Mji wa Damascus/Mji wa Dameski: Kongwe la vita tangu enzi za kabla, wakati na baada ya Yesu

Mji wa Damascus/Mji wa Dameski: Kongwe la vita tangu enzi za kabla, wakati na baada ya Yesu

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Dameski, mji mkuu wa Syria, ni mojawapo ya miji mikongwe zaidi duniani iliyokaliwa kwa mfululizo. Historia yake inajumuisha matukio mengi ya vita na migogoro, yakiangaziwa katika vyanzo vya kihistoria na Biblia.

Katika Biblia, Dameski inatajwa mara kadhaa.

Mfano maarufu ni ule wa kuongoka kwa Sauli, aliyekuwa akiwatesa Wakristo, kuwa Paulo mtume baada ya tukio la kimiujiza njiani kuelekea Dameski, kama ilivyoelezwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume. Hii inaonesha umuhimu wa mji huu katika historia ya Ukristo.

Mji huu pamoja na kwamba haujawahi kuacha kukaliwa na watu kwa zaidi ya miaka 2000 sasa, unabeba historia ya migogoro tangu enzi hizo.

Kihistoria, Dameski imekuwa kitovu cha biashara na utamaduni katika Mashariki ya Kati, ikivutia na kuhimili uvamizi na uongozi wa tawala mbalimbali, kutoka kwa Waarabu, Waturuki wa Ottoman na hatimaye wakoloni kama Wafaransa.

Mji huu umeshuhudia mapinduzi, vita vya wenyewe kwa wenyewe na migogoro mingi, ikiwemo ile ya mwanzo na hii ya karne ya 21 ambayo imesababisha uharibifu mkubwa na kuathiri vibaya maisha ya raia.

Migogoro ya Dameski imekuwa na athari kubwa, sio tu kwa Syria bali kwa eneo lote la Mashariki ya Kati, ikichangia katika masuala ya kisiasa, kijamii na kibinadamu ambayo yanaendelea kuathiri eneo hilo na ulimwengu kwa jumla.

N'yadikwa.

3495526168_29438e5362_z.jpg


PICHA: Mtaa katika mji mkongwe wa Dameski/Damascus nchini Syria
 
Dameski kwa uhakika ilikuwa ikikaliwa na watu miaka 5,000 iliyopita, miaka 3,000 BCE.

Na pia uchimbaji umeonesha ilikaliwa na watu kati ya miaka 8,000 mpaka 10,000 BCE, yaani, miaka 10,000 mpaka 12,000 iliyopita.

Yani inawezekana kuwa wakati wa Yesu miaka 2,000 iliyopita, Dameski tayari ilikuwa ishakaliwa kwa miaka 10,000.

 
Dameski kwa uhakika ilikuwa ikikaliwa na watu miaka 5,000 iliyopita, miaka 3,000 BCE.

Na pia uchimbaji umeonesha ilikaliwa na watu kati ya miaka 8,000 mpaka 10,000 BCE, yaani, miaka 10,000 mpaka 12,000 iliyopita.

Yani inawezekana kuwa wakati wa Yesu miaka 2,000 iliyopita, Dameski tayari ilikuwa ishakaliwa kwa miaka 10,000.

Ni mji mkongwe haswa. Nachelea kuhisi kwamba hata migogoro isiyoisha huenda imo kwenye vinasaba vya watu wake, ndiyo sababu haijawahi kutulia.
 
Bible inasema Damscus ipo mito miwili inaitwa Abana na Farpari ambayo ni bora kuliko mito yote ya Israel. Hii mito ni kweli hadi leo ipo Damascus.

2Wafalme 5:12

Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko maji yote ya Israeli? Je, Siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? Akageuka, akaondoka kwa hasira.
 
Miji yote duniani ni mikongwe,wenzetu walituzid na kuweka ktk kuweka ktk vitabu,sisi wakoloni walikuja na kuchoma vya kwetu na kubakisha historia chache kwa maeneo yetu kama Kilwa.
 
Bible inasema Damscus ipo mito miwili inaitwa Abana na Farpari ambayo ni bora kuliko mito yote ya Israel. Hii mito ni kweli hadi leo ipo Damascus.

2Wafalme 5:12

Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko maji yote ya Israeli? Je, Siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? Akageuka, akaondoka kwa hasira.
Bado ipo japo imebadilishwa majina Barada na Awaj. Huo Abana siku hizi unaitwa Barada, na huo Farpari siku hizi unaitwa Farpari.

Huo Barada unatiririkia mji wa Dameski kutokea upande wa Lebanoni na ndio unategemewa kunywesha mji wa Dameski na ni chanzo cha maji ya umwagiliaji kwenye Oasisi ya Ghouta.

Huo mwingine nao pia unatokea kwenye safu za milima inayopakana na Lebanon na ni mdogo kuliko huo Barada wenyewe unatiririkia Kusini Mashariki mwa Dameski. Wanautegemea kwa kilimo pia. So mito yote bado ipo kama inavyotajwa humo kwenye Wafalme 5.
Chanzo: Wikipedia.
 
Back
Top Bottom