Mjumbe Bunge la Katiba avuliwa uanachama Alliance for Tanzania Farmers Party (AFP) Zanzibar

Mjumbe Bunge la Katiba avuliwa uanachama Alliance for Tanzania Farmers Party (AFP) Zanzibar

sawa

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
2,752
Reaction score
929
Zanzibar. Mjumbe wa Bunge la Katiba kupitia Chama cha Allience for Tanzania Farmers Party (AFP), Rashid Yussuf Mchenga amevuliwa uanachama kwa madai ya kughushi saini ya Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Shaibu Masoud Salum. Uamuzi huo ulitangazwa juzi na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Said Soud Said.

Said alisema saini hiyo aliyotumia kumhalalisha katika ombi la barua yake iliyokwenda Ikulu ya Zanzibar, haikusainiwa na Naibu Katibu Mkuu wa AFP Zanzibar na tayari wamefungua kesi Kituo cha Polisi cha Madema.

Alisema majina yaliyotumwa Ikulu kwa uteuzi ni ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Rashid Mohamed Rai aliyeteuliwa kuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mahadhi Mohamed Mahadhi, (Soud) na mkewe Farida Juma Khamis.

Naye Mchenga alisema chimbuko la kuibuliwa mgogoro huo ni mwenyekiti na mkewe kukosa kwenye uteuzi huo na kwamba, hawezi kughushi saini ya mtu.

"Ni wivu wa mwenyekiti wetu. Amechukia kutoteuliwa yeye na mkewe. Hajui riziki ni mafungu saba, Bunge hili limemtoa udenda na sasa anatapatapa tu mimi ni mjumbe halali," alisema.

source: Mwananchi gazeti
 
kwa staili hii kweli tutapata katiba tunayo itarajia wanajamvi?
 
Hii katiba kweli inajeuzwa chaka la wahuni!!! Na ina maana kuwa hakukuwa na vetting ya hawa wateuliwa?? Au waliteuliwa tu ili kujaza kura za ndiyo kutimiza serikali mbili za SSM?
 
huu ni upuuzi mtupu hakuna hojA ya msingi hapo wallikuwa wapi wakati jamaa anafanya hayo yote? hawa viongozi hawa tamaa tu Hakuna kitu ..... wavuane wavalishane TUNACHOHITAJI NI KATIBA INAYOELEWEKA NA SI VINGINEVYO....
 
Ikulu ni mzigo, usalama ndio kabisaa mzigo kazi kutesa watu

Vetting ya wajumbe 201 inashindikana? Hadi mnachukua mke na mme?

Only in Tanzania
 
yale yale ya MAKAIDI mwenyekiti wa NLD anasema wanachama wenzake wa chama cha NLD wanawivu kisa ameteuliwa yeyena mkewe kukiwakilisha chama cha NLD na wiki ya kwanza ndio hiyo inakatika
 
Ameshaonja posho, kiyoyozi cha ukumbi wa bunge na viti vya kuzunguka, ukichanganya na wale kuku hapo chako ni chako hawezi kurudi Zanzibar akale urojo.

Zanzibar. Mjumbe wa Bunge la Katiba kupitia Chama cha Allience for Tanzania Farmers Party (AFP), Rashid Yussuf Mchenga amevuliwa uanachama kwa madai ya kughushi saini ya Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Shaibu Masoud Salum. Uamuzi huo ulitangazwa juzi na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Said Soud Said.

Said alisema saini hiyo aliyotumia kumhalalisha katika ombi la barua yake iliyokwenda Ikulu ya Zanzibar, haikusainiwa na Naibu Katibu Mkuu wa AFP Zanzibar na tayari wamefungua kesi Kituo cha Polisi cha Madema.

Alisema majina yaliyotumwa Ikulu kwa uteuzi ni ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Rashid Mohamed Rai aliyeteuliwa kuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mahadhi Mohamed Mahadhi, (Soud) na mkewe Farida Juma Khamis.

Naye Mchenga alisema chimbuko la kuibuliwa mgogoro huo ni mwenyekiti na mkewe kukosa kwenye uteuzi huo na kwamba, hawezi kughushi saini ya mtu.

"Ni wivu wa mwenyekiti wetu. Amechukia kutoteuliwa yeye na mkewe. Hajui riziki ni mafungu saba, Bunge hili limemtoa udenda na sasa anatapatapa tu mimi ni mjumbe halali," alisema.
source mwananchi gazeti
 
ukistajaabu hilo utaona la Musa,kuna wajumbe wawili wana jina moja wanatoka sehemu mbili tofauti wameteuliwa kwenye bunge la katiba,na wote wamepewa posho ya kujikimu 1040000/= sasa imekuja kugundulika kuwa wamekosea mtu mmoja alipewa taarifa kimakosa
 
ahahah msalani bwana,yeye anasema wanamuonea wivu,wenzake kisa wao wamekosa fursa,laki 3 kwa siku si haba yakhee
 
Maajabu! Kumbe ndiyo maana posho ni ajenda ya kwanza na muhimu!
 
Maajabu nikuwa ikulu imejibu kuwa hili halimuondolei ujumbe wake kwenye bunge la katiba
 
sijawasikia kabisa wale wajumbe wa kundi la watu wenye malengo yanayofanana,maana huu ndio ulikuwa mda wao wakuto msimamo wa pamoja,si ndio maana ya malengo yanayofanana
 
wajumbe wa kundi la malengo yanayofanana
paul makonda
julius mtatiro
abdalla majura Bulembo
kajungi MTC
Na wengine mnao wakumbuka ongezeeni hao wajumbe
 
Zanzibar. Mjumbe wa Bunge la Katiba kupitia Chama cha Allience for Tanzania Farmers Party (AFP), Rashid Yussuf Mchenga amevuliwa uanachama kwa madai ya kughushi saini ya Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Shaibu Masoud Salum. Uamuzi huo ulitangazwa juzi na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Said Soud Said.

