Duniahadaa
JF-Expert Member
- Oct 16, 2017
- 336
- 677
Kuna jamaa yangu yamemfika. Habari kamili ni kuwa waliandikiana mkataba na kandarasi ili a supply material katika site iliyopo Rukwa. Huyo bosi mndarasi alikuwa Mbeya (anakoishi). Hivyo wali draft mkataba na kutumiana kwa email na kila mtu akaridhia vipengere. Mkandarasi ali saini huko Mbeya kisha aka- scan na akautuma kwa email, jamaa (supplier) aka u- print Rukwa na kisha kumpelekea mwanasheria (wakili) naye aka saini na kugonga muhuri kuwa ameshuhudia. Ukweli ni kuwa hapo ofisini alikuwa yeye tu na yule supplier.
Jamaa aka -suply material ( mawe, mchanga, kokoto). Kilichotokea ni kwamba mkandarasi aligoma kumlipa pesa ya yale material kwa kigezo kwamba hayakuwa na kiwango (ingawa yamejengewa). Supplier kaenda mahakamani na ule mkataba, yule mkandarasi kaamua kumruka kwamba hapakuwa na mkataba wowote kati yao na anasema anataka kuona mkataba original na wakili aliyeshuhudia kama anamfahamu.
Swali (1) Je, huo mkataba ni halali kisheria? (2) Je, mahakama itapokea huo mkataba kama kilelezo? (3) Je, wakili aliyedai kushuhudia wakati upande mmoja haukuwakilishwa, alikosea? (4) kama alikosea na ikathibitika, adhabu yake ni ipi?
WANASHERIA TUSAIDIENI.
Jamaa aka -suply material ( mawe, mchanga, kokoto). Kilichotokea ni kwamba mkandarasi aligoma kumlipa pesa ya yale material kwa kigezo kwamba hayakuwa na kiwango (ingawa yamejengewa). Supplier kaenda mahakamani na ule mkataba, yule mkandarasi kaamua kumruka kwamba hapakuwa na mkataba wowote kati yao na anasema anataka kuona mkataba original na wakili aliyeshuhudia kama anamfahamu.
Swali (1) Je, huo mkataba ni halali kisheria? (2) Je, mahakama itapokea huo mkataba kama kilelezo? (3) Je, wakili aliyedai kushuhudia wakati upande mmoja haukuwakilishwa, alikosea? (4) kama alikosea na ikathibitika, adhabu yake ni ipi?
WANASHERIA TUSAIDIENI.