Mkanda wa ngono ulivyotutesa!

BatteryLow

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2011
Posts
446
Reaction score
149
Wakati nasoma nilienda likizo kwa kaka yangu, na pale akawa yupo mdogo wa shemeji, yaani mke wa bro.
Siku moja mwisho wa wiki waliondoka kwenda matembezi tukabaki nyumbani na mdogo wake shemeji, basi kumbe yeye alikuwa na mkanda wa picha za ngono lkn pale ndani hakuna aliyekuwa anajua.
Bro na shemeji walipoondoka akaleta ule mkanda na tukaanza kuangalia, baada ya muda umeme ukakatika tuss. cassette ikabaki ndani ya deki na maana yake ni kwamba kama hakuna umeme haitoki.
Tulichanganyikiwa kwani walikuwa na tabia wakirudi wanakaa sebuleni na hivyo umeme ukirudi tu, TV inaunganisha mchezo.
Tukapiga mahesabu ile deki tuichomoe tukaifiche chumbani, tukasema hapana, au tuchomoe waya kule kwenye umeme, pia tukaona haisaidii kwani wakigundua wataurudishia.
Wakati bado tunazidi kukosa amani, ghafla tukasikia geti linagongwa, nikamwambia mdogo wake shemeji, 'naenda kufungua geti lkn ww usiondoke hapo karibu na tv ili umeme ukija uchomoe deki fasta'. Ile sijafika mlangoni umeme huooooo.... Jamaa akaichomoa na mm nikenda kufungua geti.
 
Daah unanikumbusha DVD ya Anco,,,nilifunga sebule nikaondoka na funguo ni shidaa hiyo makitu ukifumwa unakodoaa!!!
 
Kwa kweli nmecheka duh nmekumbuka mbali sana
 
Mm ilishanikutaga iyo zamani sana kipind icho ndo nimemaliza 4m 4 nasubir matokeo nikaendaga kwa kaka yangu alafu ni ameokoka,,,,cku yupo church mm kama kawaida nikatupia mzgo wa xx kwa dec,,ndan ya dkk kama 10 umeme ukakata,,nikasubir mpaka dkk 30nzima haujarud,alafu ndo mida yake ya kurudi,,, ila nilisolve na bisibisi nilifunguaga dec faster nikaitoa cd...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…