Nakupa TANO Mkuu........................Akili mu Kichwa. 1: Kuwa mtulivu. 2: Mfuatilie Huyo Bibie ujue anaishi wapi 3a: Mfuate siku nyingine ili akupe ABC. 3b: Anza kufuatilia nyendo za mkeo 4:iwapo Bibie atakufafanulia ukweli wa tuhuma zake, zifanyie kazi kwa utulivu mkubwa bila kusukumwa na hisia. 5: Fanya maamuzi ya Busara (iwapo ni kweli kwanini ametoka nje? Je chanzo ni wewe au ni tamaa tu) 6: Kama ni tamaa tu, Kaka PIGA CHINI FASTA
Khaaaaaaaaaaaa!
Big shem ni wewe au kuna mtu kaiba pasiwedi!!!
Epushia mbali Sisy asipite mitaa hii maana naimajin huyo mwanamke akubali na kutaka kuambatana nawe kwao mkaongee kiutu uzima!!!
Uko kwenye mizunguko yako maeneo mbali na nyumbani kwako, mara ghafla anakutokea mwanamke usiyemjua kabisa na anakwambia kwa sauti kiasi cha kuwavuta wapita njia wengine waliokuwa wakipita na shughuli zao kusimama na kusikiliza kinachoendelea.
Mwanamke huyo anakwambia , Wee baba we, nakuomba sana umkanye mkeo kutembea na bwana angu, la sivyo nitamfanya kitu ambaccho hatakuja kukisahau maishani mwake ..Mwambie asisahau kama mie ni mzaliwa wa Tanga. Kama humtoshelezi, si akatafute wanaume mwengine huko, kuliko kutembea na mabwana za watu, mpaka anataka kunihatarishia uchumba angu, mwambie akome tena akome kama alivyokoma kunyonya titi la mama yake .. mwanamke huyo anaondoka huku akiendelea kubwabwanya na njia kwa maneno yenye kukera.
Hebu niambie kama ni wewe unachukua hatua gani ..?
Hhahaha hahahha,hhahahaha sasa ole wako Canta Umwambie.......sitakuletea tena zile raba
nitaipotezea,si unajua vichaa wengi mjini?
Ingekuwa ni mimi wala nisingeficha...............Kwani hujui kwamba mficha uke huwa hazai?Ila Babu kama ni wewe kuwa tu mkweli tukupe ushauri wa kupita kwenye supu ya pweza jioni, haingii akilini bibi atange na njia kiivo, hapo hata huyo mwanamama naye utampitia ili umonyeshe kuwa we ni rijali hahahahahaaaaa.........
Hii hainihusu mimi jamani......................! Nawasilisha tu.
namwambia nipe contacts zako ili wakiwa pamoja tufanye ufumanizi,akishanipa contacts naanza kumtongoza yeye