Mkapa akwepa maswali ya wasomi adai naye ni mwanafunzi

Ochu

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2008
Posts
976
Reaction score
47
Na Burhani Yakub Lushoto

 
Kwa nini migomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu haikutokea wakati wa utawala wa Mkapa?
 
Migomo ya wanafunzi ilitokea hata wakati wa utawala wa Mkapa. Muhimbili waligoma chuo chao kikafungwa mwaka 2002. Mlimani pia waligoma 2001 na 2004 chuo kikafungwa kwa muda wa wiki mbili(2004) hadi ikafikia hatua mh. Ng'wandu kumtaja jamaa mmoja aitwaye Bahati Tweve wa Mlimani kuwa ni kinara wa Migomo. Tofauti iliyopo kati ya awamu ya tatu na nne ni kiwango cha migomo. Migomo haikuwa mingi awamu ya tatu na nitakupa sababu

Moja: Waziri anayyeshughulikia Elimu ndiye huyo huyo anashughulikia elimu ya juu. Huyo huyo ahangaikie migomo ya walimu na wanafunzi wa chuo kikuu. Inamshinda. Kwa kifupi Waziri mwenye dhamana hii ameshachemsha ila anaogopa kusema

Mbili: Wanafunzi wa vyuo vikuu sasa hivi wana mwamko sisemi hata wale waliopitia awamu ya tatu hawana mwamko, la hasha. Isipokuwa wao sasa hivi wameunda umoja wao wa TAHLISO kwa hiyo ni rahisi kuratibu migomo yao na pia kuwa na sauti moja.

Tatu: Sera ya bodi ya mikopo nchini haiwezi kumuingi mtu akilini eti mtoto wa mkulima wa pamba (na hata pamba yenyewe haina soko), wa Kolandoto Mwanza amlipie mwanawe asilimia 40 ya mkopo wa chuo kikuu pesa ambayo hata yeye akidunduliza hawezi kufikia kiwango hicho na hata akienda benki hapati na hakubaliwi kwa sababu atakuwa hajafikia vigezo vyao. Wakati wa awamu ya tatu hiki chombo cha kuratibu mikopo kilikuwa hakijaanza rasmi na ni kutokana na uongozi mbovu wa watu fulani wa DARUSO wa miaka hiyo ndiyo waliyowaingiza chumvini. Muulizeni Zitto Kabwe ni shahidi.

Nne: Hali ngumu ya maisha, ufisadi, ulanguzi na mambo mengine kama hayo yanawafanya watu wajiulize maswali mengi hasa wasomi kwa nini wafanyiwe mambo kama haya na watu ambao wamesomeshwa bure na serikali. Baada ya kulewa mvinyo wa madaraka wanawasahau watoto wa makabwela kwa kuwa wao wanawasomesha wa kwao nje ya nchi. Kwa kubuni sera za kuikandamiza nchi yetu na kutudumaza na hii Vicious Cycle of Poverty kiaina na kinamna. Huku akaunti zao zina mabilioni ambazo zinaweza kuwasomesha wanafunzi wa chuo kikuu kwa miongo mitano na zaidi pesa ambazo ni mali ya serikali zikihifadhiwa kwenye akaunti za vigogo hao nje ya nchi.

Tano: Sera ya Elimu ya juu haijampa uhuru mwanafunzi kutoa maoni yake juu ya kuboresha kwa kuwa hao waheshimiwa hujitengea bajeti zao pamoja na perdiems na kwenda Bagamoyo picknick na viburudisho vyao wakidai wanafanya strategic plan , pamoja na risk assessment ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu nchini. Matokeo yake ndiyo hayo. Wawakilishi wa wanafunzi wanakuwa bribed na nafasi mbalimbali za ajira serikalini pamoja na shahada za uzamili ushahidi upo.

Kwa hiyo mkuu pamoja na yote katika yote wengi wetu tunatambua hali ngumu ya uchumi iliyokuwa ikitukabili miaka ya 1984 enzi za utawala wa Nyerere na chama kimoja . Kitu ambacho sitamsahau Nyerere ni kwenye upande wa elimu yeye hakulifanyia mzaha kwa sababu alijua ndio msingi na ufunguo wa maisha na ndio maana hakuna mtu aliyedaiwa mkopo . Na wewe waulize hao ambao wanajifanya kusema wanafunzi wanastahili kulipa mikopo kama wao walidaiwa senti tano na Taifa hili wameshalichangia nini na mabadiliko gani ambayo wameyafanya kama sio ufisadi na kuvimba matumbo tu. Wewe unaweza kwenda chooni ukajisaidia halafu hujaflash watu wakaja juu unajifanya unaona kinyaa wakati kinyesi ni cha kwako?

Hii nchi bwana we iache tu.
 
Heshima Mbele,

Mkapa kwenye suala la kupangua Hoja ni kiboko na kamwe hautakuja kumsikia akijibu hoja zozote za kisiasa tena zinazohusu msuala ya Serikali ya awamu ya nne.


Hivi kitila unarudi lini Tanzania?
 
Either Tanzanians are easily impressed or the reporter botched the story.

Of course there is no reason why both should not hold.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…