Wingawinga
JF-Expert Member
- Oct 31, 2021
- 623
- 1,531
- Thread starter
-
- #61
Mimi hapo kuna Jam , yai na chai ya maziwa , ile TanBong nilikuwa siipendi na kipindi hicho sija jua Milo , nilikuwa ninadhani Milo ni kahawa na nilikuwa sipendi kahawa so Milo nilikuwa siitaki kabisa, ila baadae ndio nika ijua kumbe Milo ni tamu lolNdioππ, Mimi nilikuwa nakunywa na chai kwa style ya kuiloweka kwenye chai πππ
Na Jumapili ilikuwa ni kuanzia saa 8 ni marufuku kuendesha gari. Kuendesha gari Jumapili baada ya saa 8 ilitakiwa uwe na kibali.Yes ili kuwa juma pili gari zilikuwa haziruhusiwi.
Hata sisi ilikuwa inakuja asubuhi tena habari zina sambaa kwamba ime fika , huseboy aichelew nakua imeisha .Ilikuwa inagombaniwa sana jamani, tena huku kwetu ilikuwa inakuja asubuhi
Nakumbuka hiyo baba yangu ilikuwa na shusha wa gen alipo paswa warudisha majumbani kwo baada ya kuja kutusaliia nyumbani juma pili pale Kenyatta Dr, wate,bee hadi Upanga ,ili asikamatwe na police hapo Slender Bridge.Na Jumapili ilikuwa ni kuanzia saa 8 ni marufuku kuendesha gari. Kuendesha gari Jumapili baada ya saa 8 ilitakiwa uwe na kibali.
Hilo ndio nina hisi na ndio maana haipo tena sababu market yake haipo tena sababu kunamikate bora kila sehemu.Kipindi hicho mikate ilikuwa adimu sana kama zilivyokuwa bidhaa nyingi. Mikate mingi ilikuwa inaokwa kwenye bakery ndogo ndogo za mtaani ila mikate ya siha ilikuwa inaongoza kwa ubora. Kwa sasa hivi bila shaka itaonekana ni mikate ya kwaidia tu kwani kuna mikate mingi yene ubora.
Siyo kama inawezekana ila ndiyo ukweli. Bidhaa nyingi zilikuwa adimu na hakukuwa na uchaguzi. Ukienda bar hakuna choice ya bia. Kama inatembea safari basi ni bar yote tena unaipata kama unajulikana. Kulikuwa na sehemu zinaitwa ''stoo bubu''. Hizi ni sehemu ambazo ulikuwa unaingia iwapo unajulika na kunywa bia. Mara nyingi ilikuwa ni vyumba vya kupanga na wauzaji wengi walikuwa wanawake. Ukienda ndani unaagiza kiasi kama tatu unaweka miguuni kwako kwa sababu muda wowote zilikuwa zinaweza kuisha.Asante , hilo ndio nilikuwa nina hisi, inawezekana sio kwamba ilikuwa ya ajabu sana ila tuu choices ya different dreads tulikuwa hatuna , ina wezekana ni kama hii hii ya sasa ila tuu kipindi hicho kama unavyosema ni hali ya kiuchumi,sababu najiuliza kama ilikuwa mitamu kihivyo kwanini haikuendelezwa ?
Wow, kumbe ilipatikana mpaka miaka ya 87/88? mawazo yangu labda ilikwisha huko miaka ya 84, sikumbuki ,sante kwa taarifa.Duh umenikumbusha mbali sana miaka 1987,88 nilikuwa nauza hiyo mikate maeneo ya Buguruni Relini nilikuwa na brother mmoja anaitwa Koba ( jina la utani Wamizoga)
Huyo brother alikuwa anapenda sana kununua mikate ya jana (ndaza) au ile iliotoka na sura mbaya ni nadra sana sisi kununua ya leo leo maana hiyo tulikuwa tunapata kwa bei ndogo
Mikate hiyo tulikuwa tunanunua hapo kiwandani NMC panatizamana na Tazara na tunauza hapo Buguruni Relini kwa bei ya jumla na rejareja
Salender Bridge ilikuwa ni sehemu mbaya sana sana kwa traffic polisi kukamata magari. Ukipita pale salama basi unashukuru Mungu.Nakumbuka hiyo baba yangu ilikuwa na shusha wa gen alipo paswa warudisha majumbani kwo baada ya kuja kutusaliia nyumbani juma pili pale Kenyatta Dr, wate,bee hadi Upanga ,ili asikamatwe na police hapo Slender Bridge.
dah , sikuwahifikiria kwanini watu walikuwa na story za kunua case na kuweka chini ya miguu, nilidhani ni ubishoo, kumbe ilikua uadimu wa vinywaji , asisee nilikuw amdogo kipindi hicho vitu vingi nilikuwa sivielewi ila ninaviona .Siyo kama inawezekana ila ndiyo ukweli. Bidhaa nyingi zilikuwa adimu na hakukuwa na uchaguzi. Ukienda bar hakuna choice ya bia. Kama inatembea safari basi ni bar yote tena unaipata kama unajulikana. Kulikuwa na sehemu zinaitwa ''stoo bubu''. Hizi ni sehemu ambazo ulikuwa unaingia iwapo unajulika na kunywa bia. Mara nyingi ilikuwa ni vyumba vya kupanga na wauzaji wengi walikuwa wanawake. Ukienda ndani unaagiza kiasi kama tatu unaweka miguuni kwako kwa sababu muda wowote zilikuwa zinaweza kuisha.
