Mkapa ampiku Kikwete


huyu mtu katumwa sio siri
hii comparison ni totally unfair ni njama ya kusafisha UFISADI
 
Ni nani alipiga hiyo hesabu ya uchumi wa Mkapa na ni kwa kiasi gani takwimu zake ni za kuaminika?
 
Ni kwa nini EPA, Meremeta, Tangold, n.k. hatukuzijua wakati wa mkapa??? Pamoja na matatizo ya JK, lakini uhuru wa habari umekua na umetuwezesha kujua mabaya ya Mmakonde nkapa.
na kikwete akiondoka mabaya yake mtayajua sana sijui huu utauwita uhuru wa habari
lazima mtofautishe uhuru wa habari na kukuwa kwa technolojia, watu wengi wana internet na access na habari than before kwa hiyo kwa serikali yeyote itapata shida kuvizuia vyombo vya habari

muulize kubenea/mwanahalisi uhuru wa vyombo vya habari
 
Mhhhhh mkapa alikuwa bad,kikwete ni worse.
 
Ni nani alipiga hiyo hesabu ya uchumi wa Mkapa na ni kwa kiasi gani takwimu zake ni za kuaminika?

Mkuu MMM, wapigaji wa mahesabu ni wale wale. hawajabadilika,, WB, IMF kupitia wakala wao hapa the likes of BOT na NBS, kwa hiyo labda tuwaulize kama wanamwonea gere Muungwana ndo wanamwangusha ki hivyo?

Otherwiese a double digit iflation, ina maana hata Zimbabwe wametupita..walau kwa ubunifu!
 
All in all is the nation at some point where we all dream it to be????????? Otherwise we will keep comparing for the next 100 yrs and still no changes to the life of a common man.
 
Nashindwa kuelewa kwanini, Lakini Ben mara zote aliweza kutumia sana mawazo ya Kizalendo zaidi kuzidi Jk ana pia kwake ndio maana aliweza kujenga uchumi mwenye nguvu katika Taifa letu Tanzania
 
Ni nani alipiga hiyo hesabu ya uchumi wa Mkapa na ni kwa kiasi gani takwimu zake ni za kuaminika?
BOT, UDSM, Kitengo cha uchumi, na NBS and WB, IMF and wadau wengine wa maendeleo, lakini kuja haja ya kutazama na kuvumua upya mipangilio yetu ya uchumi na takwimu zake maana inatisha shaka sana katika kujua na kutambua nini hasa kipo
 
Ni kwa nini EPA, Meremeta, Tangold, n.k. hatukuzijua wakati wa mkapa??? Pamoja na matatizo ya JK, lakini uhuru wa habari umekua na umetuwezesha kujua mabaya ya Mmakonde nkapa.


Sasa kujuwa peke yake kunasaida nini kama huwezi kuyafanyia kazi???

Kuhusu uhuru wa habari hakuna la kumsifia hapa huu umekuja kwa ajili ya udhifu wake tu wa kuongoza. Yeye mwenyewe toka aingie hata mambo yake mwenyewe yanaibuliwa. Hivi unafikiri kweli alitaka tujuwe haya ya Downs, EPA, Richmond na mikataba ya Buzwagi iliyofanyiwa hotelini tena miezi kadhaa tu baada ya yeye kupewa dhamana???

Hata kama nikitaka kukubaliana nawe kuwa alitaka tujuwe nchi yetu inavyoliwa then what??? Bora tusijuwe kama alivyosema MMJJ siku za nyuma.
 
- Mnyonge mnyongeni, tatizo la hii analysis ni kwamba ingesubiri kwanza Kikwete amalize na yeye miaka 10, ndio kwanza yupo wa nne, ingawa sio siri kwamba dalili ziko wazi tunakoelekea sio kwema!

Respect.

FMEs!

Mjomba, kwa uongozi wa JK, sidhani kama tusubiri miaka 10 ili tuweze kumpima. Anaonekana wazi ni mtupu kichwani.
 
