Mji Mwema ndani ya Kiwira Coal Mines

Mji Mwema ndani ya Kiwira Coal Mines

Papa Mopao

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2009
Posts
4,153
Reaction score
2,647
Huu mji ulikuwa maarufu sana miaka ya zamani pale Kiwira Coal Mines, zamani hapo palikuwa na ukumbi japokuwa haikuwa ya kisasa, ulijengwa kwa kutumia makuti, disco zilikuwa zinapigwa sana mle ndani watu kama kawa walizicheza sana mpaka vumbi mwili mzima.

Mji Mwema kulikuwa na makazi ya watu wa kila aina, ujirani ulikuwa na ladha ya aina yake, nyumba nyingi asilimia kubwa zilikuwa za makuti miaka hiyo kabla ya kujengwa nyumba za kisasa Block E na Block D kama sikosei, kulikuwa na Makazi ya Wachina kule juu mlimani tulikuwa tunapaita Msasani, sijajua chimbuko la Msasani ni nini pale kwa Wachina.

Kulikuwa na uwanja wa Mpira, Netball vyote vilikuwa jirani na Mji Mwema.

Hakika huu mji ulijenga utamaduni fulani wa Ujirani mwema kwa maeneo yote ya Kiwira Coal Mines miaka ya mwishoni mwa 80 hadi miaka ya 90 mwanzoni kabla ya kubomolewa na kujengwa nyumba za kisasa.

Kwa wakaazi wa Kiwira Coal Mines watakumbuka kwa huu mji
 
Kilichobaki sasa pale Kiwira Coal Mines(Stamico) ni muonekano tu kwamba paliwahi kuwa mji mkali. Kamji ka maana enzo hizo. Majengo yemedhoofu na STAMICO wanashindwa kukarabati na kurudisha hali yake ya zamani.
 
Kilichobaki sasa pale Kiwira Coal Mines(Stamico) ni muonekano tu kwamba paliwahi kuwa mji mkali. Kamji ka maana enzo hizo. Majengo yemedhoofu na STAMICO wanashindwa kukarabati na kurudisha hali yake ya zamani.
Kwa kweli, kile kiwanda muhimu sana kwa uzakishaji wa umeme
 
Ni eneo ambalo siwezi kulisahau
Palinoga sana miaka hiyo, kulikuwa na maisha ya aina ya Ujamaa fulani hivi, nakumbuka Tancut band walifika pale kutumbuiza, kulikuwa na Ligi daraja la nne pale timu nyingi zilishiriki pale, vikundi vya sanaa vilitumbuiza ule ukumbi unaopakana na dispensary yaani ilikuwa burudani kwa ujumla
 
Palinoga sana miaka hiyo, kulikuwa na maisha ya aina ya Ujamaa fulani hivi, nakumbuka Tancut band walifika pale kutumbuiza, kulikuwa na Ligi daraja la nne pale timu nyingi zilishiriki pale, vikundi vya sanaa vilitumbuiza ule ukumbi unaopakana na dispensary yaani ilikuwa burudani kwa ujumla
Umetaja TANCUT umenikumbusha na KIMULIMULI JAZZ BAND ya Mafinga
 
Back
Top Bottom