Hii ni moja ya kauli za Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) wa Mkoa wa Mbeya, Ndugu Ndele Jailos Mwaselela, alipotekeleza ahadi yake ya kuchangia ukarabati wa ofisi 32 za chama hicho katika Wilaya ya Mbeya Vijijini leo, Februari 15, 2025.
Katika hatua hiyo, M-NEC Mwaselela ametoa jumla ya Shilingi milioni 30, ambapo leo amekabidhi Shilingi 700,000 kwa kila kata ya chama hicho.
Makabidhiano ya fedha hizo yamefanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Mbalizi High School, mbele ya viongozi wa CCM kutoka kata zote 32 za wilaya hiyo.
Katika hotuba yake, Mwaselela amewasihi viongozi kuepuka malumbano yasiyo na tija, akisema kuwa migogoro yao haiwasaidii wananchi.
Hii ni moja ya kauli za Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) wa Mkoa wa Mbeya, Ndugu Ndele Jailos Mwaselela, alipotekeleza ahadi yake ya kuchangia ukarabati wa ofisi 32 za chama hicho katika Wilaya ya Mbeya Vijijini leo, Februari 15, 2025.
Katika hatua hiyo, M-NEC Mwaselela ametoa jumla ya Shilingi milioni 30, ambapo leo amekabidhi Shilingi 700,000 kwa kila kata ya chama hicho.
Makabidhiano ya fedha hizo yamefanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Mbalizi High School, mbele ya viongozi wa CCM kutoka kata zote 32 za wilaya hiyo.
Katika hotuba yake, Mwaselela amewasihi viongozi kuepuka malumbano yasiyo na tija, akisema kuwa migogoro yao haiwasaidii wananchi.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa (NEC) wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Ndele Jailos Mwaselela ametekeleza ahadi ya kuchangia zaidi ya Shilingi milioni 30 ili ziweze kutumika kwa ajili ya ukarabati wa ofisi 32 za kata za chama hicho wilaya ya Mbeya Vijijini.
Akizugumza wakati wa kukabidhi fedha hizo MNEC Ndele amesema kutoa mchago huo ni takwa la mwanachama wa Chama cha Mapiduzi, “Kwa kuzingatia maombi ya kata zote zilizowasilisha maombi yao kupitia ofisi ya wilaya na mkoa, mchango huu unaeda kuleta chachu na hamasa kuwa katika mkoa wetu wa kila kata iwe na ofisi ya chama ambayo sisi wote wanachama tumeijenga kwa umoja wetu” Alisema Ndele.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mbeya Vijijini Akimu Mwalupindi baada ya kupokea fedha hizo amemshukuru MNEC Ndele na kuwataka viogozi wa kata kwenda kuzifanyia kazi inayotakiwa, “Ndugu MNEC niseme mbele yako na kutoa maelekezo kwa kata zote 32 naomba fedha hiyo ikafanye kazi iliyokusudiwa na sisi tumeshapewa maelekezo ya kutoka kuja kukagua ile kazi iliyofanyika baada ya fedha ile mliyoipata leo hii hapa” Alisema Mwalupindi.