Mjumbe wa Baraza la Maulamaa na Imamu wa Msikiti wa Manyema, amewageukia wanaokataa kura ya wazi.

Mjumbe wa Baraza la Maulamaa na Imamu wa Msikiti wa Manyema, amewageukia wanaokataa kura ya wazi.

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2013
Posts
5,536
Reaction score
2,266
Shekhe Hamid Jongo ambaye ni Mjumbe wa Baraza la Maulamaa na Imamu wa Msikiti wa Manyema, Kariakoo Dar es Salaam, amewageukia wanaokataa kura ya wazi akisema ni wanafiki na waoga, huku akiwatupia vijembe wasomi, akiwaambia, “hamuoni kwa macho, hata kupapasa!” aliwashangaa wanaotaka kura ya siri wakati walipodai posho waliweka mambo hadharani.

“Tulitoa hoja zetu kuhusu posho kwa uwazi bila kunong’ona, wananchi wakatuzomea, magazeti yakaandika, sasa kura tunataka kwenda kimyakimya. Na mimi naunga mkono mpaka kieleweke. “Hapana, tupige kura ya waziwazi tufahamike, hakuna hoja ya mantiki ya kujificha. Kama posho hatukunong’ona, tunaogopa nini?” alihoji Shekhe Jongo.

Akichangia hoja hiyo, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM) amesema kama wazee wa zamani walimwogopa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere katika kudai Serikali ya Tanganyika, ‘basi imekula kwao.’

“Hili la Tanganyika hatulitaki. Kuna watu wanadai hapa kuwa wao tu ndio jasiri, wakati ni waoga tu. Majasiri wako wengi, mimi ni jasiri na watu wanajua. Hata Mandela alikuwa jasiri sana. “Kama mlishindwa kuipata Tanganyika yenu wakati huo, imekula kwenu.Kama mlimwogopa Mwalimu hadi akafa ndio mnadai Tanganyika, imekula kwenu. Tuko Mwalimu mwingine,” alisema Lusinde akishangiliwa na wajumbe wenzake. “Watu wanateseka kwa foleni pale kumsubiri Mzee Pinda na viongozi wengine wapite, leo mnataka kuwa na viongozi sita. Acheni uroho wa madaraka.”

Lusinde aliyekuwa akizungumza huku akitoa mifano mbalimbali yenye kufurahisha, alionekana dhahiri kumjibu Mjumbe mwenzake, Christopher Mtikila aliyedai ndiye jasiri pekee nchini na anayejulikana kuwa ni muumini wa Tanganyika.

Kwa upande wake, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano, Job Ndugai alionya matumizi mabaya ya lugha hasa kuhusu masuala ya Muungano.

“Tumevumilia sana, mahali penyewe pa kuongea ndio hapa. Lakini tuwe makini, vinginevyo tutagawana mbao hapa. Tumekuja wamoja, tuondoke wamoja. Tukianza lugha za ajabu ajabu hapa, hatutafika,” alisema Ndugai. Kauli ya Ndugai ilitokana na Mjumbe Said Ali Mbarouk aliyesema kuwa utungaji wa Kanuni ni lazima uanze kwa kuipa Zanzibar maamuzi yake, kwani kwa miaka 50, kumekuwa na uonevu na dhuluma kubwa.
Chanzo: Habari leo.
 
Kama wajumbe wameenda kwenye bunge la Katiba kusimamia maslahi ya wananchi waliowatuma, kitu gani kinawafanya watake kujificha kwenye maamuzi ya mwanvuli wa kura ya siri katika kupitisha, kukataa au kubadilisha vipengele vya Rasimu ya Katiba?.

Wananchi wanataka kufahamu kile wajumbe wao wamekikubali na kukikataa bungeni ili iwe ni historia iliyoandikwa kwa kila mjumbe na siyo kwa mwanvuli wa wajumbe wote wa bunge la Katiba.

Kujificha kwenye kura za siri katika maamuzi haya muhimu ya kitaifa ni kujenga taifa la waoga na wanafiki kitu ambacho ni hatari sana katika mstakabali wa Taifa endelevu.