Hakuna Shaka kuwa kila mtu anaweza kuona ubaya wa mwezake kama akitoka katika mfumo wa Taifa hili na kujenga taswira mbaya kwa mwezake
 

Tena inasemekana mkwere ndo aliyesaini mkataba wa wizi wa IPTL akiwa waziri wa nishati na madini. Ni yeye huyohuyo aliye rafiki mkubwa wa bwana Sinclair anayeetuibia madini yetu kila kukicha na uswahiba wao inasemekana umeanza tangu mkwere akiwa waziri wa nishati na madini.
 
Of course uchumi ulionekana kukua kwa sababu revenue yao kubwa ilikuwa kuuza mali za watanzania kwa juhudi ila wagawane cha juu. sasa hivi hamna cha kuuza ni Taksi tu na hizo pia watu wanaiba....
 
Mjomba, kwa uongozi wa JK, sidhani kama tusubiri miaka 10 ili tuweze kumpima. Anaonekana wazi ni mtupu kichwani.

Hapana JK ni raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,hawezi kuwa mtupu kama unavyotaka kutuaminisha. Nakubali kama binadamu anaweza kuwa na mapungufu yake lakini sidhani kama tumefika huko kumuona kama mtupu kichwani! Mtu mtupu kichwani ni kichaa na katiba ya nchi hii inazuia mtu mtupu kichwani kugombea wadhifa wowote.

Naamini siku moja tutamkubali JK let's wait and see.Pengine uchaguzi wa 2005 na mambo yaliyomzunguka katika ngwe ya kwanza yalimnyima kumeremeta.
 
Bado naona kuwa Mkapa alifanya vizuri sana katika uchumi, tofauti sana na Kikwete

Mi hapo ndo nashangaa uzuri upi huo ambao wengi wetu hatuuoni? Au ndiyo hizo Meremeta, Tangold, Ndege yake, Radar, EPA, MV Bukoba, Tanesco, etc?
Je, nani alifaidika?
 
Mi hapo ndo nashangaa uzuri upi huo ambao wengi wetu hatuuoni? Au ndiyo hizo Meremeta, Tangold, Ndege yake, Radar, EPA, MV Bukoba, Tanesco, etc?
Je, nani alifaidika?
Mkuu wala huna haja ya kuuliza mengi, kumbuka kuwa
MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO, inatoa majibu mengi sana.
 
Ni kweli kabisa naunga hoja mkono kuwa Mkapa kampiku mjomba JK, lakini atlest hatuwezi sema hajafanya lolote. Kwa mfano wale mafisadi waliokuwa wanapigiwam kelele enzi zile za mkapa, yeye alikua anadai leteni ushahidi ndio awashughulikie. Kitu ambacho kilikua kinwavunja moyo wananchi na inawezekana ndio walikua wanaiba wote
 
Hapana shaka kuwa Mkapa alipata washauri wazuri katika masuala ya uchumi na japo kuwa yeye siyo economist kama ilivyo kwa mzee mzima wa kaya
 
Mkapa aliuza mali zetu na kipato kikapanda.Sasa hakuna ch akuuza lakini jitihada zinaonekana.Kama katika maendeleo ya jamii elimu na kilimo vimepewa kipaumbele zaidi kuliko wakati wa Mkapa.

Na hatuwezi kumpima mtu katika muda wa miaka mitano ya kwanza lakini tunaweza kufanya hivyo baada ya miaka kumi.

Mkapa amejiwekea rekodi ya ufisadi,wizi na mauaji ya raia kuliko kiongozi yeyote tangu tupate uhuru wetu.
 
Mkuu wala huna haja ya kuuliza mengi, kumbuka kuwa
MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO, inatoa majibu mengi sana.
Kaka yangu Mkandara, Sikatai kuwa Mkapa alifanya makosa mengi sana, na pia kama akishatakiwa basi wafanye hivyo, ila ukweli unabaki pale pale kuwa aliimarisha sana uchumi kuliko ilivyo hivi sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…