Said alisema saini hiyo aliyotumia kumhalalisha katika ombi la barua yake iliyokwenda Ikulu ya Zanzibar, haikusainiwa na Naibu Katibu Mkuu wa AFP Zanzibar na tayari wamefungua kesi Kituo cha Polisi cha Madema.

Alisema majina yaliyotumwa Ikulu kwa uteuzi ni ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Rashid Mohamed Rai aliyeteuliwa kuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mahadhi Mohamed Mahadhi, (Soud) na mkewe Farida Juma Khamis.

Naye Mchenga alisema chimbuko la kuibuliwa mgogoro huo ni mwenyekiti na mkewe kukosa kwenye uteuzi huo na kwamba, hawezi kughushi saini ya mtu.

“Ni wivu wa mwenyekiti wetu. Amechukia kutoteuliwa yeye na mkewe. Hajui riziki ni mafungu saba, Bunge hili limemtoa udenda na sasa anatapatapa tu mimi ni mjumbe halali,” alisema.

source: Mwananchi gazeti

Duh kazi ipo na hawa wachumia tumbo wajanja wajanja....
 
ndio mambo na maajabu ya nchi yetu
 
Baadhi ya Wanzazibar wanawivu sana hadi wana bore
 
Uzoefu wetu wa muda mrefu umetuonyesha pasipo shaka kwamba mambo mengi yanayotendeka Tanzania hayawezi kutendeka katika nchi nyingine.

Tanzania imekuwa taifa la ajabu na masikitiko yetu ni kwamba mporomoko wa maadili katika jamii yetu umeziba mitima na dhamira za viongozi wetu na jamii nzima kwa jumla kiasi cha kuyaona matendo hayo kama mambo ya kawaida.

Tunayo mifano ya matukio lukuki ya ajabu na ya kushtusha yaliyowahi kutokea hapa nchini lakini yakaonekana kama ya kawaida.

Fikiria wafanyabiashara walioiba mabilioni ya fedha za Epa ambao muda mfupi kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2005 walikwenda Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakati wa siku za mapumziko na kukwapua mabilioni hayo kwa njia za udanganyifu. Fikiria wezi hao walivyoahidiwa kwamba iwapo wangezirudisha wasingechukuliwa hatua yoyote.

Ebu fikiria nchi ambayo kiongozi wake anakwenda ughaibuni na kutangaza kuwapo kwa majangili mapapa 40 na kusema kiongozi wao yuko mikoa ya Kaskazini, badala ya kusema hayo akiwa nchini, ikiwa ni pamoja na kuyakamata majangili hayo na kuyachukulia hatua.

Ebu fikiria matukio haya mawili ambapo Waziri Mkuu anatamka bungeni kwamba ni sawa tu kwa Jeshi la Polisi kuwapiga wananchi ‘wakorofi', huku mkuu wa nchi akikiagiza chama chake cha siasa ambacho yeye ni mwenyekiti kuwapiga wapinzani anaodai wanafanya vurugu dhidi ya wafuasi wa chama chake. Ni nchi gani ambayo viongozi wake wakuu wanaweza kutoa amri hizo za hatari?

Tumesema yote hayo kutokana na kitendo cha ajabu na aibu kilichofanywa na Mwenyekiti wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Dk Emannuel Makaidi cha kufanya ulaghai na kujiwezesha yeye na mkewe kuteuliwa kuingia katika Bunge la Katiba.

Katika utetezi wake, ametoa hoja za kuchefua na kughadhabisha kuwa, kwa vile mke wake naye ni mwanachama wa chama hicho alikuwa na haki ya kuteuliwa kama ilivyo kwa Rais Kikwete na mke wake ambao wote ni wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM.

Tunasema uteuzi huo haukubaliki hata kidogo kutokana na kukiuka taratibu zilizowekwa kisheria kwamba vyama vya siasa lazima viwe na sura ya Muungano katika mfumo na uendeshaji wake.

Ni ujasiri na uthubutu wa kiwango cha juu kujiteua yeye na mkewe kama vile NLD ni mali ya kifamilia. Kudai kwamba aliteua majina ya wanachama wanne na Rais akamchagua yeye na mkewe ni uongo wa kupitiliza.

Hii inaonyesha kwamba zilikuwapo mbinu chafu katika mchakato wa uteuzi huo, vinginevyo wanachama wa Zanzibar wangenyimwa vipi uwakilishi? Hatua ya chama hicho upande wa Zanzibar ya kumtaka Rais Kikwete atengue uteuzi wa Dk Makaidi na mkewe lazima iungwe mkono.

Tatizo hapa ni hatua ya Serikali kuendelea kuvibeba kwa sababu za kisiasa vyama vya siasa vilivyokufa siku nyingi. Ukweli ni kwamba NLD na vyama vingine vingi ambavyo kwa mujibu wa sheria ya vyama ya 1992 vinapaswa kufutiwa usajili wa kudumu bado vinatambuliwa kiasi cha viongozi wake kuingizwa katika Bunge Maalumu la Katiba bila kuwa na sifa stahiki.



MAMBO YA MAKAIDI HAYO
 
Back
Top Bottom