Mkataba wa DP World ni biashara za wachache CCM, ushahidi huu hapa

Mkataba wa DP World ni biashara za wachache CCM, ushahidi huu hapa

Stuka

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
282
Reaction score
906
Mpaka sasa ukiusoma mchezo unagundua suala la DP World ni la Chongolo na baadhi ya watu wake na sio dili la CCM kwa ujumla wake, mfano mdogo ni ziara ya Kinana tangu ameanza mikutano Rufiji, akaenda Kondoa na sasa yuko Manyara sijamsikia akipigia debe suala la mkataba wa bandari.

Ndani ya CCM ajenda hii ni ya Chongolo na watu wake wachache kama kweli ni jambo la Chama kwanini Kinana hazungumzi chochote kuhusu DP? Lakini hata Mwenyekiti mwenyewe wa CCM Samia ni wapi amewahi kutamka neno la kupigia debe DP? ukiona hivyo ujue hili dubwasha ni la watu wachache.

Soma hotuba ya Serikali ya Mwaka 2023/2024 kama utaona hata mstari mmoja unaozungumzia DP. ukimaliza hapo Msikilize Mstaafu Kikwete ameongea na vyombo vya habari siku za karibuni kama umemsikia amezungumza neno DP.

Ukifanya uchambuzi kwa kina utakubaliana nami kwamba Ishu ya DP ni ya watu wachache ila inataka kugeuzwa na kulazimishwa kwamba ni jambo la CCM. Wakati wana CCM wenyewe huku chini hawataki mkataba wa DP ila wanahitaji wawekezaji wa kuboresha na kuongeza mapato ya nchi.
 
Huu ndio Ushahidi ?

Binafsi hata kama mradi huu ungekuwa ni wa watanzania wote kwa madudu niliyoyasikia ningeupinga binafsi (yaani mimi peke yangu vs watanzania wote)

In that case let the record show kwamba Logikos hakubaliana na huu mkataba au mikataba yoyote ambayo ina USIRI sababu USIRI huu imekuwa ni kichaka cha kufichia madudu
 
Hili dili halifai kutetea, kujaribu kulitetea unatakiwa uwe chawa (usiwe na akili timamu) Kikwete na Kinana hawataki aibu ya kijinga, naona wameamua kuacha Steve Nyerere ndio asaidie kuelimisha JAMII
 
DP ameletwa na washamba tu ilitakiwa ainunue TICTS (Tz) kabla haijaboronga na automatically anaendelea na mkataba ule.

Haya mambo yanahitaji watoto wa mjini wenye uzoefu akina RA huyo DC kaja mjini na lori la matikiti.

NB: Waarabu huweka dau kubwa na ndiyo maana unamuona DP katapakaa duniani kama akina COSCO na PSA walionza 1960s ilhali yenyewe ni ya 2005 ni kwa kununua kampuni zenye mikataba tayari.
 
Mpaka sasa ukiusoma mchezo unagundua suala la DP ni la Chongolo na baadhi ya watu wake na sio dili la CCM kwa ujumla wake, mfano mdogo ni ziara ya Kinana tangu ameanza mikutano Rufiji, akaenda Kondoa na sasa yuko Manyara sijamsikia akipigia debe suala la mkataba wa bandari
Mmmmggh HAPANA HAPANA, twendeni SAWA, huu mchongo ni WA kwenu nyote, msitake kumtoa kafara MTU mmoja, HAPANA hili zigo ni la kwenu
 
Jinsi wanavyosakamwa watafikia sehemu watalopoka bila kujua.Kila muhalifu huacha ushahidi,hata kama ni wa kutafuta kwa tochi, kwenye njia za uhalifu wake.Ni suala la kuwa makini tu na utambaini.
 
Mpaka sasa ukiusoma mchezo unagundua suala la DP World ni la Chongolo na baadhi ya watu wake na sio dili la CCM kwa ujumla wake, mfano mdogo ni ziara ya Kinana tangu ameanza mikutano Rufiji, akaenda Kondoa na sasa yuko Manyara sijamsikia akipigia debe suala la mkataba wa bandari.

Ndani ya CCM ajenda hii ni ya Chongolo na watu wake wachache kama kweli ni jambo la Chama kwanini Kinana hazungumzi chochote kuhusu DP? Lakini hata Mwenyekiti mwenyewe wa CCM Samia ni wapi amewahi kutamka neno la kupigia debe DP? ukiona hivyo ujue hili dubwasha ni la watu wachache.

Soma hotuba ya Serikali ya Mwaka 2023/2024 kama utaona hata mstari mmoja unaozungumzia DP. ukimaliza hapo Msikilize Mstaafu Kikwete ameongea na vyombo vya habari siku za karibuni kama umemsikia amezungumza neno DP.

Ukifanya uchambuzi kwa kina utakubaliana nami kwamba Ishu ya DP ni ya watu wachache ila inataka kugeuzwa na kulazimishwa kwamba ni jambo la CCM. Wakati wana CCM wenyewe huku chini hawataki mkataba wa DP ila wanahitaji wawekezaji wa kuboresha na kuongeza mapato ya nchi.DP
DPW ni deal la sa100 na wanawe
 
Back
Top Bottom