Mjue Kissendi Nyanda Ntalima Mpandagoya Mkushi, Muongoza harakati za Waafrika kujitambulisha wao na asili yao

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Jina Kissendi Nyanda Ntalima Mpandagoya au Mkushi sio jina maarufu kama walivyo wanasiasa, wanamichezo na wasanii.

Kissendi Nyanda Ntalima Mpandagoya a.k.a Mkushi, yeye ndio muasisi wa makundi zogozi yanayojulikana kwa jina la Waafrika Tujitambue, ambapo amekuwa akifundisha mambo mbalimbali juu ya historia ya mtu mweusi, namna alivyokuwa kinara wa Mapinduzi ya ustaarabu na teknolojia duniani.

Lakini kutokana na husda na fitna za husda za NYAHUNI au mtu mweupe, akautweza utu wa mtu mweusi na kumsahaulisha kabisa asili yake kwa kutumia dini za Ukristo na Uislam.

NYAHUNI waliwakata mikono watu wote waliotokea kwenye koo za wahunzi.

Hizi harakati zina nia njema sana, lakini sidhani kama zitawafurahisha mabeberu
 
Hivi we mzee umeandika kitu gani? Au ni mimi ndio nazeeka vibaya? Mabeberu kwani bado wapo?
 
Neno ustaarabu lina mzizi wa kwenda kiarabu.

Linatueleza kwamba Waarabu ndio walioleta "civilization" Afrika.

Hivyo, katika habari inayotaka kunasibisha Uafrika na "civilization", kutumia neno "ustaarabu" kwa sisi tunaoangalia mizizi ya maneno ni kusema kinyume, ni kuonesha Waafrika hawana "civilization" bila kupitia uarabu.

Kimsingi maana ya asili ya ustaarabu ni uarabu.

Sasa ukimsifia muafrika na civiliztion yake, kwa kusema alikuwa kinara wa mapinduzi ya uarabu, hapo hujamsifia, umemkejeli.
 
Eti ni kweli wewe ni shemasi?
 
Yaani unafosi msib wa jamaako uwe wa kitaifa .
 
Achacheni na uzushi na upotoshi wa mapanafricanist.
Wapi wahunzi walikatwa mikono,mwafrika hajawahi kuwa na ustaarabu kabla ya ujio wa dini
 
Mkuu , kwani neno linaloeleza ''civilization au Ustaraabu' kwa lugha zetu ni lipi? Lugha yoyote tu tunayoijua
 
Mkuu , kwani neno linaloeleza ''civilization au Ustaraabu' kwa lugha zetu ni lipi? Lugha yoyote tu tunayoijua
Mkuu mimi lugha ya Kiafrika ninayoimudu ni Kiswahili, na Kiswahili ndiyo kishatuvuruga hivyo.
 
Mkuu mimi lugha ya Kiafrika ninayoimudu ni Kiswahili, na Kiswahili ndiyo kishatuvuruga hivyo.
Mkuu tulipokubali Kiswahili kiwe 'lingua franca' katika Taifa letu tulikubali mengi ikiwemo ku-borrow maneno.
Kiswahili kina maneno ya kiingereza, Kijerumani na sehemu kubwa sana Kiarabu .

Na kwavile hakuna neno lolote katika lugha yetu linaloeleza '' ustaarabu au Civilization'' tukubali kutumia neno hilo kwa maana ya mawasiliano na si kubeba uarabu au kiingereza.

Hata majirani zetu wa EAC ambako Kiswahili kimeenea na kuonekana kuwaunganisha zaidi mfano DRC bado watatumia neno 'ustraabu' kwasababu ndio neno lililopo, vinginevyo watatumia kifaransa.

Hakutakuwepo na tofauti ya kiingereza, kifaransa na kiarabu. Huo ndio msingi wa kukuuliza neno mbadala
 
Sawa.

Mimi ninekuwa naangalia sana logical fallacies hapa na sitaki kufanya logical fallacy ya argument from dictionary. Kwa hiyo nakuelewa.

Lakini pia, lugha inakua. Na tunaweza ku coin neno lingine linalowakilisha civilization ambalo si ustaarabu.

Kwa sababu, we can't get away from the fact that the etymology of ustaarabu equates civilization with being Arabic.

Kukataa kubadilika kwa sababu tu huko nyuma tulifanya mambo kwa njia fulani ni logical fallacy nyingine. Ni argument from tradition.
 
You are forever alive
 
Tumia ustaafrika au kuelevuka. Umenikumbusha bwana uvuvwevwevwe onyetenyevwe ugwemubwem ossas toka Nigeria na Andrianampoinimerinatompokoindrindra toka Madagascar.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…