KERO Mkandarasi akamilishe Barabara ya Njelela kupitia Miva kwenda Njombe, imejaa vifusi, gari hazipiti vizuri

KERO Mkandarasi akamilishe Barabara ya Njelela kupitia Miva kwenda Njombe, imejaa vifusi, gari hazipiti vizuri

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
Sisi watumiaji wa barabara ya kutoka Njelela kupitia Miva na Uwemba Wilayani Ludewa Mkoani Njombe tunasikitika kutelekezwa kwa vifusi vilivyomwagwa kwenye barabara hiyo.

Tunaelewa lengo zuri za Serikali kuweka vifusi hivyo lakini ni mwezi sasa tangu vifusi hivyo vimwagwe jambo linalosababisha barabara hiyo kupitika kwa taabu.
IMG-20241204-WA0011.jpg
Jana Desemba 4, 2024, tukiwa tunatoka Njombe kwenda Kijiji cha Njelela kupitia Miva ilibidi abiria tushuke kwenye gari na kuanza kusambaza vifusi, hivyo ili tuweze kuendelea na safari. Hii ni kwasababu magari yanakwama kwa kuwa njia ni ndogo sababu ya vifusi hivyo.

Msimu huu wa mvua barabara za huku kwetu zinatutesa sana sasa na hivi vifusi vilivyotelekezwa hapa ndo vinazidisha mateso. Tunaomba serikali izingatie umuhimu wa matumizi ya barabara hii na kukamilisha matengenezo hayo kwa haraka.
IMG-20241204-WA0014.jpg
IMG-20241204-WA0018.jpg
IMG-20241204-WA0013.jpg
IMG-20241204-WA0019.jpg
 

Attachments

  • IMG-20241204-WA0021.jpg
    IMG-20241204-WA0021.jpg
    63 KB · Views: 4
Nakufahamu huko nilikua naenda Mundindi.!

Poleni sana, naanimi wahusika wamesikia na watakuja kuwajibika
 
Back
Top Bottom