Mjue Boxer bora aliyekuwa anapigana kilevi, The drunken Master

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Emanuel Augustus/Emanuel Burton A.K.A Drunken Master amezaliwa January 2, 1975 Brownsville Marekani. Alianza mapambano kama professional boxer miaka ya 1990 hadi mwaka 2011. Huyu mtu hakupata umaarufu mkubwa kwa kuwa watu wengi walikuwa hawaipendi style yake ya kujifanya kalewa wakati anapigana.

Kwenye mchezo wa boxing wengi huwa wanakomaa na foot work, yeye kama mlevi alikuwa hajali sana foot work, hali hii ilimfanya kumnyima ushindi wa mapambano mengi ambayo amewahi kupambana.

Nasema huyu jamaa alikuwa mpambanaji mzuri waamuzi walikuwa hawampendi kutokana na namna ya uchezaji wake, huku wengi wakimuambia wazi kuwa abadilishe namna ya kucheza ili aweze kushinda Zaidi.

Amenyimwa ushindi mara nyingi ndio inaleta rekodi kuwa mapambano 78 aliyopigana aliweza kushinda mapambano 38 pekee, huku mapambano 20 akishinda kwa Knock Out. Sasa utashangaa inakuwaje mtu ashinde kwa KO mapambano mengi kiasi hicho ikiwa alikuwa mpambanaji wa hovyo, kilichotokea ni kwamba alikuwa anaonekana kama sio professional boxer.

Hali hiyo inaonyesha wazi kuwa mtu kama ni best loser hauwezi kuwa na kiwango hiko cha KOs ila kwa kuwa wengi walikuwa hawapendi namna alikuwa nafanya fighting akiwa kwenye boxing ring.

Your browser is not able to display this video.
 
Dah...mb 44? ila poa tu acha nimcheki nione km alikuwa na jipya!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…