Wananchi wanataka kuweka historia wazi kwa kila mjumbe kwa kizazi hiki na cha baadaye.

Kama kuna watu wameingia kwenye Bunge la Katiba bila kuelewa umuhimu wao katika mstakabali wa taifa na mpaka sasa bado wameendelea kuwepo, basi hawataweza kusamehewa kwa makosa makubwa kama haya kwa taifa.

Kila mjumbe lazima aubebe msalaba wake wa kuingia kwenye bunge la Katiba na siyo kujificha kwenye mwanvuli wa corrective responsibility.

Moja ya nguzo kuu ya CCM iliyochangia kwa chama kudumu mpaka sasa katika ahadi zake ni pamoja na kusema kweli daima na fitina ni mwiko.
 
CCM wanataka kura za wazi ili kuwabaini na kuwashughulikia wale wanaoenda kinyume na matakwa ya Chama ndio maana wajumbe wanaogopa kung'olewa kucha. Hivyo basi, ni vema Kura ikawa ya siri, period!
 
Kama wajumbe wameenda kwenye bunge la Katiba kusimamia maslahi ya wananchi waliowatuma, kitu gani kinawafanya watake kujificha kwenye maamuzi ya mwanvuli wa kura ya siri katika kupitisha, kukataa au kubadilisha vipengele vya Rasimu ya Katiba?.

Wananchi wanataka kufahamu kile wajumbe wao wamekikubali na kukikataa bungeni ili iwe ni historia iliyoandikwa kwa kila mjumbe na siyo kwa mwanvuli wa wajumbe wote wa bunge la Katiba.

Kujificha kwenye kura za siri katika maamuzi haya muhimu ya kitaifa ni kujenga taifa la waoga na wanafiki kitu ambacho ni hatari sana katika mstakabali wa Taifa endelevu.

Wananchi wanataka kuweka historia wazi kwa kila mjumbe kwa kizazi hiki na cha baadaye.

Kama kuna watu wameingia kwenye Bunge la Katiba bila kuelewa umuhimu wao katika mstakabali wa taifa na mpaka sasa bado wameendelea kuwepo, basi hawataweza kusamehewa kwa makosa makubwa kama haya kwa taifa.

Kila mjumbe lazima aubebe msalaba wake wa kuingia kwenye bunge la Katiba na siyo kujificha kwenye mwanvuli wa corrective responsibility.

Moja ya nguzo kuu ya CCM iliyochangia kwa chama kudumu mpaka sasa katika ahadi zake ni pamoja na kusema kweli daima na fitina ni mwiko.
Kura iwe ya siri. Wajumbe wanaogopa kung'olewa kucha na meno bila ganzi. Wanajua kilichompata Dr Mvungi ambaye alikuwa champion wa serikali tatu!
 
mbona inazuiwa sana kuidai TANGANYIKA wakati ZANZBAR inaogopwa na wala haikemewi inapojitwalia madaraka kamili. Hapo huwa sielewi kama watanganyika tumerogwa au?
 
Hii thread imeletwa na mpiga picha wa kinana hana kazi ningine zaidi ya kuwalamba miguu maboss zake
 
Ccm wanataka kura ya wazi ili kuwabaini watakao kwenda kinyume na matakwa yao ili washughulikiwe! Na ikumbukwe kuwa wajumbe wengi wa ccm ni waoga na wanafiki wasioweza kusimamia misimamo yako!
 
Kura ya kificho ni uhuni kwani tunaficha nini mangapi tumefanya wazi watanzania wanataka kuona mchakato wote hakuna kificho hapo.
 
Kura iwe ya siri. Wajumbe wanaogopa kung'olewa kucha na meno bila ganzi. Wanajua kilichompata Dr Mvungi ambaye alikuwa champion wa serikali tatu!
Tunataka kura ya wazi ili watanzania waone tumefanya nini kwa niaba yao siri ndiyo nini.
 
Jamani wana JF na hili lituhangaishe? Siri na sio Siri? Yaani nini faida ya kuwa ya Siri na nini faida ya kuwa ya wazi? Nini hasara ya Siri na wazi?