Hahahahahahaha nakumbuka hilo , police walikua pale na enzi hizo kutoa rushwa ni ngumu na huwezi tumai mabavu kusema Mimi ni fulani .Salender Bridge ilikuwa ni sehemu mbaya sana sana kwa traffic polisi kukamata magari. Ukipita pale salama basi unashukuru Mungu.
Inawezekana hiyo .Hadi sasa hapa nchini hakuna mkate wenye viwango vya SIHA
HIyo ina weekana kabisa, quality ya vitu vingi imehuka sana , ina wezekana na hii moja wapo, sasa sijui kwanini hakuna mjanja aliyejaribu mimicking the recipe , hata kwa alio kuwa kwenye kitengo cha kuchanganya mazaga zaga , ili kitoke kitu kifananae na original kwa namna fulani , maana kama kweli ilikuwa na utofauti kihivyo basi ikija now itakua a big hit kwanye bakary industry .Watu wa zamani walieliimika. Kwa sasa mkate wa Baharesa na super roof halina viwango, ndiyo maana tumeachie ugali uendelee. Hawana wapishi wenye viwango hadi serikali itakapo anzisha ushindani na viwanda vya mikate vya Ulaya.
Mikate ya Siha ilikuwa inatengenezwa na NMC pale Tazara, bekari alipewa AZAM na hstujui mitambo aliipeleka wapi, huenda viongozi wa CCM wanajua kwani ndio waliohujumu viwanda na makampuni yote isipokuwa cha majani ya chai tu.Kwa wale wahenga wenzangu wa Oysterbay na Masaki, mnakumbuka kipindi cha miaka ya 80, pale Morogoro stores, kulikuwa na duka lina uza Mikate ya Siha, kipindi hicho niko mdogo sana sikumbuki vizuri ila ninachokumbuka kama vile ilikuwa inapaikana mara moja kwa week na kulikua kama inagombewa.
Sijui sababu haswa ilikuwa ni nini kugombewa kihivyo na kwanini ilipatikana mara moja kwa weeki na je, Mkate wa Siha ulikuwa mkate unatengenezwa kwa nini haswa, sababu ulikuwana utamu a aina yake.
UPDATE.
Leo nime tambua jambo kuhusu MIkate ya Siha, siku zote nilidhani ni Mikate toka kwnye Bakery moja ndogo ya binafsi in Oysterbay na ndio ilikuwa ina bake hiyo mikate kwa ajili ya wateja wakazi wa Masaki, Oyesterby na Masasani na ndio maana nikasema Wahenga enzangu wa Masaki ana Oysterby ,sababu tulinunua hapo Morogoro stores in Oysterbay ( Pale ilipoPale maeno ya ilipo kuwa Maisha Club kwa wasio tambua Morogoro stores ) kumbe sivyo , Mikate ilikua Populary sehemu kubwa ya Tanania
Itabidi tuwahoji why wamefanya Chai isiwe fun kama zamani . lolMikate ya Siha ilikuwa inatengenezwa na NMC pale Tazara, bekari alipewa AZAM na hstujui mitambo aliipeleka wapi, huenda viongozi wa CCM wanajua kwani ndio waliohujumu viwanda na makampuni yote isipokuwa cha majani ya chai tu.
Ikarius nimeipanda sana lile roli aisrr lilikuwa likipita sehem kama ni posta likipita panabakia peupeeee, halikuwa na ruti maalumNakumbuka Ikarus na mabasi ya Kamata, mabasi ya kamata yalikuwa hayo yalipita nje ya nyumbani kwetu , kipindi hicho niko mdogo , hausgeli wetu alikua ana penda kunitisha kama nilileta utundu kwamba ata niletea basi la Kamata nilinakate na nilikuwa na uoga mkubwa nikiona basi la Kamata.
Mabasi ya Ikarus nilikuwa ninayaona mjini zaidi ,kununua unga NMC hiyo sikumbuki vizuri ,pia nakumbuka mzee wangu siku ya Jumapili alikua haweze endesha gari, nadhani serikali ili zuia sababu ya ku save mafuta , tulikuwa na marafiki wa mzee wangu wanaishi Upanga, hivyo alikuwa akiwarudisha nyumbani kama wamekuja kututembelea nyumbani Jumapili ,basi alikuwa ana wafikisha mpaka maeneo ya Kenyatta Dr , pale wana shuka na kuetmbea kwenda Upanga sababu ukifika Slender Bridge gari ingekamatwa .
Sahihi kabisa, ilikuwa inatengenezwa na NMC (National Milling Cooperation),ambalo lilikuwa shirika la umma. Yaani hiyo mikate ilikuwa mizuri mnoo (kwa sasa naweza kuilinganisha kwa mbaali na mkate wa SUPER LOAF [emoji506] from Kenya). Enzi hizo nikiwa Mburahati NHC ukiokota coins unaenda kununua Mkate wa Siha nusu na paketi ya maziwa ya KCC... Hawa NMC walikuwa wana magodown makubwa ya nafaka, bakeries etc kiukweli sijajua mambo yalikuja kuharibika kwa kweli...Siha maana yake ni afya njema, huo mkate ulikua ni wa NMC nadhani
Kula chuma hapo chini
Hii ni dedication kwetu sisi wahenga
Habari za jioni wana JF Imetokea nikapata tafakari (reminisce) utamu wa maisha yetu ya kale. Pale ambapo ulikua unajiandaa kwenda shule asubuhi, kwa mbaali unasikia kipindi cha "mazungumzo baada ya habari" kikiendeshwa na Marehemu David Wakati. Unachukua begi lako pamoja na ufagio wako wa...www.jamiiforums.com