari nimeshamjulisha Mhariri wangu ( Raia Mwema) kaka John Bwire juu ya uamuzi wangu huu. Natumia fursa hii kuwashukuru kwa dhati ndugu zangu wa 'Raia Mwema' kwa kunipa fursa ya kuandikia gazeti hilo. Nimekuwa nikiandika bila kukosa tangu toleo la kwanza. 'Raia Mwema', kama ilivyokuwa kwa gazeti la 'Rai', limenisaidia kuifikia jamii pana ya Watanzania. Nimetengeneza mahusiano mema na Watanzania wengi wa ndani na nje ya nchi. Katika muda wangu na ' Raia Mwema', nimejaribu kwa uwezo wangu wote kuitumikia jamii yetu kupitia kalamu yangu. Nami nimejifunza mengi kupitia wasomaji wa gazeti hilo.

Naam. Nimepumzika. Kwa sasa nitabaki kuwa msomaji wa ' Raia Mwema'.
/Maggid
 
Uamuzi huo wa Mjengwa si bure, kuna jambo!. Naamini it has something to do with safari ya kuelekea 2010. Kwa mawazo yangu, haiwezekani Mzee wa Makala tangu enzi na enzi akizungumzia mambo ya siasa, uchumi na jamii ghafla akabwaga manyanga eti kisa anataka kuimarisha kijarida cha 'Gozi Spot' ambacho kiko limited kwenye michezo.

Naamini ama anajipanga kuibukia gazeti jingine, ama dhamira yake itamsuta.

Mimi ni mmoja kati ya wanunua magazeti kwa ajili ya makala mbalimbali, kwa sisi wasomaji wa makala zake, kutuacha just like that, 'its a betrayor'
 
Hata "Gozi Spoti" alitangaza kwa blogu yake kuwa wameliondoa kutoka orodha ya msajili tarehe 19/02. Hivyo nadhani kama wana jipanga kuanzisha Gazeti kamili litakaloripoti masuala yote (Siasa, biashara nk) na si michezo peke yake.
 
tumpongezee kwa kujipanga upya kwani huo ndo mwanzo wa kupanuka zaidi kwa kufungua milango mingi...

maggid natumai bado una nia ya dhati ya kuendelea kuburudisha, kuelimisha na kusasahisha jamii yetu inayojaribu kujenga uwezo wa kupambanua zaidi mambo kwa mustakabali wa taifa hili...

HONGERAAA...
 
Hongera mjengwa kujiondoa kwa mazuri ni changamoto kwako na kwa wengine pia
 
Hii ina harufu ya 2010 au makundi ya CCM yanajaribu kuingia Raia Mwema. Kumbuka Afisa Mahusiano wa Richmond (Salva Rweyemamu) alikuwa Rai na Mjengwa. Rai ilipouzwa kwa Rostam, Salva akaenda Ikulu kwa kufanikisha uuzaji wa Rai, na ndipo Mjengwa akahama na Jenerali kwenda Raia Mwema. Hivi sasa JK na kundi lake wanatafuta namna ya kuyapunguza nguvu magazeti "hostile". Linalokataa kununuliwa, ananunuliwa mwandishi. Sisemi Mjengwa amenunuliwa, lakini Tanzania yetu, kila mtu ana bei, na pungufu unaongea mwenyewe!

Kwa nini hakuwaaga wasomaji wake ndani ya makala ya mwisho anakuja kuaga kupitia blogu?
 
Hii ina harufu ya 2010 au makundi ya CCM yanajaribu kuingia Raia Mwema. Kumbuka Afisa Mahusiano wa Richmond (Salva Rweyemamu) alikuwa Rai na Mjengwa. Rai ilipouzwa kwa Rostam, Salva akaenda Ikulu kwa kufanikisha uuzaji wa Rai, na ndipo Mjengwa akahama na Jenerali kwenda Raia Mwema. Hivi sasa JK na kundi lake wanatafuta namna ya kuyapunguza nguvu magazeti "hostile". Linalokataa kununuliwa, ananunuliwa mwandishi. Sisemi Mjengwa amenunuliwa, lakini Tanzania yetu, kila mtu ana bei, na pungufu unaongea mwenyewe!

Kwa nini hakuwaaga wasomaji wake ndani ya makala ya mwisho anakuja kuaga kupitia blogu?

Maggid.
Yaelekea anayosema huyu ndugu yangu baija bolobi ni kweli. Unaweza kuja hapa kujitetea? Vinginevyo tutaendelea kuamini haya huyu bawana aliyosema maana yanaonekeana yako karibu na ukweli.
 
- Raia Mwema Hakati Tamaa
- Raia Mwema Husema Ukweli
- Raia Mwema Hasaliti watu
- Raia Mwema Hapokei Rushwa
- Raia Mwema Haachi Mbachao
 
Au ndio kama yale ya Deodatus Balile kuacha Tanzania Daima? Walau yeye aliaga kwa makala kwenye gazeti alilokuwa anaandikia.
Mmmmhhhh!
 
...mmmm, nina wasiwasi na aliyeileta post hii! Post ya kwanza tu habari ya Mjengwa?? Ama ndio wewe mwenyewe????
 
If i remember correct kuna wakati fulani hata mzee Mwanakijiji alishawahi kutangaza kuwa anapumzika kuandika katika gazatte fulani lakini sikumbuki haswa lilikuwa ni gazeti gani fikira zangu zinaniambia ni huyo huyo raia Mwema je na yeye anajiandaa for 2010?
 
If i remember correct kuna wakati fulani hata mzee Mwanakijiji alishawahi kutangaza kuwa anapumzika kuandika katika gazatte fulani lakini sikumbuki haswa lilikuwa ni gazeti gani fikira zangu zinaniambia ni huyo huyo raia Mwema je na yeye anajiandaa for 2010?

Yeye hakusubiri 2010, alianza baada ya kutangaza na anafanya vizuri kabla hata ya kuchaguliwa.
 
Mjengwa,
Umetuangusha wapiganaji wenzako.Nilishaona dalili wapi unaelekea baada ya makala kama iliyokuwa ikimsifia JK kuwa anakatiza mitaani Bagamoyo kwa miguu,kuwa JK mtu wa watu.
Kama Balile,baadaye tutajua wapi ulipo hata ukitumia jina bandia.Au kasheshe za ngurumo zimekutoa mbio?
 
Back
Top Bottom