Siri kwenye kura mengine wazi? Lakini mshahara wa Pinda uwe wazi na kura Siri? Posho mlizokuwa mnadai zilikuwa hoja za wazi wazi kura Siri?

Kuna usemi usemao" two things that a man can not hide is when is in love and drunk" kwa hiyo ukiwa na mapenzi na chochote huwezi kujifisha hata ufanyaje!

Sioni mantiki ya kuwa na Siri!
 
mbona inazuiwa sana kuidai TANGANYIKA wakati ZANZBAR inaogopwa na wala haikemewi inapojitwalia madaraka kamili. Hapo huwa sielewi kama watanganyika tumerogwa au?

Mkuu,

Serikali ya Zanzibar imemezwa ndani ya serikali ya muungano!Idadi ya watu wa Zanzibar ni sawa kabisa na idadi ya watu wa wilaya ya Temeke.

Kwa hiyo hata ukiwaacha wazanzibar wote waje Tanganyika kuishi hawatakuwa na effect yoyote ile!

Kwa ufupi Zanzibar HAINA MADHARA yoyote kwenye muungano,hata wakipewa uhuru kamili wanaoutaka!
 
CCM wanataka kura za wazi ili kuwabaini na kuwashughulikia wale wanaoenda kinyume na matakwa ya Chama ndio maana wajumbe wanaogopa kung'olewa kucha. Hivyo basi, ni vema Kura ikawa ya siri, period!

Kwa hiyo kuna watu waoga sana kusimamia wanachokiamini kiasi kwamba tuwaendekeze; kama hawawezi kusimama na kuchukua huo uamuzi wao wajiondoe kwenye hilo Bunge lao... kwani lazima wawepo?
 
Jamani wana JF na hili lituhangaishe? Siri na sio Siri? Yaani nini faida ya kuwa ya Siri na nini faida ya kuwa ya wazi? Nini hasara ya Siri na wazi?

Siri kwenye kura mengine wazi? Lakini mshahara wa Pinda uwe wazi na kura Siri? Posho mlizokuwa mnadai zilikuwa hoja za wazi wazi kura Siri?

Kuna usemi usemao" two things that a man can not hide is when is in love and drunk" kwa hiyo ukiwa na mapenzi na chochote huwezi kujifisha hata ufanyaje!

Sioni mantiki ya kuwa na Siri!

huna point,pumba tupu!!!!
 
Mi nadhani hili suala sasa lifikie mwisho. We should move on...
 
Mkuu,

Serikali ya Zanzibar imemezwa ndani ya serikali ya muungano!Idadi ya watu wa Zanzibar ni sawa kabisa na idadi ya watu wa wilaya ya Temeke.

Kwa hiyo hata ukiwaacha wazanzibar wote waje Tanganyika kuishi hawatakuwa na effect yoyote ile!

Kwa ufupi Zanzibar HAINA MADHARA yoyote kwenye muungano,hata wakipewa uhuru kamili wanaoutaka!

pumba tupu! ndo maana tunasema miccm mingi ipoipo tu hata kwenye hilo bunge la katiba,imekalilishwa maneno na kina nape ,haijajiandaa kwa mjadala na majadiliano yatapoanza itaumbuka sana!!!!
 
Hivi ww mwanadiwani kwa nn unajitoa ufahamu? Hiyo kauli ya Ndugai imemhusuje huyo mbaruk aliyetaka mamlaka ya Zanzibar na isimuhusu Lusinde aliyetaka Tanganyika isiwepo?
Kwani hoja ya lusinde ina mashiko gani kwa kizazi hiki? Habari za Nyerere aliyoyafanya isiwe kisingizio cha kudumisha yasiyopendeza. Mbona AZIMIO LA ARUSHA WALILIZIKA ZANZIBAR HALISEMWI HILO VIJIJI VYA UJAMAA PIA HAVIPO HATA MUUNGANO UTAJADILIWA KAMA UNA KASORO UTAUNDWA UPYA KABISA.
 
Back
Top Bottom